Watu wengi wana hofu na GMOs kwa vigezo tofauti lakini vinavyojitokeza mara kwa mara ni kama:
Usalama wa GMOs katika matumizi ya chakula: Wengi hujiuliza hivi GMOs zipo salama kwa kula? Mara nyingi hili swali hujitokeza hasa kama kinasaba (gene) imetoka kwa kiumbe kingine zaidi ya mmea (non-plant origin). Wanaoleta hoja hii waelewe kwamba a gene is just a gene. Iwe imetoka kwa mnyama au mmea DNA ni molecule na ina tabia ile ile. Hoja isiwe ni gene kutoka wapi, bali umuhimu wa hiyo gene katika matumizi ya binadamu au mnyama. Kama regulatoy body imejiridhisha vya kutosha kuwa ni salama, tatizo liko wapi tena?
Madhara katika mazingira (ekolojia). Mara nyingi transgenes (GMOs) huwa na vigour yaani zina nguvu kuliko mazao ya asili. Na kuna hofu ya kimsingi kabisa kwamba transgene inaweza kusambaa kwa kasi hadi kufutilia mbali mazao ya asili. Lakini hilo linazuilika lakini kuna mbinu za kisayansi za kuvuka kikwazo hicho. Kwa mfano unaweza kuisolate transgenes (yaani kuyalima kwenye maeneo tengefu maalumu) lakini kisayansi unaweza kupandikiza gene yako kwa eneo maalumu katika cell ya mmea isyohusika na reproduction na hivy kuondoa shaka la kusambaa kwa transgene weed.
Kwamba transgene ni hatari zinaweza kuua viumbe vingine. Na mfano utolewao na wapinzani wa GMOs ni monarch butterflies katika jaribio kwenye maabara moja huko chuo kimoja Marekani (Cornell University) ambapo wanasayansi waliwalisha vipepeo hao transgene food lakini waliwalisha zaidi ya chakula chao cha kawaida. Chakula hicho ilikuwa ni pollen za mahindi ya GMOs na kwa vile hao vipepeo walikufa zaidi (statistically, by the way). Hiyo experiment kwanza ilikuwa na agenda. Kwanini uwape vipepeo hao chakula zaidi ya mlo wao wa kawaida? Na kama ni kuonyesha madhara ya GMOs kwa viumbe vingine, tunasahau kwamba huko Marekani winter moja huua zaidi ya vipepeo milioni 10 kila mwaka.
Hoja ninayoiona humu JF ni kwamba kwani ni lazima tutumie GMOs? Hoja hii mara nyingi hutumiwa na wapinzani wa GMOs kwa kulipa sura ya upebari wa kimagharibi (mf. Mosanto) kujipa utajiri kwa mgongo wa nchi masikini kama Tanzania. Lakini tunasahau kwamba kama kigezo ni ubepari wa kimagharibi, hao hao wa Magharibi ndio hao wanatengeza minoti ya kufa mtu kwa kutuuzia agrochemicals zinazoharibu mazingira balaa, kuliko inavyoweza kufikirika kwa matumizi ya GMOs. Wachina na India walikuwa masikini kama sisi, Ilakini kwao siasa linapokuja swala la kufa na kupona kama ishu ya kilimo, siasa huziweka kando.
La mwisho kwa sasa ni hii kitu yako GMOs versus organic and green. Hii ndio siasa kabisa. Mbona hatukukataa unga wa Yanga? Wazambia walipokata unga wa US eti ni mahindi ya GMO, njaa ilipokaba wakala, kwani walikufa? Waafrika siasa zisaidie sayansi, siyo kupinga sayansi.