Mbabe SATANA alikufa au bado yu hai?

Mbabe SATANA alikufa au bado yu hai?

Kwa wanaokumbuka miaka ya 80 kulikua na bwana akiitwa Santana. Huyu jamaa alikua mbabe sana akicheza karate. Kutwa nzima akishinda stendi za mabasi sanasana kituo cha manzese (msufini). Akiamua aliweza kupora chochote pasipo kufanywa chochote. Kuna wakati alisaidia wanafunzi kuingia kwenye mabasi makonda wakimuogopa kwelikweli. Ni zaidi ya miaka 25 sijamsikia tena
Watu wa dizaini hiyo huwa wanapotea na kuishia kifo na ndio kisa hajasikika
 
Abajalo vs Sinza star...
Friends ranger vs kagera ranger.
Messina vs Swazi inter
Bomu vs Ashanti
Beach boy vs friend ranger..
Abajalo vs sheki utd.
Sifa vs Faru dume.

Zikipigwa hizo game lazima mitaa ifungwe, na hapo ndipo utaona watu walivyopinda..
Hahahahaahahaa usinikumbishe mechi ya friends ranger uwanja mwananyamala B ngoma zilipigwa nikakimbia peku viatu soksi na t-shirt sikujua nilivivulia wapi mpaka nilipofika kwa alimaua
 
mainchamber derby lingine ilikuwa la msebenze vs ajaxpressure (mapusha)
Ngoma ikipigwa si la kitoto
Mechi moja wa shabiki walirusha sana vinyesi uwanjani

Ova
 
Hahahahaahahaa usinikumbishe mechi ya friends ranger uwanja mwananyamala B ngoma zilipigwa nikakimbia peku viatu soksi na t-shirt sikujua nilivivulia wapi mpaka nilipofika kwa alimaua
Mechi hzo refa kiuononi anachezesha yuko na Sime au beto....refa lazima awe mbabe naye

Ova
 
Unamkumbka kamsopi alikuwa ndy mtukutu wa upanga
Alikuwa anakaa zile flates zinazoangaliana na puma/Manji

Ova
Kamsopi mchumba tu.

Nimemgungia safari Forodhani, nikaoneshwa Kamsopi ndiyo huyu, akanikimbia.

Hapo nimeenda kutafuta ugomvi kumjua huyu Kamsopi ni nani, nimekuja na timu yangu kutoka Tambaza all the way to Forodhani!
 
Kamsopi mchumba tu.

Nimemgungia safari Forodhani, nikaoneshwa Kamsopi ndiyo huyu, akanikimbia.

Hapo nimeenda kutafuta ugomvi kumjua huyu Kamsopi ni nani, nimekuja na timu yangu kutoka Tambaza all the way to Forodhani!

Alikuwa anawapa sana watoto wa upanga wkt mgumu mpka kuna day mshikaji mmja anakaa upanga akaja mitaa ya Kino shamba kuomba tag,kwenda huko kumuona jamaa ahh Akasanda ila watoto wa kishua hko alikuwa anawatisha
Ila upanga ya sahv syo kama zamani
Upanga imepwaya iko kimya

Ova
 
Uliwahi kukutana na Mkama sharp mkuu?

Mkama sharp watoto wa keko walimfanyizia alilewa akaingia anga zao dah wakamla ndogo basi ukimkuta taifa akaanza kuwa mnyoonge na ile mikwara yote ikaisha..
 
Ah wa babe wakina Paul siza
Hyo kdg niyakanyage naye hapo langata enzi hzo maana wengine tulikuwa tnaonekana mabaharia
Siza aanatamani cheni nkaona ohooo
Sema aliishiaa kuwa mkabaji
Badaye akaingia kwenye ujambazi akayanyaga sehemu raia waakammaliza
Siza alikuwa bondia mzuri heavyweight
Alikuwa anakosa mapambano

Ova
Paul Siza alifariki kwenye tukio la ujambazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom