Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 242
Maudhui ya shairi la wanafunzi yamchefua DC
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Henry Clemens, juzi aligeuka mbogo baada ya kukasirishwa na shairi lililoimbwa na wahitimu watarajiwa wa Kidato cha Nne katika Shule ya sekondari ya Kata ya Kiparanganda.
Maudhui ya shairi yalikuwa yanaeleza manunguniko yao dhidi ya serikali kutokana na matatizo kibao yanayozikabili shule za kata ikiwemo ukosefu wa walimu huku wakidai kwamba walengwa wa shule hizo ni watoto wa walalahoi.
Wahitimu hao katika mashairi yao walidai kuwa matatizo mengi yanayozikabili shule za kata yanachangia wengi wao kufeli na kujikuta wakiishia mitaani wakikosa kazi za kufanya huku watoto wa vigogo wakiendelea kuneemeka na elimu bora wanayoipata kutokana na wazazi wao kuwa na uwezo.
Baadhi ya maneno yaliyopo kwnye mashairi hayo yanasema :shule za kata wamejengewa masikini, watoto wa wakubwa hawaonekani, maisha mitaani magumu, wanafunzi wanafeli, nyumba za kupanga, wengi wanakatisha masomo yao, wazazi wengi masikini, hakuna walimu tabu nyingi wanapata mitaani, wazazi hawana uwezo wanategemea mashamba. Serikali itupe suluhisho la matatizo haya.
Baada ya wanafunzi hao kumaliza mashairi yao, Mkuu wa huyo wa Wilaya aliwageukia wazazi wao na kuwaonya kutohusisha ujenzi wa shule hizo na masuala ya kisiasa.
Pia aliwataka waache tabia ya kukumbatia umasikini wakati wana uwezo wa kuwasomesha watoto wao.
kuna matatizo ya hapa na pale lakini motto akianza kutembea anatambaa ndiyo hatua ya kwanza. Jitihada za serikali kujenga shule za sekondari Mkuranga ni tofauti na maeneo mengine hapa nchini kulikuwa na shule za sekondari nne lakini hadi sasa zipo 22, ni sawa na ongezeko la asilimia 450, maeneo mengine hayana asilimia hiyo licha ya halmashauyri nyingine kuwa na umri wa miaka 100, tusiulize serikali iko wapi, tuseme serikali ijitahidi kuongeza ubiora wa shule, alisema Mkuu wa Wilaya..
Aliongeza: Serikali ipo na kama isingekuwepo msingepata nguvu za kusema maneno hayo.
Alisema hakubaliani na waliosoma mashairi hayo na kuwataka wanafunzi hao wasome na kwenda kuwasaidia wazazi wao..
Mimi mbona nilisoma shule za kimasikini na hadi sasa nina digrii zangu mbili na nataka nikaongeze nyingine, na wale wanaotaka kuwa na watoto wa wakubwa nitawapeleka Masaki mkakae nao, msikae kuukumbatia umasikini, shule za kata zimejengwa kwa ajili ya wananchi wote na siyo kuwalenga watoito wa kimasikini, umasikini ni wa kujitakia hata ukiwa tajiri huwezi kukamilika kwa kila kitu. Shida yenu ni kupata elimu au kusoma na watoto wa wakubwa? alisema na kuhoji na kuwataka waachane na mambo ya siasa kwa kuwa hayana mwisho.
Chanzo: Nipashe
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Henry Clemens, juzi aligeuka mbogo baada ya kukasirishwa na shairi lililoimbwa na wahitimu watarajiwa wa Kidato cha Nne katika Shule ya sekondari ya Kata ya Kiparanganda.
Maudhui ya shairi yalikuwa yanaeleza manunguniko yao dhidi ya serikali kutokana na matatizo kibao yanayozikabili shule za kata ikiwemo ukosefu wa walimu huku wakidai kwamba walengwa wa shule hizo ni watoto wa walalahoi.
Wahitimu hao katika mashairi yao walidai kuwa matatizo mengi yanayozikabili shule za kata yanachangia wengi wao kufeli na kujikuta wakiishia mitaani wakikosa kazi za kufanya huku watoto wa vigogo wakiendelea kuneemeka na elimu bora wanayoipata kutokana na wazazi wao kuwa na uwezo.
Baadhi ya maneno yaliyopo kwnye mashairi hayo yanasema :shule za kata wamejengewa masikini, watoto wa wakubwa hawaonekani, maisha mitaani magumu, wanafunzi wanafeli, nyumba za kupanga, wengi wanakatisha masomo yao, wazazi wengi masikini, hakuna walimu tabu nyingi wanapata mitaani, wazazi hawana uwezo wanategemea mashamba. Serikali itupe suluhisho la matatizo haya.
Baada ya wanafunzi hao kumaliza mashairi yao, Mkuu wa huyo wa Wilaya aliwageukia wazazi wao na kuwaonya kutohusisha ujenzi wa shule hizo na masuala ya kisiasa.
Pia aliwataka waache tabia ya kukumbatia umasikini wakati wana uwezo wa kuwasomesha watoto wao.
kuna matatizo ya hapa na pale lakini motto akianza kutembea anatambaa ndiyo hatua ya kwanza. Jitihada za serikali kujenga shule za sekondari Mkuranga ni tofauti na maeneo mengine hapa nchini kulikuwa na shule za sekondari nne lakini hadi sasa zipo 22, ni sawa na ongezeko la asilimia 450, maeneo mengine hayana asilimia hiyo licha ya halmashauyri nyingine kuwa na umri wa miaka 100, tusiulize serikali iko wapi, tuseme serikali ijitahidi kuongeza ubiora wa shule, alisema Mkuu wa Wilaya..
Aliongeza: Serikali ipo na kama isingekuwepo msingepata nguvu za kusema maneno hayo.
Alisema hakubaliani na waliosoma mashairi hayo na kuwataka wanafunzi hao wasome na kwenda kuwasaidia wazazi wao..
Mimi mbona nilisoma shule za kimasikini na hadi sasa nina digrii zangu mbili na nataka nikaongeze nyingine, na wale wanaotaka kuwa na watoto wa wakubwa nitawapeleka Masaki mkakae nao, msikae kuukumbatia umasikini, shule za kata zimejengwa kwa ajili ya wananchi wote na siyo kuwalenga watoito wa kimasikini, umasikini ni wa kujitakia hata ukiwa tajiri huwezi kukamilika kwa kila kitu. Shida yenu ni kupata elimu au kusoma na watoto wa wakubwa? alisema na kuhoji na kuwataka waachane na mambo ya siasa kwa kuwa hayana mwisho.
Chanzo: Nipashe