Maulizo juu ya ajira mpya 2020

Maulizo juu ya ajira mpya 2020

Nakushukuru sana Mungu wa Mbinguni muumba mbingu na nchi. Hakika pamoja na kwamba ujana ulichangia lakini nakushukuru sa a kwa kuniepusha na hili janga la ualimu. Sijui leo hii ningekuwa mgeni wa nani
Ilikuwaje kaka.
 
Hakuna ajira zozote zitakazo toka kama unabisha endelea kusubiri uone. Wameshindwa kuajiri polisi wasaidie kusimamia uchaguzi ndio waje kuajiri walimu ambao mpaka sasa hivi wapo likizo ya corona?
 
Mazee ungekuwa kada, ungekuwa unashika chaki muda huu
 
Sidhani kama TAMISEMI wanahusika moja kwa moja katika hili. TAMISEMI kazi yao ni kuwasilisha idadi ya nafasi za kazi kwa sekritarieti ya ajira. Hawa ndio wanasimamia na kuratibu ajira za utumishi wa umma kwa sasa. Kuanzia application, interview hadi allocation.

Not sure kama waalimu wanakuaga na interview nadhani wao ni application na allocation moja kwa moja kama Madaktari.

Ushahuri wangu kama hakuna interview kwenye ualimu kama kada zingine basi connection unayotakiwa kuipata ni kule sekretarieti ya ajira wanapofanya allocation za ajira.
 
Jamani na Mimi naombeni connection nipate dili msimu huu . Mana nipo kitaa kitambo . Nilipata dili sehemu flani lakini kwa sababu sikuwa na sapoti nikanyimwa mkataba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachelea kusema unataka kupata ajira kupitia mlango wanyuma!! Hii inaweza kuchukuliwa kama ni rushwa.
 
Kwa hivyo unakiri kua elimu uliyoipata haijakusaidia kupambana na mazingira yako mpaka ubebwe tena na ajira?
Wabongo kwa kujifanya wajuaji mwana anapambana bado mnajifanya wajuaji, ungekua Co-founder wa JF tungekuelewa your platform your rules, we have all been there acha watu wafanye kilichobora kwao, kama anapambana na anahisi bado ajira kwake muhimu let him be.
 
Sidhani kama TAMISEMI wanahusika moja kwa moja katika hili. TAMISEMI kazi yao ni kuwasilisha idadi ya nafasi za kazi kwa sekritarieti ya ajira. Hawa ndio wanasimamia na kuratibu ajira za utumishi wa umma kwa sasa. Kuanzia application, interview hadi allocation.

Not sure kama waalimu wanakuaga na interview nadhani wao ni application na allocation moja kwa moja kama madaktari.

Ushahuri wangu kama hakuna interview kwenye ualimu kama kada zingine basi connection unayotakiwa kuipata ni kule sekretarieti ya ajira wanapofanya allocation za ajira.
Hizi ajira za ualimu huwa zinaratibiwa na Tamisemi sekretarieti ya ajira haihusiki
 
Siku hizi mwenye kibali cha ajira za ualimu ni raisi na tamisemi wala siyo afisa elimu.
Mkuu wa shule ana nguvu ya ushawishi Tamisemi na wengi hufanya hivyo,nimeshuhudia walimu kama 4 wa sayansi wameajiriwa katika shule walizojitolea kutokana na kufanyiwa mchongo na mkuu wa shule
 
Ndugu tafuta shule afu jitolee hususani shule za bweni maana utakuwa na hakika ya accommodation na chakula,siku hizi wanaajiriwa wanaojitolea hivyo mkuu wa shule atatuma maombi ya kukuombea ajira tamisemi, hii ndio njia rahisi zaidi.
 
Mimi binafsi yangu nimeshaelewa kwanini hukupata ajira miaka mitatu yote (na wala hutapata) kwasababu hakuna shule yoyote ya Serikali wala Binafsi panapofundishwa masomo hayo... just joking my fellow teacher!

Turudi Kuhusu swala lako sikushauri sana ufanye hicho ulichokiandika (japokuwa inauma sana mpaka kufikia kuwaza hivyo ni kwamba umesota sana huku ukisikilizia ajira matokeo yake kila post unapitwa).

Ushauri wangu zidisha juhudi, subira na uvumilivu tu naamini one day yes. Cha msingi kuwa current na updates zote kuhusu maswala ya ajira.

Ngoja kwa kutumia mfano, nikwambie kwanini sikushauri uhangaike na watu fulani fulani eti kisa wana connections kwenye TAMISEMI...
Nakupa stori yangu mimi binafsi

SEHEMU A
Nimehitimu form IV 2012 nikascore four ya 29 ikarekebishwa mpaka 27.
2013 Tukaanza kutuma maombi serikalini kuomba kujiunga kwenye vyuo vya kati binafsi nilituma vyuo vi5 tofauti (yaani sekta 5 tofauti).

Majibu yanatoka awamu ya kwanza siyo mifugo kilimo ualimu wala nini hakuna nilipochaguliwa akaja mzee wangu mmoja akasema KUNA MWANAMAMA MMOJA ANAFANYIA KAZI WIZARA YA TAMISEMI aongee naye nifanyiwe mpango niungwe mojakwamoja chuo chochote cha ualimu

Basi kuongea nae akasema (kuwaambia wazee wangu) kwajili ni wao hatawashika hela yoyote ila watalazimika kutoa laki mbili na nusu tu kwajili ya kugharamia mambo madogomadogo tu ya kufanikisha swala hilo. Tena akaomba atanguliziwe laki halafu ishu ikitiki laki na nusu imaliziwe

Basi bwana sikumbuki vizuri post za awamu ya pili na huo mpango kipi kilitangulia lakini post za pili hizo mwanaume kama kawa kama dawa sijachaguliwa! Wakiwasiliana nae anasema wasijali mimi nitaenda mojakwamoja chuoni majina kwenye ubao yasinitishe

Mara paap! Kuna ambao hawakuripoti walipopangwa kwahiyo wahuni wanaenda kufanyiwa magumashi vyuoni palepale wanajiunga hata kama haukuchaguliwa (sijui ni kivipi vipi lakini kuna masela wangu walioendaga Mpwapwa na Bustani).

Basi bwana kutonywa nikatupia rupia huko nako nikadunda lakini yule mhusika chuoni nashukuru aliweka wazi kabla kwamba kuna kutiki na kubuma kwahiyo ikibuma siyo aonekane tapeli na kuwekeana ubaya maana hataweza kurudisha hela.

Baada ya hapo ikaja ishu ya JKT nikaomba hapo ndo nikakosa mchana kweupeee na sababu iliambiwa nimezidi miezi mi3 (wengine walitolewa eti wamezidi siku 2, 3 nk). Sasa hiyo interview yenyewe inavyoendeshwa ndo utasema tu asante Mungu nimeingia kwa DC na kupata walau nafasi ya kuongea na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Basi Bwana ikawa nimedunda vitu vyote pamoja na kwamba kwenye vyuo vingine niliandika barua mara mbilimbili na baadhi yao nilituma maombi kwa njia ya EMS. Ikawa yule mama wazee wanaogopa hata kumpigia simu maana alisema ishu ikitiki atawapigia mwenyewe kuwataarifu ( alisisitiza kuwa ni jambo dogo tu- tena hata alisema kabisa kwamba tusitafute chuo chochote kwani jambo lile ana uhakika nalo kuwa angefanikisha).

Sasa watu wakaripoti wee mpaka tarehe ya mwisho kuripoti kukaribia mzee ikabidi ampigie, yule mama akasema wala siyo ishu tarehe hiyo ila hebu niacheni saivi niko bize nitawacheki kesho. Kesho yake hakupiga mzee akipiga hapokei. Basi siku tatu mbele kila mzee akipiga simu haipokewi basi siku za kuripoti zikaisha yule mama hapokei simu si ndo mzee akaandika sms moja matata sana na ndo tukaachana naye.

Yote haya yule mzee wangu aliyetuunganishaga na yule mwanamama hajayajua mpaka leo maana yeye yupo zake mbali na nyumbani alipowaunganisha wazee kule yeye akajua hamsini zake. Mzee wangu alininyima namba za yule mwanamke na hata za yule mzee eti alihofia nisije nikaharibu urafiki wao wale wawili.

Hela nyingine hazikuniuma lakini hiyo ilinitia hasira maana mzee aliishiwa siku hiyo akasema nimpe elfu 50 aongeze hamsini yeye nikampa hela ambayo nilivyoipata tu MwenyeziMungu mwenyewe shahidi.

Ndipo mzee akapata kwamba kuna chuo cha private kipya kina bei ya chini (ada) ndipo nikafanyiwa maandalizi ya fasta kihasirahasira nikaenda kusoma (zile hekaheka zote ilikuwa ni kutafuta serikalini kwenye kuendana na hali zetu).

Ndo hivyo ndugu yangu nikasoma private japo napo kuna mambo yalinikumba magumu sana lakini ngoja nifupishe tu nikahitimu pale na kuanza kungojea ajira.

SEHEMU B
Sasa mazoea yakatuumiza tulio wengi kwamba unahitimu May ajira ni kuanzia October hadi March. Bwana we! Ngoma ilianzia kubadilika pale waliotutangulia walipopelekwa JKT ndipo wakapangiwa vituo vya kazi tukashangaa wamecheleweshwa.

Ilipofika zamu yetu sasa ndo mambo yakawa ya ajabu zaidi kwani ilikuwa kila kukicha ngonjera za kwenda JKT mara zikakatika ikabaki ishu ya post za ajira subiri subiri na wewe hakuna ajira wala nini ni ngonjera tu. Nakumbuka radio uhuru siku hiyo wakatoa taarifa eti serikali kumwaga ajira za walimu elfu 40 sisahau ile. Ikatokea ajira ngapi sijui zile nikakoswa niliwaza sana maana kigezo chao nilikuwa nacho

Ikafikia nikawa kama nakata tamaa muda mwingine halafu ghafla tena narudi kuwa na subira. Nakumbuka mpaka watu wakawa wanatukanana mitandaoni kisa kufanyiana masihara kuhusu ajira wengine wakatapeliwa sana na wengine kudanganyana sana kwajili ajira zilikuwa hazitolewi na serikali ipo kimya kama hakuna jambo la kudili nalo

Kipindi hicho nikivuta picha aisee nilikuja kuwa kama nunda fulani hivi halafu nikawa naichukia serikali (viongozi wakubwa wa serikalini- hasa wa vyeo vya kuteuliwa na raisi). Siyo siri kumbe kukosa ajira kunauma na kunabadilisha moyo wa mtu

Mungu si Magufuli bwana siku ya siku nashangaa napigiwa simu ajira kadhaa zimetolewa na mimi nimechaguliwa hata sikuamini nikawa naingia mtandaoni mara kwa mAra kuhakiki jina langu.

Sasahivi ni mwalimu kwenye shule X nachapa kazi. Nimeanza kuyasahau kidogokidogo yaliyopita yote na ndo hata nikaamua kubadili ID humu nianze ukurasa mpya. Nakusihi kama ni connections basi ziwe za kule kujuana na ujamaa tu zisiwe za kupigwa hela utajikuta unapagawa tu bure kwani hela utakayopoteza ni sawa na mshahara au mtaji wako

Dah! Nimekumbuka mbali sana ngoja nikomee hapa
 
Back
Top Bottom