Mawakili wa Serikali walaani Azimio la TLS

Mawakili wa Serikali walaani Azimio la TLS

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
745
Reaction score
1,470
Chama cha Mawakili wa Serikali (PBA) kimesema hatua zilizochukuliwa na viongozi wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) cha kuwataka mawakili wa kujitegemea kutoshiriki kwenye shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi ni kinyume cha sheria za nchi na miiko ya kazi za wanasheria.

Akizungumza na waandishi wa habari Jiini Dar eskali Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho, Wakili Addo November, amesema TLS, kama taasisi ya kisheria, ina wajibu wa kikatiba wa kuhakikisha kwamba maamuzi yake hayapingani na sheria iliyoianzisha (TLS Act) na sheria nyingine husika kama Legal Aid Act.

Vilevile, amesema taasisi zote za kitaaluma zinapaswa kushirikiana kwa weledi katika kulinda misingi ya haki, usawa, na utawala wa sheria, badala ya kuchukua hatua zinazoweza kuzorotesha huduma za kisheria kwa wananchi wa kawaida nchini.

Nao baadhi ya Mawakili wa Kujitegemea, akiwemo aliyewahi kuwa Rais wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Francis Stolla, wamesema TLS inapaswa kutetea haki za wanachama wake wanaoingia kwenye migogoro na vyombo vingine vya kisheria, pasi na kuvunja sheria na katiba ya nchi.

Chanzo @TBC @FLOW MEDIA tz

PIA SOMA:


View: https://youtu.be/vATHWZ-f14E?si=xOcZponr2om48VIH
 
Kuvunja katiba kaanza bi chura na mwendazake kwa kutaka mihimili yote iwe chini ya Executive sasa impact yake ndo hii executive imekuwa na nguvu mno kiasi kwamba hii mihimili mingine ni kama bendera fata upepo....

Sasa TLS isiposimamia kuilinda hii taalum tutaisha
 
Chama cha Mawakili wa Serikali (PBA) kimesema hatua zilizochukuliwa na viongozi wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) cha kuwataka mawakili wa kujitegemea kutoshiriki kwenye shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi ni kinyume cha sheria za nchi na miiko ya kazi za wanasheria.

Akizungumza na waandishi wa habari Jiini Dar eskali Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho, Wakili Addo November, amesema TLS, kama taasisi ya kisheria, ina wajibu wa kikatiba wa kuhakikisha kwamba maamuzi yake hayapingani na sheria iliyoianzisha (TLS Act) na sheria nyingine husika kama Legal Aid Act.

Vilevile, amesema taasisi zote za kitaaluma zinapaswa kushirikiana kwa weledi katika kulinda misingi ya haki, usawa, na utawala wa sheria, badala ya kuchukua hatua zinazoweza kuzorotesha huduma za kisheria kwa wananchi wa kawaida nchini.

Nao baadhi ya Mawakili wa Kujitegemea, akiwemo aliyewahi kuwa Rais wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Francis Stolla, wamesema TLS inapaswa kutetea haki za wanachama wake wanaoingia kwenye migogoro na vyombo vingine vya kisheria, pasi na kuvunja sheria na katiba ya nchi.

Chanzo @TBC @FLOW MEDIA tz

PIA SOMA: Tamko La Rais Wa TLS Juu Ya Kitendo Cha Polisi Kuzunguka Ofisi Za TLS


View: https://youtu.be/vATHWZ-f14E?si=xOcZponr2om48VIH

Ni pure breeds ya CCM, better named "Mawakili wa Chama Cha Mapinduzi"
 
Ila Wakili Mwanachama wa TLS aliposhambuliwa na Mapolisi akiwa anatekeleza majukumu yake Mahakamani ambapo ni eneo lake la kazi, hawakuliona hilo. Kwanini hawakutoa tamko la kulaani tukio lile?? Watched unafiki.
Ni wanafiki kweli
 
Back
Top Bottom