Mawaziri hawa wana tatizo gani?

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
WAKATI tetesi za kupanguliwa Baraza la Mawaziri zikizidi kupamba moto, hali ya afya ya baadhi ya mawaziri imeelezwa kuwa tete hivyo kulazimika kupelekwa India kwa matibabu.Miongoni mwa Mawaziri hao ni wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami ambaye jana aliibuka na kuwataka watu aliowaita wanye uchu wa kuchukua nafasi yake, waache mara moja kutumia afya yake kupiga propaganda chafu za kisiasa.

Hadi sasa, mawaziri ambao taarifa za kuugua kwao zinafahamika ni pamoja na Profesa Mark Mwandosya mwenye dhamana ya Maji, Naibu Waziri Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Dk Chami. Wengine ambao taarifa zinaonyesha kuwa walikuwa nje ya nchi kwa matibabu ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe na Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani.

Ingawa haijafahamika maradhi yanayowasumbua hadi sasa, wadadisi wa mambo ya kisiasa wamekuwa wakichukulia hali ya afya ya baadhi yao kama moja ya sababu inayoweza kuwafanya wawekwe kando pale Rais Jakaya Kikwete atakapoamua kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ili kuwapa fursa ya kupumzika na kuendelea na matibabu
MWANANCHI
 
tmebaki na mawaziri wawili tu tibaijuka na magufuli,pamoja na naibu wetu mwanri,hao uliowataja wakapumzike tu jaman,na tena mwanri anafaa kuwa waziri mkuu
 
tmebaki na mawaziri wawili tu tibaijuka na magufuli,pamoja na naibu wetu mwanri,hao uliowataja wakapumzike tu jaman,na tena mwanri anafaa kuwa waziri mkuu

kwa sababu ya kelele zake za juzi iringa? Au kuna cha ajabu kingine alikifanya wapi?
 
mwanri anatoa macho sana hana lolote kada mahiri wa chama hawezi kuongoza ktk zama hizi za ustaarabu wa itikadi tofauti.
 
Hawa mafisi wanaosubiri miili ya mawaziri iingie kweny jeneza...watasubiri sana-by Chami
 
tmebaki na mawaziri wawili tu tibaijuka na magufuli,pamoja na naibu wetu mwanri,hao uliowataja wakapumzike tu jaman,na tena mwanri anafaa kuwa waziri mkuu

Wewe umenena. Pia na Wakurugenzi wa Taasisi kama TBS na TAKUKURU nao wangepisha nafasi kwani utendaji wao una walakini.
 
Kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi, CELINA KOMBANI aendelee kuugua salama mpaka baraza jipya lipangwe.
 
kwa sababu ya kelele zake za juzi iringa? Au kuna cha ajabu kingine alikifanya wapi?[ AGREY mwanri Mbona ndio injini tangu kitambo.co kwa sababu ya kelele za iringa]
 
Wewe umenena. Pia na Wakurugenzi wa Taasisi kama TBS na TAKUKURU nao wangepisha nafasi kwani utendaji wao una walakini.

Tawire baba. Ingekuwa JK ni msikivu, angesham-sack Hosea miaka mingi sana, lkn kama unavyojua Hosea anajua inside out ya Richmond, ndo sababu yupo kazini hadi leo.
 
tmebaki na mawaziri wawili tu tibaijuka na magufuli,pamoja na naibu wetu mwanri,hao uliowataja wakapumzike tu jaman,na tena mwanri anafaa kuwa waziri mkuu

Tibaijuka tu - sio huyo mwingine uliyemtaja
 
Hivi na yule zeruzeru wa TRA Bado tu haijafika 60? Naona yule wa POLISI anafikisha 60 Sasa!Atastaafu au bado? Naona umri wa kustaafu unaongezwa kinyemela kila siku.
 
Pinda naye apumzike. Hivi sophia Simba naye bado ni waziri?

rafiki unajua gharama za baada ya kua waziri mkuu? kifupi ni noma
ni bora aendelee pinda wetu kwanza ana busara sana la sivyo achaguliwe kiongozi ambaye tayari alisha kua rais au w.mkuu kuepuka hizo gharama.
tuepende Tanzania yetu
 
Back
Top Bottom