Matrekta ya 'Kilimo Kwanza' yanaozea Dodoma

Mimi nipo Dodoma nathibitisha kwamba yapo. Area D barabara ya kwenda Morogoro sehemu inayoitwa Njedengwa. Yapo mengi sana tu.
Kimsingi mpango wa trekta ungeliwezesha taifa sana katika mambo ya uchumi. Lakini ugumu unakuja pale ambapo unalima halafu mipaka ya nchi inafungwa na hawa viwavi jeshi. Hivi ni nani anayetaka hasara. Mimi ninunue trecta huku nikijua kabisa, nachezea shilingi kwenye mdomo wa choo? Haiwezekani hata kidogo.
Wengi tunapenda sana kutumia mashine kwenye kilimo lakini sera za nchi hii ni kama moshi ndani ya tembe siku ya mvua kubwa. Sheria zinazunguka tu, hazieleweki kabisa.
Unajua miaka haifanani, serikali ingekuwa na sera za kuwalinda watu wake, mfano umelima mwaka wa kwanza na umepata hasara. Kimsingi kungekuwa na tathmini na serikali ione ni kwa namna gani inaweza kumsaidia mtu huyu lakini ndo kwanza wanachelea kumpokonya kila kitu. Haya ndiyo matokeo yake. Nakwambia watashusha bei lakini bado yataoza.

mliokuwa mnaulizia yapo wapi mmepewa data, nendeni huko mlikoambiwa harafu mje mkanushe hapa. tujue mbivu na mbichi
 
kama ulikuwa ukifuatilia suala hili kwa karibu nadhani ulisikia majina yaliyokuwa linked na hii biashara maana wengine tayari wapo mahakamani kwa makosa ya kusababisha hasara kama hayo matrekta yatakavyoozea hapo yalipo. Na hata ulisikia 'ugomvi' baina ya haohao waibaji!

Mimi ninachojiuzila (of course wote tunajua) inakuwaje serikari ilishatangaza kujitoa kwenye ufanyaji wa biashara alafu inapitia mlango wa nyuma kwa jina la SUMA JKT ambapo nimeona hata magaqri yao hayana namba za 'JW' bali 'T123 ABC' kama za walipa kodi wengineo wa mtaani.

Daima Muda umekuwa lafiki wa wasema ukweli na naamini hautawatupa hata kwenye jambo hili
Kama ilivyo kawaida serikali yetu huanzisha mipango kabambe ambayo kwa sababu moja au nyingine utekelezaji wake huwa mgumu.Miaka michache iliyopita serikali ilikuja na mpango wa KILIMO KWANZA. Ili kukamilisha azma hiyo power tilers na matrekta yaliagizwa kwa wingi nchini ili wakulima waweze kuyanunua.

Jambo la kusikitisha ni kwamba yale yaliyopelekwa kwenye 'yard' ya Dodoma ni mengi na hayanunuliwi. Kwa sasa yamesongwa na kufunikwa na nyasi ndefu. Inasikitisha, na pengine naweza kusema serikali ilikurupukia mpango huo.
 
kwa faida ya wanajf,

Ile yadi niya bwana mmoja anayejulikana kama MAIMU,AMBAYE alitajwa kama mwekezaji na mmiliki wa sehemu ya eneo ambapo wakazi wa njedengwa walibomolewa nyumba zao.

Pia anatajwa kutoka kijiji kimoja na naibu ambaye mlikuwa mnasema ni mchapakazi (Mwanri) na kunataarifa kuwa yeye ndiye aliyempa mchongo wa matrecta hayo.

Historia inaonesha katika ukumbi ambao ccm waliutumia kumpendekezea kikwete awe raisi,na bilali awe mgombea mwenza mwanzoni ulikuwa ni ghala la maindi,na huyu bwana (MAIMU) ndio aliyepigiwa upatu ili apate dili ilo la kuhamisha maindi na kuwezesha kufanyika kwa mkutano huo pale kizota.
 
Taarifa imejaa porojo, usanii ni kama imetoka mtaa wa mchikichini karikaoo kwa wauza mitumba.

Maswali yenu na mwenzako yamejibiwa, tena kwenye thread hii hii (achilia mbali habari kama hizi zilizoandikwa kwenye gazeti - tena la serikali Daily News wiki iliyopita). Na kuna thread nyingine inayotoa tangazo la punguzo la bei za matrekta yaliyoletwa kwenye huo "mpango" wa kilimo kwanza, sasa kama yananunulika bei itapunguzwa? Wapunguze na bei ya Umeme basi.

Hata kama ni ajira yenu kuitetea serikali hii (ambayo hata mwehu anajua kuwa imeshindwa ku-perform kwa practically kila jambo) basi angalau mjenge hoja, sio kung'ang'aniza hata visivyong'ang'anizika!
 
"Kilimo kwanza" was never intended to help the Tanzanian peasant. Ni mpango ulioandaliwa na wafanyabiashara ili kujinufaisha na mafungu ya pembejeo. Hakuna utaalamu wa kilimo au mifugo uliohusishwa kwenye andiko lote la mpango huu. Wapo wanaojiita Agroeconomists (sio wataalamu wa kilimo wala mofugo bali wachumi wa kilimo na mifugo) na wale wanaojiita Entrepreneurs (S&M enterprises) na walaji wakubwa wa TCCIA.

Serikali iliingizwa mkenge nao wakaenda kichwa kichwa.
 
Huyo jamaa aliona atauza matrekta kisa kilimo kwanza.
Kilimo kwanza sio matrekta pekee
OTIS
 
mliokuwa mnaulizia yapo wapi mmepewa data, nendeni huko mlikoambiwa harafu mje mkanushe hapa. tujue mbivu na mbichi

Mkuu tatizo ni kuwa tuna wakina Tomaso wengi sana humu.
 
Walidhani kwa kuyaweka barabarani, kwenye kiwanja cha mtu anayejijengea shule yake, yangenunuliwa wapi bwana, huyo aliyewadanganya ameshakula 10%, maisha yanaendelea
 
Niko Dodoma ni mji mdogo mbona sijaona matrekta hayo yapo eneo gani la Dodoma na mimi nikajionee sasa hivi kama ni kweli. Nitauliza na wahusika kama nitawakuta
Angalia mbele, siyo kuweka macho yako utosini!
 
Hapo umenena, huwezi kuweka investment ya hela kwenye kilimo pale unapofanikiwa kupata mazao serikali inapanga bei za ajabu na kibaya zaidi mipakani wanazuia wananchi wasiuze mazao yao nje. Upuuzi mtupu umejaa, kuwe na open/free market na serikali inunue mazao na kuhifadhi kama kutatokea janga la njaa na wananchi pia siyo wajinga hivyo kuuza kila kitu. Wananchi wapatiwe mikopo ya pembejeo na madawa na soko liwe huru uchumi utakuwa haya mambo ya kuleta tractors bila kuwa na strategy ya masoko ya mazao yetu tofauti na hapo utasikia serikali inadaiwa kulipa madeni ya IMF. WB kwa matreka yalisomama na kuozea chini.
 
kuna watu wanafikiri kwa kutumia ma.vi na si m.akalio tu.

oo lete ushahidi oo mimi nipo dodoma oo lete picha.

sasa lete ubishi tukupe namba ya maimu huyu mchaga alikuwa anataka kujenga shule hapa kushindana na mchaga mwenzake mmanga mwenye shule ya martin luther pale kisasa akachemsha alijenga fensi barabarani ikapigwa x akasalimuamri hiyo yadi kaachia mafisadi wameweka matrekta lukuki pale na kupitia haohao ndio wamefukuza watu kule njedengwa.

mkiipenda ccm yenu msijekutetea upuuzi humu.

nina hasira ningewachapa vibao pu.....fu.
 
Back
Top Bottom