Mazungumzo na Dr. Slaa: Maswali na Majibu

Status
Not open for further replies.

Jenifa

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
605
305
Nina maswali magumu ya kumuuliza.

tafadhali baba rudi jf tujadili ile posho kubwa ya milioni 7.5

ninayo maswali mengine kuhusu mchumba wako wa kudumu kuwatumia waheshimiwa sms za mipasho.

maswali mengine yanahusu demokrasia finyu ndani ya chama chako. eti diwani wa arusha hawezi kuamua kitu mpaka lichama kule nyumbani kwa mtei liseme yeah!
 
WanaJF,

Naamini hamjambo. Msiwe na wasiwasi, nimejaa tele vijijini. Kazi kawaida ya Chadema mapambano yanaendelea Bungeni, na Slaa anaendelea kujenga Chama. Wiki hii nilikuwa Wilaya ya Kisarawe, na tumefanya mikutano mikubwa Chole, Maneromango na jana tumehitimisha Kisarawe mjini.

Kazi yetu kubwa ni kuwaelimisha watanzania, kuwaamsha wajue majukumu yao katika kulinda rasilimali zao, kuwasaidia kwanini tuko kwenye harakati za ukombozi wa mara ya pili, ambao kimsingi ni mgumu kuliko kazi ya kumwondoa mkoloni. Hii ndiyo kazi ya Dr Slaa na Sekretariat yake. Time is money hatuna muda wa kupuuza kujibu maswali yasiyo na tija kwa Mtanzania.

Kama ni posho na mishahara ya Dr Slaa hata Kisarawe wametuelewa. Wamejua jinsi TRA ilivyo wazembe wameikimbia Chadema baada ya kuja kwa mbwembwe, na leo washindwa kwa aibu kwa kuwa tumewaonyesha ukwepaji mkubwa ulioko serikalini ni aibu tupu. Kama rafiki yangu anahitaji kufahamu naomba afuatane nasi ziara ijayo vijijini.

Kama yuko mwenye maswali yenye tija kwa Taifa hili, pamoja na shughuli nyinmgi, pamoja na ukosefu wa umeme niko tayari kuyajibu. Lakini yenye tija kwa Mtanzania siyo ya kujifurahisha.



namtafuta daktari wa wakatoliki slaa. nina maswali magumu ya kumuuliza.

tafadhali baba rudi jf tujadili ile posho kubwa ya milioni 7.5

ninayo maswali mengine kuhusu mchumba wako wa kudumu kuwatumia waheshimiwa sms za mipasho.

maswali mengine yanahusu demokrasia finyu ndani ya chama chako. eti diwani wa arusha hawezi kuamua kitu mpaka lichama kule nyumbani kwa mtei liseme yeah!

yapo mengine mengi pamoja na kutaka kujua utaoa lini tutume michango maana uchumba huku mnazaa ni aibu kwa mkatoliki.

haya libaba usikimbie jf ukiwa rais usije ukakimbia wananchi. mpiga kura wako nimekumiss!
 
Dr Slaa una majukumu mazito kwa Taifa, sitegemei kama utajibu hawa waandishi wa magazeti ya udaku, hapa nategemea utueleze ni lini huyu Mamluki Shibuda mtamuondoa ndani ya chama, hafai hata kidogo.
Kumbuka ukiona mtu hata ccm hawamtaki basi juwa huo ni mzigo usiobebeka.
 
WanaJF,
Naamini hamjambo. Msiwe na wasiwasi, nimejaa tele vijijini. Kazi kawaida ya Chadema mapambano yanaendelea Bungeni, na Slaa anaendelea kujenga Chama. Wiki hii nilikuwa Wilaya ya Kisarawe, na tumefanya mikutano mikubwa Chole, Maneromango na jana tumehitimisha Kisarawe mjini. Kazi yetu kubwa ni kuwaelimisha watanzania, kuwaamsha wajue majukumu yao katika kulinda rasilimali zao, kuwasaidia kwanini tuko kwenye harakati za ukombozi wa mara ya pili, ambao kimsingi ni mgumu kuliko kazi ya kumwondoa mkoloni. Hii ndiyo kazi ya Dr Slaa na Sekretariat yake. Time is money hatuna muda wa kupuuza kujibu maswali yasiyo na tija kwa Mtanzania. Kama ni posho na mishahara ya Dr Slaa hata Kisarawe wametuelewa. Wamejua jinsi TRA ilivyo wazembe wameikimbia Chadema baada ya kuja kwa mbwembwe, na leo washindwa kwa aibu kwa kuwa tumewaonyesha ukwepaji mkubwa ulioko serikalini ni aibu tupu. Kama rafiki yangu anahitaji kufahamu naomba afuatane nasi ziara ijayo vijijini.
Kama yuko mwenye maswali yenye tija kwa Taifa hili, pamoja na shughuli nyinmgi, pamoja na ukosefu wa umeme niko tayari kuyajibu. Lakini yenye tija kwa Mtanzania siyo ya kujifurahisha.

daktari shikamoo.

asante kwa kuja kuchangia maswali yangu.

muuza mitumba analipa kodi iweje kiongozi mkuu wa chama upate posho milioni 7.5 bila kodi.

kulipa kodi ni wajibu wa sisi raia wote. uzembe wa TRA si sababu ya kushindwa kulipa kodi. ukishindwa kulipa kodi unakuwa na kosa. tuambie kwanini ni sawa kwa wewe kuwa na pato la milioni 7.5 na kushindwa kulipa kodi.
 
Dr Slaa kipenzi cha watanzania yupo vijijini anawaelimisha watanzania ili wajue dhuruma ya chama cha MGAMBA CCM dhidi ya watanzania.
 
daktari shikamoo.asante kwa kuja kuchangia maswali yangu.muuza mitumba analipa kodi iweje kiongozi mkuu wa chama upate posho milioni 7.5 bila kodi.kulipa kodi ni wajibu wa sisi raia wote. uzembe wa TRA si sababu ya kushindwa kulipa kodi. ukishindwa kulipa kodi unakuwa na kosa. tuambie kwanini ni sawa kwa wewe kuwa na pato la milioni 7.5 na kushindwa kulipa kodi.
Hivi wewe huwa unasomaga hili jamvi vizuri na thread by thread, topic by topic??maana unarudia vitu vile vile ambavyo vilisha jadiliwa, find something else cha kuongelea kama umeme na kwa nini unalala na giza na sio maswali ya kipuuzi na too personal na yasikuhusu na umbeya.
 
1) dK Slaaa. baadhi ya waislam wanalalamika eti Cdm ni chama kinachoongozwa kwa misingi ya dini ya kikiristo . jee nini maoni yako hasa ukiwa ndio mtendaji wa chama hicho?(Linafaida kwa taifa sana tu)
Maoni yangu waislam tuache kudanganywa na wajinga wachache kama BAKWATA ambao ni adui namba moja wa waislam tangia enzi za uhuru,BAKWATA ipo kwaajiri ya kulinda maslahi ya serikali ya CCM Badala ya waislam ambao tuna matatizo mengi.
 
1) dK Slaaa. baadhi ya waislam wanalalamika eti Cdm ni chama kinachoongozwa kwa misingi ya dini ya kikiristo . jee nini maoni yako hasa ukiwa ndio mtendaji wa chama hicho?(Linafaida kwa taifa sana tu)
Acheni maswali ya kijinga haya,hivi unavyoona CHADEMA inaongozwa kidini au wakitaka kufanya kitu lazima waingize dini??au CCM yenu pia inaongozwa kidini??acheni mambo ya udini na tuangalie why tunalala na giza bila sababu za msingi na sio kutoa upupu usiokuwa na mpango.......
 
WanaJF,
Kama yuko mwenye maswali yenye tija kwa Taifa hili, pamoja na shughuli nyinmgi, pamoja na ukosefu wa umeme niko tayari kuyajibu. Lakini yenye tija kwa Mtanzania siyo ya kujifurahisha.

Wasalaam Dr Slaa, na nakushukuru sana kuwepo kwako hapa jamvini.

Natambua kuwa CHADEMA hawajakamata dola na hivyo wana-limitation katika kutatua matatizo ya watanzania wengi maskini. Hata hivyo tumeshughudia mchango mkubwa wa CHADEMA katika kutatua tatizo la sukari (yaani kushusha bei) na kubwa zaidi, kuilazamisha serikali ya ccm kuanza mchakato wa katiba mpya.

Sasa hivi tuna tatizo sugu la umeme na kila kukicha inaonekana kama mambo yanazidi kuwa mabaya zaidi kuliko hata jana yake! Kama taifa tunaanza kupoteza imani na walio madarakani juu ya uwezo, na nia ya kutatua tatizo hili. Ningeomba kujua CHADEMA wana-mpango kuishinikiza serikali hii ya ccm @kutambua kuwa umeme kwa sasa hivi ni janga la kitaifa? (b)kuweka msimamizi mwenye uelewa mpana na uwezo/uthubutu katika wizara ya nishati na madini, na (c)kuunganisha nguvu ya watanzania katika kudai marekebisho ya haraka kwenye hili tatizo la umeme?

Nasema haya kwa sababu binafsi siamini kama Mh Ngeleja ana uwezo wa kutatua 'complexities' kwenye sekta ya nishati ya umeme. Na pia siamini hata kidogo kuwa tatizo ni bwala la Mtera 'kukataa' kujaa maji. Taarifa nilizonazo ni kuwa kuna wakulima wa mpunga wanashirikiana na bwawa la Mtera, je ushirikiano wao unaathiri (kwa kiasi chochote hata kama ni 1%) ujao wa maji wa bwawa la Mtera? na pia nijuavyo mimi, initial agreement ya IPTL ilikuwa kuleta mitambo ambayo ingeweza kutumia both oil na gas (baada ya technicak adjustment) lakini mitambo iliyoletwa nchini ni ya kutumia oil peke!

Then Symbion, sasa hivi wanazalisha chini ya capacity kwa sababu hawapati gas ya kutosha toka Songosongo, na kuna mchezo wa kuku na yai unaendelea maana Songosong wanawaambia Symbion kuwa wakitaka gas waongee na Tanesco na Tanesco wanawaambia Symbion wakitaka gas waende Songosongo!

Najua una sources nyingi na unaweza ku-double check haya matatizi niliyoandika lakini nadhani ingesaidia sana kama wananchi wote wangejua maana haiingii akilini kwa nini Mtera haijai!

Shukrani
 
Waislam wengi sasa hivi wanashabikia CCM kwa vile inaongozwa na muislam na sio chama chenye dini tofauti ambacho kinataka kuleta maslahi kwa taifa na kwa ajili ya vijana wetu wanaochipukia,this is nonsense kabisa na siwezi kufanya huo ujinga,mtu kabisa anakaa na kuuliza nonsense kwa ajili ya ku support chama ambacho hakina maslahi kwa taifa....tuangalie tulikotoka na tunakoenda,sasa hivi imefikia kwa day unapata umeme 4 hours je bado mnalizika na hili swala???na tukiwaachia hawa watu madaraka mnaona tunaenda wapi?na tutaishi vipi??si tutakuwa hatuna umeme kabisa??tufikirie zaidi na udini tuweke pembeni ili tuweke mabadiliko mapema kwenye hii nchi kabla haijawa too late.........
 
daktari shikamoo.asante kwa kuja kuchangia maswali yangu.muuza mitumba analipa kodi iweje kiongozi mkuu wa chama upate posho milioni 7.5 bila kodi.kulipa kodi ni wajibu wa sisi raia wote. uzembe wa TRA si sababu ya kushindwa kulipa kodi. ukishindwa kulipa kodi unakuwa na kosa. tuambie kwanini ni sawa kwa wewe kuwa na pato la milioni 7.5 na kushindwa kulipa kodi.
nadhan utakuwa na upungufu wa mawazo kama sio akili, posho ya sh milion 7 bila kulipa kodi ni uzembe wa serikali yako kutoweka na kutokuwa tayar kuweka mikakat ya kudhibit mambo kama haya. Kama serikali inataka kata kodi katika hela hii n lazma strategies za kukusanya mapato wazbadilishe. Hiyo n changamoto kwa serkal ya ******. If you cant beat me then join me. Hamwez pambana na cdm, bas unganen nasi.
 
Malaria Sugu,
Wiki hii nimekuwa maeneo mbalimbali ya Kisarawe. Wengi wao waislamu. Unawazungumzia Waislamu gani? Waislamu ninaokutana nao wanazungumzia tatizo la kuwa na mlo usio na uhakika wa siku, kutokuwa na maji safi na salama, hakuna zahanati na dawa, hakuna barabara, wanaishi nyumba za makuti. Unawazungumzia wepi na ulikutana nao wapi?
 
Acheni kuwa na akili mgando watu wa MAGAMBA ambao leo mnajifanya rafiki wa sisi waislam mnatumia udhaifu wa viongozi wetu wa dini ambao hawajasoma,zaidi ya elimu ya madrasa kwa kuwapa elfu ishirini ili waendelee kuwanyonya watanzania,tangia lini CCM imekuwa marafiki wa waislam?
Mkuu ndio ambacho nashangaa,ni upuuzi tu na hamna jipya,wanaona kabisa magamba wanafanya ujinga eti kwa vile ni waislam basi lazima kuwatetea....ni upuuzi uliokithiri kabisa na kukosa kazi ya kufanya,tuangalie chama chenye maslah kwa taifa na chenye kuweza kufanya mabadiliko.....toka lini CCM ikawa marafiki wa waislam??shtuka.
 
SHKAMOO DK SLAA. KATIBU MKUU NA ALIEKUWA MGOMBEA URAIS WA CDM.
Swali no 2.
I)Ubunge ulianza lini. jee kwanini wakati wa mkapa wakatu ulikuwa mbunge ulikuwa kimya sana tofauti na sasa. jee hakuna harufu ya udini hapa?
we dogo sikiliza usione watu wanakukaushia tu hapa sio kwamba hatukuoni ...nnyie mumeuliza dokta yuko wapi na amekuja hapa kujibu hoja zenu sasa inabidi muulize maswali ya msingi yenye tija kwenye jamii kuna vitu vingine sio nvya kuuliza wewe ushawahi hata kupiga stori na kikwete au Nape??? huwezi hata siku moja sasa umepata fursa ya kujibiwa hoja zako na viongozi wa wakubwa kama hawa moja kwa moja inabidi uweke jazba zako na maswali ya kipuuzi pembeni ..
 
FJM,
Thanks. Very serious concern. Ni dhahiri kwa hali tuliyonayo uchumi utadidimia zaidi.
i) Sina hakika kama nitamaliza sentensi kwa kuwa niko kwenye reserve charge na sina umeme nilipo, kiashiria cha dhahiri. Mgawo umekuwa mkali kuliko wakati wowote katika historia ya Tanzania.
ii) Serikali imeonyesha udhaifu, kushughulikia kuliko wakati wowote ule
iii) Serikali imekuwa ikitoa kauli tata, za udanganyifu na upotoshaji
iv) Serikali/Tanesco imeingia kwenye mkataba kinyume na amri ya mahakama na hivyo kuzua utata zaidi kuhusu nia na malengo ya mkataba na Symbion na hakuna uwazi katika mchakato wa kuingia mkataba huo.

Chadema, tutakuwa na Kamati Kuu hivi karibuni, itakayofuatiliwa na Operation Sangara Dodoma, Singida, na Morogoro. Tutatoa kauli ya Chama kufuatia Kikao cha Kamati Kuu, ikiwa ni pamoja hatua mahususi za kuishinikiza Serikali.

Wasalaam Dr Slaa, na nakushukuru sana kuwepo kwako hapa jamvini.

Natambua kuwa CHADEMA hawajakamata dola na hivyo wana-limitation katika kutatua matatizo ya watanzania wengi maskini. Hata hivyo tumeshughudia mchango mkubwa wa CHADEMA katika kutatua tatizo la sukari (yaani kushusha bei) na kubwa zaidi, kuilazamisha serikali ya ccm kuanza mchakato wa katiba mpya.

Sasa hivi tuna tatizo sugu la umeme na kila kukicha inaonekana kama mambo yanazidi kuwa mabaya zaidi kuliko hata jana yake! Kama taifa tunaanza kupoteza imani na walio madarakani juu ya uwezo, na nia ya kutatua tatizo hili. Ningeomba kujua CHADEMA wana-mpango kuishinikiza serikali hii ya ccm @kutambua kuwa umeme kwa sasa hivi ni janga la kitaifa? (b)kuweka msimamizi mwenye uelewa mpana na uwezo/uthubutu katika wizara ya nishati na madini, na (c)kuunganisha nguvu ya watanzania katika kudai marekebisho ya haraka kwenye hili tatizo la umeme?

Nasema haya kwa sababu binafsi siamini kama Mh Ngeleja ana uwezo wa kutatua 'complexities' kwenye sekta ya nishati ya umeme. Na pia siamini hata kidogo kuwa tatizo ni bwala la Mtera 'kukataa' kujaa maji. Taarifa nilizonazo ni kuwa kuna wakulima wa mpunga wanashirikiana na bwawa la Mtera, je ushirikiano wao unaathiri (kwa kiasi chochote hata kama ni 1%) ujao wa maji wa bwawa la Mtera? na pia nijuavyo mimi, initial agreement ya IPTL ilikuwa kuleta mitambo ambayo ingeweza kutumia both oil na gas (baada ya technicak adjustment) lakini mitambo iliyoletwa nchini ni ya kutumia oil peke!

Then Symbion, sasa hivi wanazalisha chini ya capacity kwa sababu hawapati gas ya kutosha toka Songosongo, na kuna mchezo wa kuku na yai unaendelea maana Songosong wanawaambia Symbion kuwa wakitaka gas waongee na Tanesco na Tanesco wanawaambia Symbion wakitaka gas waende Songosongo!

Najua una sources nyingi na unaweza ku-double check haya matatizi niliyoandika lakini nadhani ingesaidia sana kama wananchi wote wangejua maana haiingii akilini kwa nini Mtera haijai!

Shukrani
 
Dr Slaa ni mtu smart siyo kama KIKWETE ambaye kila siku yupo nje ya nchi wakati watanzania wanaishi katika maisha magumu,kuna janga la umeme ambalo linarudisha maisha ya mtanzania nyuma,kazi ya KIKWETE anayofanya sasa hivi ni kuitumia BAKWATA KUENEZA PROGANDA AMBAYO KIMSINGI IPO KWA AJIRI YA KUWAGANDAMIZA WAISLAM KWA KWA KUFICHA UOVU WA SERIKALI YA CCM,ILA UZURU JAMII IMESHAELEWA MBINU HIZO ZINAZOTUMIWA NA SERIKALI YA KIKWETE KWA KUWEKA MAKONGAMANO YA BAKWATA AMBAYO YAPO KWA AJIRI YA KUILINDA SERIKALI YAKE KWA MAOVU YAKE
 
Dr. Unapozungumzia nyumba bora sikuelewi!nakumbuka coverage moja channel ten ilimuonyesha mzee wako yaani Slaa akiwa katika makazi duni sana tena yenye kukatisha tamaa hivi usemi wa ''charity begins at home'' hauna maana?

Leo unaubiri makazi bora huku ukijua for the past fifteen years as an MP bila ufisadi usingeshindwa kumjengea baba yako nyumba ya kisasa.Hapa kuna tatizo la aidha ubinafsi au hujui unachokiubiri.Mzee hawezi kuishi na Mbuzi ndani hata kidogo.

Sitaki upambe,nahitaji Dr. anijibu hili kwani linamuhusu moja kwa moja katika jitihada zake za kutukomboa katika umasikini kama anavyodai.
 
SHKAMOO DK SLAA. KATIBU MKUU NA ALIEKUWA MGOMBEA URAIS WA CDM.
Swali no 2.
I)Ubunge ulianza lini. jee kwanini wakati wa mkapa wakatu ulikuwa mbunge ulikuwa kimya sana tofauti na sasa. jee hakuna harufu ya udini hapa?

@Malaria Sugu, ili kuwa na a very cilivilised debate ni vizuri tukangea issue based on facts kuliko hisia. Dr. Slaa amekubalika kwa wananchi wengi Tanzania kupitia 'bunge'. Ni kutokana na umahiri wake wa kuibua uzembe, ubadhirifu na kutozingatia sheria katika governance system yetu ndiko kumemfanya akajulikana kwa watanzania. Na amekaa bungeni miaka 15, kama utakuwa umesahau mapambano yake ndani ya bunge kaombe 'hansard' za bunge ili uweze kuandaa essay yenye mashiko.

Hii tabia ya character assissination ili mtu aogope/ashindwe kuibua mapungufu kwenye utawala wa umma is extremely low and un-guided way of dealing with the malfunctions on your part.
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom