Mbeya: Afisa Mtendaji kizimbani kwa kuomba na kupokea rushwa ya TZS 200,000

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,280
Afisa Mtendaji Kata ya Lusungo, Bw. Edestus Clemence Ndunguru, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya kwa shtaka la kuomba na kupokea Rushwa ya TZS 200,000/= ili amsaidie mwananchi kuongea na askari polisi waweze kumpa dhamana katika Kituo cha Polisi Ipinda.

Akisoma shtaka katika kesi hiyo ya Jinai Na. 2946/2024 mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Mhe. A. S. Njau na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Wakili Sospeter Tyeah alisema, kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na 11 ya Mwaka 2007

MSHTAKIWA ALIKANA KOSA HILO na alipelekwa mahabusu baada ya kukosa dhamana kwa kutokutimiza masharti ya dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 20, 2024 ambapo mshtakiwa atasomewa hoja za awali(phg)
 
Maskini Tanzania yangu,mafisadi yanakula hela ndefu za nchi,chombo cha kuyadhibiti kipo bize na watendaji wa kijiji na rushwa za 200000.
Tukubaliane tu kuwa ukiona TAKUKURU wamekupeleka mahakamani ujue hujafika nao dau.
 
Afisa Mtendaji Kata ya Lusungo, Bw. Edestus Clemence Ndunguru, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya kwa shtaka la kuomba na kupokea Rushwa ya TZS 200,000/= ili amsaidie mwananchi kuongea na askari polisi waweze kumpa dhamana katika Kituo cha Polisi Ipinda.

Akisoma shtaka katika kesi hiyo ya Jinai Na. 2946/2024 mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Mhe. A. S. Njau na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Wakili Sospeter Tyeah alisema, kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na 11 ya Mwaka 2007

MSHTAKIWA ALIKANA KOSA HILO na alipelekwa mahabusu baada ya kukosa dhamana kwa kutokutimiza masharti ya dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 20, 2024 ambapo mshtakiwa atasomewa hoja za awali(phg)
ashughulikiwe kwa adhabu kali zaidi, ikithibitika pasina shaka ametenda kosa hilo ili iwe fundisho kwa watumishi wengine wenye tamaa na wasio waaminifu...

R.I.P Laigwanan comrade ENL
 
Back
Top Bottom