Mauaji ya visasi

Nilichojifunza kwenye maisha haya ni kwamba ukizisoma amri kumi za Mungu na ukazielewa utakuwa salama duniani na huko utakapoenda baada ya kufa. Barikiwa sana brother mshana.
 
Inakuwaje sasa kiumbe kilichoumbwa kwa moto (Lucifer/Malaika) kuwa na na hisia za kibaiolojia hadi atamani kiumbe kilichoumbwa kwa udongo (Binadamu)?

Inamaana Malaika kabla ya kuasi nao walikuwa wana Humans biological hormones kuratibu gametiume/gametiuke hadi wawe na ashki/nyege za kugegedana na Binadamu?

Mbona kama kamba hii
 
Chifu jazia nyama tafadhali maana si kila kinachoendelea duniani sote tuwe tunakijua sababu wakati mwingine tunakuwa tuko bize ktk ujenzi wa Taifa
 
umenikumbusha kisa kilichotokea kanda ya ziwa jamaa alieua familia nzima mpk kichanga....inasikitisha na kuogopesha
Weka hapa hicho kisa Unforgettable, kama Kingsmann kashindwa kukutunza mkulingwa nipo nitakulea kimatunzo tu ila ki-baiolojia ni big NO(utani)
 
Mkuu reference ni bible kwa hiyo ukisema ni chai meaning Bible ndio chai sio Mimi nayeleta story kutokea humo.

Bible ipo clear kwamba "Wana wa Mungu" walizaa na hao binadamu na reference ni Mwanzo 6 na hiyo Yuda 1. Ukitaka kuona hili hata uzao wao haukufutika kwa gharika rejea Mwanzo 13 utaona wapo hao watoto wa cross breeding hii.

Kuhusu malaika kuwa na hisia, ndio hoja ya shape shifting inapoingia hao walioasi ni wale walikua "watchers" yaani walipewa jukumu la kuwafunza wanadamu mambo mengi kama kuwinda, kusoma nyota, medicine, engineering n.k sasa mfano wakati wanamtembelea Abraham malaika waliweza hadi kula chakula, walisikia njaa, na hata yule aliyepigana na Yakobo "alichoka" baada ya mpambano wa usiku kucha.

Nachojaribu kusema in reference kwa biblia Ina maana malaika wote waliofanya interaction na binadamu walivaa miili ya kibinadamu hivyo kuchukua character zetu kama vile njaa, kuchoka, na tamaa kama iliyowakuta hao malaika wanaotajwa kwenye Injili ya Yuda.
 
hajui kuwa hata malaika waliwahi shuka duniani na kutembea na wanadamu na kuzaa nao watoto!
 
Kisa cha nane
Huyu hakuuliwa bali alitiwa kilema cha chongo kwenye biashara ya mirungi

Ni kisa cha miaka ya 80 mwishoni huko Tanga milimani
Jamaa waliandaa mzigo wa kama roba kumi hivi za mirungi, wateja wakiwa wako Mombasa Kenya.. Mmojawao aliyekuwa na kazi ya kupelekea wateja mzigo akaingiwa na tamaa baada ya kuuza mzigo wote Tanga mjini na kutimkia Dar mazima

Baada ya mwaka mmoja kupita akakutana na wale jamaa zake aliowapiga mzigo mitaa ya manzese(kumbe walikuwa wanamfuatilia)

Walimkuta jamaa bar moja ya uswazi Manzese midizini, jamaa akashikwa na taharuki na kujaribu kujitetea kwamba alikamatwa na mzigo ukataifishwa naye akafungwa miezi 9 jela

Jamaa zake wakajifanya kusikitika sana na kumpa pole nyingi na bia zikaendelea kunyweka huku wakichoma mishkaki kwenye jiko la mkaa karibu yao
Miaka ile mishkaki ilichomekewa kwenye spoke za baiskeli zilizochongwa vema
Basi walimzuga jamaa mpaka woga ukamuisha na ku relux kabisa. Kumbe kati ya zile spoke kuna moja iliwekwa kwenye mkaa na ikakolea moto mpaka ikawa nyekundu kabisa

Kwa ghafla sana wale jamaa watatu walisimama na kumkamata jamaa
Mmoja akambana kichwa
Mwingine akambana miguu na mikono
Ma wat mwisho akaichukua ile spoke iliyokolea moto akamfunua jicho na kumchoma nayo
Baada ya pale walimwachia huku akipiga kelele nyingi za maumivu na jamaa wakatimka wakapotea!
 
Kisa cha tisa
Mauaji ya Ilala! Chanzo dhuluma
Jamaa waliuziana gari, mnunuzi akalipa pesa ya kianzio lakini akashindwa kumaliza
Mwenye gari kila akikumbushia pesa yake jamaa anampiga kalenda
Siku ya siku mdaiwa akamuita mdai wake afike nyumbani kwake Ilala ampatie pesa yake

Jamaa akafika home kwa anayemdai, akakaribishwa vema lakini kufika ndani kumbe mwenzake alikuwa na lake moyoni! Akamuua na kumzika karibu na mashimo ya vyoo kisha akasakafia vema kabisa
Mauaji yalikuja kujulikana miaka takriban mitatu baadae
 
Yule jamaa wa kipemba. Mshkaji alimwonea sana, gari analo, fedha hajalipa na bado akamuua muuzaji
 
Yule jamaa wa kipemba. Mshkaji alimwonea sana, gari analo, fedha hajalipa na bado akamuua muuzaji
Ndio huyo huyo aisee sijui kesi yake imefikia wapi
 
Sasa mbona mkuu umesema Abel hakuwa mtoto wa ndoa? Na huko unasema Kaini alikuwa mtoto wa ibilisi?
 
Ndio huyo huyo aisee sijui kesi yake imefikia wapi
Nimeona mitandaoni kuwa ndio inasikilizwa sasa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo tarehe 15.09.2022 shahidi wa kwanza upande wa Mashtaka alianza kutoa ushahidi wake na kesi ikaahirishwa mpaka kesho yake tarehe 16.09.2022, nafikiri itakuwa inaendelea kusikilizwa au kusubiriwa uamuzi kama mtuhumiwa ana kesi ya kujibu.
 
Asante mkuu jamaa bado yuko mahabusu tangu 2014
 
SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya mauaji inayomkabili Hemed Ali, ameieleza mahakama jinsi mshtakiwa huyo alivyoishi ndani ya nyumba yake na baadaye kupokea taarifa kuwa kuna mtu alifukiwa katika nyumba hiyo na mshtakiwa.

Shahidi huyo, Hamjat Nassoro ambaye ni mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiishi mshtakiwa maeneo ya Ilala Sharif Shamba mkoani Dar es Salaam, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Minde.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Grace Lwila, Hamjat alidai kuwa Hemedi alianza kuishi katika nyumba hiyo Julai 23, 2013 kwa mkataba wa mwaka mmoja ambao uliisha Julai 23, 2014.

“Awamu ya kwanza tulikuwa na mkataba, awamu ya pili alinilipa kodi bila mkataba lakini hakumaliza muda alikaa miezi mitano akasema anahama amenunua nyumba Magomeni,” alisema shahidi huyo.

Aliendelea kudai akiwa ndani ya nyumba hiyo mshtakiwa alitoa malalamiko kuwa kuna tatizo la shimo la maji taka kujaa mara kwa mara, hivyo aliomba amruhusu aende kwa mjumbe akaombe kuchimba shimo nje ya nyumba ili atapishe maji taka naye akamruhusu.

Alidai hata hivyo mjumbe hakutoa ruhusa hiyo na Ali alirudi kwa Hamjat akimwomba amruhusu achimbe shimo kwa ndani ya uzio wa nyumba.

“Aliponiomba nikamruhusu lakini nilimwambia achimbe kama ana hakika atafukia vizuri kama palivyokuwa, alichimba katika eneo la dirisha la mbele, baada ya hapo sikufuatilia tena kilichoendelea kwa sababu mimi nikishampangisha mtu huwa sitaki kumbughudhi,” alidai.

Alidai baada ya miezi mitano ya awamu ya pili akiwa safarini mshtakiwa alihama bila kumwambia na aliporejea ndipo alipompa taarifa kwamba amehama na akamtuma mtu apeleke ufunguo kwake.

Akielezea tukio la kuzikwa mwili kwenye nyumba hiyo, Hamjat alidai Februari 9, 2015 alipokea simu kutoka kwa polisi wakimtaka aende katika nyumba yake kuna tukio mshtakiwa alilifanya naye akaenda.

“Nilipofika niliwakuta polisi na watu wa afya kutoka Hospitali ya Amana, waliniambia kuna mwili umezikwa na wanataka kufukua niliwaruhusu. Niliondoka eneo hilo kwa kuwa sikuwa najisikia vizuri kushuhudia tukio hilo hivyo sikushuhudia mwili ukitolewa mahali hapo,” alisema.

Kabla ya ushahidi kuanza mshtakiwa huyo alisomewa mashtaka yake ambapo ilidaiwa Juni 12, 2014 alimuua ,Farahani Abdulsalum, mashtaka ambayo aliyakana mbele ya Hakimu Minde. Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…