Mbegu za GMO ni Siasa Chafu!

Mbegu za GMO ni Siasa Chafu!

Kwa mazingira fulani fulani, GMO ni necessary lakini kwa Tanzania bado hakuna umuhimu mkubwa wa matumizi ya GMO. Vyovyote iwavyo, lengo kuu la GMO ni kuongeza tija/productivity...unit production per every unit of land. Swali la kujiliza hapa ni je, Tanzania hakuna mazingira mengine yanayowezesha kuongeza uzalishaji badala ya matumizi ya GMO?! Wakulima wanapata mavuno kidogo wakati mwingine kutokana na jua....kumbe hapo suluhisho si GMO bali kufanya kilimo cha umwagiliaji!

Wakulima wengine huwa wanapata mavuno haba kwa sababu tu ardhi haina rutuba; kumbe hapo suluhisho si GMO bali matumizi sahihi ya mbolea au kile kinachoitwa good agromechanical activities! Wakati mwingine(kawaida sana hii) wakulima wanapata mavuno haba kwa sababu tu wanalima vishamba vidogo vidogo....kumbe hapo solution wala si GMOs, bali matumizi ya trekta yatakayowawezesha kulima maeneno makubwa!

Wakati mwingine wakulima wanapata mavuno haba kwa ajili tu ya wadudu; kumbe suluhisho hapo wala si matumizi ya GMOs bali matumizi sahihi ya dawa za kuulia wadudu waharibu! Mifano ipo mingi ambayo kwa mazingira ya Tanzania utaona kwamba suluhisho la matatizo yote hayo wala si matumizi ya GMO bali matumizi ya kilimo bora!

Tanzania ni nchi yenye ardhi ya kutosha ambayo wala haijatumika ipasavyo hivyo si sahihi hata kidogo kuona GMO ndio suluhisho la kilimo chetu wakati hata zule njia za kawaida za kilimo salama hatujazitumia! Tanzania kuna source ya kutosha ya maji inayowezesha umwagiliaji na hivyo kuendelea kujikita na kilimo salama na bado tukaongeza uzalishaji maradufu ya sasa pasipo na matumizi ya GMO.

Ingawaje ni kweli pia linapokuja suala la GMO watu huwa wanakuza sana mambo lakini ukweli bado utabaki pale pale kwamba though GMO sometimes is necessary but there's no sufficient condition for country like Tanzania kuamini katika GMO.
 
babayah67 ninawasiwasi kama kweli umeshabobea vizuri kwenye hii fani mpaka unatoa a strong conclusion kama hii. Kwataarifa yako Marekani wanaathirika sana na hili janga la GMO. Pia licha ya kuleta madhara kwenye kuharibu genetic resources za asili, it has been proved scientifically kwamba kuna modifications nyingine zinaleta athari kubwa kwenye miili ya binadamu na viumbe wengine. Unaweza tafuta scientific findings kwenye hili, kama utashindwa kuzipata naweza kukusaidia kukutafutia baadhi. Nami pia nipo eneo hili na ni kweli nimedhibitisha haya niliyoandika hapa.

Nitashukuru ukinitumia hizo fact
 
Last edited by a moderator:
Iko hivi makampuni ya GMO yanaanda hizo mbegu kisha wanaandaa na sumu za kudhibiti mfano magugu na kisha binadamu akiathirika aidha kwa sumu hiyo au mazao yaliyozalishwa, makampuni hayo pia ndiyo yenye shares kubwa kwenye pharmaceutical industry. Hivyo unaweza kuona ni jinsi gani inavyohitaji akili ya ubinafsi kuikubali GMO.
 
na EU wana fear of the unknown??

EU wanatumia Sana tu GM foods Siku nyingi. Kama ushafika moja ya nchi za EU utakuwa ushashuhudia watermelon hazina seeds. ni GM food hiyo. Usisahau nyanya na Canola oils.
 
MaCCM kwa akili zao hizi za sembe..wataona ni dili tuu....monsato ndio shetwani mkuwa...tupo Arusha,kilimanjaro ,manyara etc..shamba yangu ya mahindi Moshi nimekuta mahindi yamechukua mbegu za hao jamaa..ukilima mara moja yanatoa mbegu..nyepesi sana na isiyotakiwa ota tena.

Jamaa eti wana patent hadi ktk genes za binadamu.
 
EU wanatumia Sana tu GM foods Siku nyingi. Kama ushafika moja ya nchi za EU utakuwa ushashuhudia watermelon hazina seeds. ni GM food hiyo. Usisahau nyanya na Canola oils.

wanatumia GMO foods sawa, lakini wazalisha chakula chao kwa GMO? may be yes? wanaipinga GMO hilo ni swali lingine kabisa.
 
Iko hivi makampuni ya GMO yanaanda hizo mbegu kisha wanaandaa na sumu za kudhibiti mfano magugu na kisha binadamu akiathirika aidha kwa sumu hiyo au mazao yaliyozalishwa, makampuni hayo pia ndiyo yenye shares kubwa kwenye pharmaceutical industry. Hivyo unaweza kuona ni jinsi gani inavyohitaji akili ya ubinafsi kuikubali GMO.

Its all business for real...hawa watu kila kitu wanataka kiwe ni biashara. Watanzania tuko nyuma kdogo kwa teknolojia ila SISI SIO WAJINGA na lazima wajue!
 
babayah67 ninawasiwasi kama kweli umeshabobea vizuri kwenye hii fani mpaka unatoa a strong conclusion kama hii. Kwataarifa yako Marekani wanaathirika sana na hili janga la GMO. Pia licha ya kuleta madhara kwenye kuharibu genetic resources za asili, it has been proved scientifically kwamba kuna modifications nyingine zinaleta athari kubwa kwenye miili ya binadamu na viumbe wengine. Unaweza tafuta scientific findings kwenye hili, kama utashindwa kuzipata naweza kukusaidia kukutafutia baadhi. Nami pia nipo eneo hili na ni kweli nimedhibitisha haya niliyoandika hapa.

Jamani mbona Phenomenon ya genetic mix-up of closely related species ipo in nature? Bila hiyo hatuna Evolution ambao ndio msingi wa succession of generation
 
Last edited by a moderator:
Watu wote wanaopinga uzalishaji wa GMO hufanya hivyo, siyo kwa basis zozote za kisayansi, bali kwa mwendelezo ule ule wa siasa za wabongo --maneno mengi bila ukweli.

Nina ujuzi wa msingi kuhusu biotech (nimesomea na ninafanya utafiti) hivyo nahisi naweza kuchangia kwa namna ninavyofahamu:

Kwanza, ni kushindwa kusoma historia ya mabadiliko ya technolojia katika uzalishaji wa chakula kutakakoifanya Afrika --ikiwemo Tanzania--tuendelee kubaki nyuma katika kila nafasi inayopatikana ya kusukuma kilimo chetu mbele.

Wakati mapinduzi ya kijani (green revolution) yaliposhika moto, wazungu wakiwa busy kulima kijanja (umwagiliaji wa kisasa, kutumia mbegu bora --improved varieties, mechanized agriculture, etc), sisi tulikuwa busy kufanya siasa. Green revolution ikatupita kando, kilimo kikapuuzwa kisiasa na kiutamaduni. Njaa ilipopiga, unga wa Yanga ulipoletwa kama msaada kutoka USA, hakuna aliyeuliza unga umepatikanaje. Ilikuwa ni kunusuru maisha, maulizo baadaye. Zama hizi ndo tunastuka na siasa za vilimo kwanza kwa kutumia mbinu za kizamani kweli zilizozalisha unga wa Yanga USA.

Achaneni na siasa, wekezeni katika biotech kama tunataka kutoka katika kilimo. Mabadilko ya rutuba ya ardhi, spidi ya ongezeko la watu duniani, mahitaji ya ubora wa uzalishaji katika kilimo cha biashara, yote haya yatategemea ni namna gani sayansi ya GMO inaendelezwa.

Sijaona ni namna gani madhara ya GMO yanazidi faida zake. Tukiacha kutumia GMO kwa kisingizio cha ekolojia, tayari pestcides zimeshaharibu mazaingira ya ardhi zetu beyond recovery. Kwa nini sasa usilime pest resistance variety badala ya kutumia pestcides?

Kama ni kusingizia madhara kimwili, toa ushahidi. Watu kila siku wanakula GMOs (apples kutoka south africa, mchele kutoka Thailand, vyote hivyo ni imported), lakini linapokuja swala la kuwahimiza wakulima wetu walime wenyewe hizo GMO ili waweze kushindana, debates za siasa zinaanza bungeni. Raia gani sisi?
 
EU wanatumia Sana tu GM foods Siku nyingi. Kama ushafika moja ya nchi za EU utakuwa ushashuhudia watermelon hazina seeds. ni GM food hiyo. Usisahau nyanya na Canola oils.

Wanatumia sana tunajua..ila pamoja na hayo wamegundua kwamba zina matatizo na ndio mana wanazipiga vita sana, na kwa hilo wanatusaidia pia sisi ambao tulikua hatujaingia huko tujue matatizo na tuweze kubadili mwelekeo while its still early!
 
MaCCM kwa akili zao hizi za sembe..wataona ni dili tuu....monsato ndio shetwani mkuwa...tupo Arusha,kilimanjaro ,manyara etc..shamba yangu ya mahindi Moshi nimekuta mahindi yamechukua mbegu za hao jamaa..ukilima mara moja yanatoa mbegu..nyepesi sana na isiyotakiwa ota tena.

Jamaa eti wana patent hadi ktk genes za binadamu.

Mkuu haya uliyoyasema ni matokeo ya watu kushindwa kusimamia nafasi zao...wanaanza taratibu kutunyonga ili tukishakosa kabisa mbegu ndio watuletee makapi yao!
 
Watu wote wanaopinga uzalishaji wa GMO hufanya hivyo, siyo kwa basis zozote za kisayansi, bali kwa mwendelezo ule ule wa siasa za wabongo --maneno mengi bila ukweli.

Nina ujuzi wa msingi kuhusu biotech (nimesomea na ninafanya utafiti) hivyo nahisi naweza kuchangia kwa namna ninavyofahamu:

Kwanza, ni kushindwa kusoma historia ya mabadiliko ya technolojia katika uzalishaji wa chakula kutakakoifanya Afrika --ikiwemo Tanzania--tuendelee kubaki nyuma katika kila nafasi inayopatikana ya kusukuma kilimo chetu mbele.

Wakati mapinduzi ya kijani (green revolution) yaliposhika moto, wazungu wakiwa busy kulima kijanja (umwagiliaji wa kisasa, kutumia mbegu bora --improved varieties, mechanized agriculture, etc), sisi tulikuwa busy kufanya siasa. Green revolution ikatupita kando, kilimo kikapuuzwa kisiasa na kiutamaduni. Njaa ilipopiga, unga wa Yanga ulipoletwa kama msaada kutoka USA, hakuna aliyeuliza unga umepatikanaje. Ilikuwa ni kunusuru maisha, maulizo baadaye. Zama hizi ndo tunastuka na siasa za vilimo kwanza kwa kutumia mbinu za kizamani kweli zilizozalisha unga wa Yanga USA.

Achaneni na siasa, wekezeni katika biotech kama tunataka kutoka katika kilimo. Mabadilko ya rutuba ya ardhi, spidi ya ongezeko la watu duniani, mahitaji ya ubora wa uzalishaji katika kilimo cha biashara, yote haya yatategemea ni namna gani sayansi ya GMO inaendelezwa.

Sijaona ni namna gani madhara ya GMO yanazidi faida zake. Tukiacha kutumia GMO kwa kisingizio cha ekolojia, tayari pestcides zimeshaharibu mazaingira ya ardhi zetu beyond recovery. Kwa nini sasa usilime pest resistance variety badala ya kutumia pestcides?

Kama ni kusingizia madhara kimwili, toa ushahidi. Watu kila siku wanakula GMOs (apples kutoka south africa, mchele kutoka Thailand, vyote hivyo ni imported), lakini linapokuja swala la kuwahimiza wakulima wetu walime wenyewe hizo GMO ili waweze kushindana, debates za siasa zinaanza bungeni. Raia gani sisi?

Hivi umewahi kukaa chini na kjiuliza ukubwa wa nchi yetu na kiasi hadi sasa kinalimwa? Unajua ni kwa nini tunazalisha kwa kiasi kidogo?

Hivi Kama serikali ingeweke miundombinu mizuri watu wangetawanyika na wangelima mara kumi ya sasa! Hapa nazungumzia miundombinu ya umwagiliaji, barabara, mabwanashamba nk.

Kwanini sasa unatakakutuaminisha kuwa kuna less productivity hapa nchini?

Kuna madhara mengi sana naomba upitie kwenye comments zangu hapo juu na leo hii nenda kwenye yahoo news uone jinsi wakulima wa marekani wanavyolia juu ya weedresistance!
 
Ndg.kuna wanasayansi wachache wanaolipwa kwenye miradi inayofadhiliwa na hayo makampuni ndo wanaopigia upatu GMO kwa Tanzania mf. Dr. Kulaya amestaafu ARI Mikocheni na Dr. Roshani Abdallah atakuwa amestaafu TPRI Arusha. Kifupi Mh. RAIS amekataa kurithia mpango wa kubadilisha kinachoitwa strictly liability ambacho ni kipengele kilichokuwa kinataka kuwanusuru pro GMO kama madhara yatajitokeza kutokana na GMO. Kifupi GMO kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla haifai

Typical. Siyo kweli kwamba kuna motives za kifedha kwa wanasayansi kuadvocate GMO. Kwa taarifa yako kelele kuhusu GMO zinafadhiliwa na makampuni makubwa ya kuzalisha mbolea za viwandani na agrochemicals maana wanahisi GMOs ni kitisho kwa biashara zao.

Kule ulaya GMO is not a big deal, lakini wenzako ni wajanja. Serikali, wanasayansi na national laboratories za ulaya hazipuuzi GMOs katika mfumo wa utafiti --zinatengwa budget ya kutosha kuhakikisha tafiti za GMO zinafanywa na breeds zinazopatikana zinatunzwa vyema mpaka pale itakapohitajika.

Afrika ni tofauti. Hivi kwa ule ukame wa Ethiopia inaleta akili kuwazuia wahabesh wasilime GMO ambayo ni drought resistant? Kweli mwenye shibe hamjali mwenye njaa.
 
Watu wote wanaopinga uzalishaji wa GMO hufanya hivyo, siyo kwa basis zozote za kisayansi, bali kwa mwendelezo ule ule wa siasa za wabongo --maneno mengi bila ukweli.

Nina ujuzi wa msingi kuhusu biotech (nimesomea na ninafanya utafiti) hivyo nahisi naweza kuchangia kwa namna ninavyofahamu:

Kwanza, ni kushindwa kusoma historia ya mabadiliko ya technolojia katika uzalishaji wa chakula kutakakoifanya Afrika --ikiwemo Tanzania--tuendelee kubaki nyuma katika kila nafasi inayopatikana ya kusukuma kilimo chetu mbele.

Wakati mapinduzi ya kijani (green revolution) yaliposhika moto, wazungu wakiwa busy kulima kijanja (umwagiliaji wa kisasa, kutumia mbegu bora --improved varieties, mechanized agriculture, etc), sisi tulikuwa busy kufanya siasa. Green revolution ikatupita kando, kilimo kikapuuzwa kisiasa na kiutamaduni. Njaa ilipopiga, unga wa Yanga ulipoletwa kama msaada kutoka USA, hakuna aliyeuliza unga umepatikanaje. Ilikuwa ni kunusuru maisha, maulizo baadaye. Zama hizi ndo tunastuka na siasa za vilimo kwanza kwa kutumia mbinu za kizamani kweli zilizozalisha unga wa Yanga USA.

Achaneni na siasa, wekezeni katika biotech kama tunataka kutoka katika kilimo. Mabadilko ya rutuba ya ardhi, spidi ya ongezeko la watu duniani, mahitaji ya ubora wa uzalishaji katika kilimo cha biashara, yote haya yatategemea ni namna gani sayansi ya GMO inaendelezwa.

Sijaona ni namna gani madhara ya GMO yanazidi faida zake. Tukiacha kutumia GMO kwa kisingizio cha ekolojia, tayari pestcides zimeshaharibu mazaingira ya ardhi zetu beyond recovery. Kwa nini sasa usilime pest resistance variety badala ya kutumia pestcides?

Kama ni kusingizia madhara kimwili, toa ushahidi. Watu kila siku wanakula GMOs (apples kutoka south africa, mchele kutoka Thailand, vyote hivyo ni imported), lakini linapokuja swala la kuwahimiza wakulima wetu walime wenyewe hizo GMO ili waweze kushindana, debates za siasa zinaanza bungeni. Raia gani sisi?

Mbona mnatuuzia uwoga mjini kwa kuleta sera za kusomea?, au mnafikiri bcoz wengine tumecomment bila kuelezea educational background zetu basi tutakua tunabishana bila ya facts?. We unatuletea historia ya unga wa njano..kwa hiyo kama makosa yalifanyika kutokana na kutokua na info za kutosha kuhusu madhara ya GMO ndo unataka kujustify kwamba hazina madhara?.Pitia vizuri comment ya NasDaz hapo juu itakuboost fikra zako into another dimension.
 
Bugorobi mimi nashindwa kabisa kumwelewa huyo mtu..anasema ardhi imeharibika beyond recovery sijui hizo takwimu kazitolea wapi...the last time I checked ni robo tu ya ardhi ya Tanzania imetumika sasa sijui yy anatolea wap hzo facts zake
 
Hivi umewahi kukaa chini na kjiuliza ukubwa wa nchi yetu na kiasi hadi sasa kinalimwa? Unajua ni kwa nini tunazalisha kwa kiasi kidogo?

Hivi Kama serikali ingeweke miundombinu mizuri watu wangetawanyika na wangelima mara kumi ya sasa! Hapa nazungumzia miundombinu ya umwagiliaji, barabara, mabwanashamba nk.

Kwanini sasa unatakakutuaminisha kuwa kuna less productivity hapa nchini?

Kuna madhara mengi sana naomba upitie kwenye comments zangu hapo juu na leo hii nenda kwenye yahoo news uone jinsi wakulima wa marekani wanavyolia juu ya weedresistance!

Kwa nini unatumia kipengele kimojawapo cha madhara ya ekolojia (weed competitiveness) kama kigezo cha kuminya matumizi ya GMO? Wanasayansi tayari washajua siku nyingi sana kwamba GMO tends to outcompete natural varieties hivyo matumizi yake ni lazima yazingatie uangalifu. Na kimsingi kuna regulatory body (USFDA) US Food and Drug Admnistration ambayo inahusika kuruhusu au kutoruhusu matumizi ya GMO. Ikisharuhusiwa ujue haina madhara.

Ukiona mtu anaanza kusema mbona tuna ardhi kubwa, kwani serikali imeshindwa hivi na vile, miundo mbinu....ujue huyo ni mwanasiasa.

Tuna ardhi kubwa ndiyo lakini kilimo chetu ndo hivyo. Watu hatusubiri kufa kwa njaa na ndo maana wanasayansi wetu hawapotezi muda na maneno maneno yasiyo na vitendo. It is a vital opportunity and we cannot afforod to lose it.
 
NasDaz

Argument yako ni kama vile sahihi lakini unaposema "lakini ukweli bado utabaki pale pale kwamba though GMO sometimes is necessary but there's no sufficient condition for country like Tanzania kuamini katika GMO" hiyo ni sentensi unayoweza kuikuta kwenye brochures za wapinzani wa GMO kibiashara.

Ukweli ni kwamba GMO advocates hawasemi kwamba mbegu za asili zisitumike badala yake zitumike GMOs. Wao wanasema iwapo traditional agriculture isipojitosheleza GMO inaweza kuwa ukombozi.

Na kwa mazingira ya Afrika ni muhimu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa nini unatumia kipengele kimojawapo cha madhara ya ekolojia (weed competitiveness) kama kigezo cha kuminya matumizi ya GMO? Wanasayansi tayari washajua siku nyingi sana kwamba GMO tends to outcompete natural varieties hivyo matumizi yake ni lazima yazingatie uangalifu. Na kimsingi kuna regulatory body (USFDA) US Food and Drug Admnistration ambayo inahusika kuruhusu au kutoruhusu matumizi ya GMO. Ikisharuhusiwa ujue haina madhara.

Ukiona mtu anaanza kusema mbona tuna ardhi kubwa, kwani serikali imeshindwa hivi na vile, miundo mbinu....ujue huyo ni mwanasiasa.

Tuna ardhi kubwa ndiyo lakini kilimo chetu ndo hivyo. Watu hatusubiri kufa kwa njaa na ndo maana wanasayansi wetu hawapotezi muda na maneno maneno yasiyo na vitendo. It is a vital opportunity and we cannot afforod to lose it.

Kwa hiyo kwa sababu kilimo chetu ndio hvyo ww unaona suluhisho ni GMO au suluhisho ni kulima kwa tija kwa kutumia mbinu za kisasa ambazo zipo na hazihusishi GMO?
 
Kwa nini unatumia kipengele kimojawapo cha madhara ya ekolojia (weed competitiveness) kama kigezo cha kuminya matumizi ya GMO? Wanasayansi tayari washajua siku nyingi sana kwamba GMO tends to outcompete natural varieties hivyo matumizi yake ni lazima yazingatie uangalifu. Na kimsingi kuna regulatory body (USFDA) US Food and Drug Admnistration ambayo inahusika kuruhusu au kutoruhusu matumizi ya GMO. Ikisharuhusiwa ujue haina madhara.

Ukiona mtu anaanza kusema mbona tuna ardhi kubwa, kwani serikali imeshindwa hivi na vile, miundo mbinu....ujue huyo ni mwanasiasa.

Tuna ardhi kubwa ndiyo lakini kilimo chetu ndo hivyo. Watu hatusubiri kufa kwa njaa na ndo maana wanasayansi wetu hawapotezi muda na maneno maneno yasiyo na vitendo. It is a vital opportunity and we cannot afforod to lose it.

Kwa hiyo tunakosa kuzalisha kwa vile ardhi imearibika beyond recovery!!! Sijui hii data umeito wapi! siwezi kuweka vipengele vyote vyenye athari coz mimi naangalia kwa mazingira ya kwetu! Kuna athari nyingi za kiafya hapo mwanzo nimeongelea athari hizo check comments zangu kwenye uzi huu.

Regualatory body ya USA imezidia pamoja na kuruhu GMO zilizofanyawia tafiti bado sideeffect zimezidi faida, soma AFP news leo uone!

Huwezi kutenganisha siasa na maisha yetu ya kila siku! ninaposema hatuzalishi vyakutosha kwa vile serikali imeshindwa kuweka miundo mbinu ukaita siasa sijui tutaongea nini ambacho sio wansiasa wanachoamua! Leo hii nyinyi mnaojiita wanasayansi mnategemea maamuzi ya wanasiasa! SO GMO IS NOT THE WAY TO GO! ORGANIC ECOLOGICAL AGRICULTURE IS THE WAYFORWARD FOR OUR DEVELOPING NATIONS. PERIOD
 
Argument yako ni kama vile sahihi lakini unaposema "lakini ukweli bado utabaki pale pale kwamba though GMO sometimes is necessary but there's no sufficient condition for country like Tanzania kuamini katika GMO" hiyo ni sentensi unayoweza kuikuta kwenye brochures za wapinzani wa GMO kibiashara.

Ukweli ni kwamba GMO advocates hawasemi kwamba mbegu za asili zisitumike badala yake zitumike GMOs. Wao wanasema iwapo traditional agriculture isipojitosheleza GMO inaweza kuwa ukombozi.

Na kwa mazingira ya Afrika ni muhimu.

Dont try to fool us these two things can not live side by side!
 
Back
Top Bottom