Maziwa ya mama kukata ghafla

Maziwa ya mama kukata ghafla

braity

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2020
Posts
424
Reaction score
600
Habari wanajamvi.

Kuna mama ana mtoto wa miezi 4 na amepatwa na hali ya ajabu maziwa ya kumnyonyesha mtoto yamekata ghafla.

Hii hali inasababishwa na kitu gani maziwa ya mama yakate ghafla?
 
Labda kuna jambo anapitia linamsababishia stress,hii yaweza kuwa sababu mojawapo.
 
Labda kuna jambo anapitia linamsababishia stress,hii yaweza kuwa sababu mojawapo.
Stress zinaweza kusababisha maziwa yasitoke? Mbna ni kama hakuna uhusiano kabisa?
 
Stress zinaweza kusababisha maziwa yasitoke? Mbna ni kama hakuna uhusiano kabisa?
Stress homoni kama Cortisol husababisha mrejesho hasi/negative feedback kwa homoni zinazohusika na kuzalisha maziwa kama Prolactin na hivyo kuathiri kwa kikubwa kiasi cha maziwa yanayozalishwa.
 
Pole mkuu fanya hivi
Kesho asbhi na mapema mpe huyo.mama wa mtoto mchai chai bila sukari
 
Msongo wa mawazo na uchovu mkubwa, Kupungua au kuacha kunyonyesha ghafla, Matumizi ya baadhi ya dawa kama za uzazi wa mpango, Mimba mpya, Magonjwa au homoni kutofanya kazi vizuri, Lishe duni na upungufu wa maji mwilini, Kuvuta sigara n.k

Ikiwa sababu ni lishe ulaji wa mbegu za maboga huweza kusaidia 🙏
 
Back
Top Bottom