GE2010 Matokeo ya Uchaguzi Mkoa wa Morogoro

GE2010 Matokeo ya Uchaguzi Mkoa wa Morogoro

Chromium

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2008
Posts
589
Reaction score
187
"...Kaka kituoni kwangu CCM 43, CHADEMA 65, CUF 3, APPt 1, zimeharibika 2..." Kwa njia ya SMS.
 
Hahahah! safi sana mkuu wapi hapokituo gani hicho mkuu? hapo ni za urais au mbuge mkuu?
 
Thanks for the update,
Kweli mwaka huu ni wa people's power.
 
Hizo za Urais, morogoro mjini kuna jamaa yangu anasimamia kituo. CCM walie tu!
 
"...Kaka kituoni kwangu CCM 43, CHADEMA 65, CUF 3, APPt 1, zimeharibika 2..." Kwa njia ya SMS.
Du,,ina maana kituo hicho kilikuwa na wapiga kura @110...!
Haya sasa, hii kweli ni rasharasha, mvua zaja!
 
"...kaka kituoni kwangu ccm 43, chadema 65, cuf 3, appt 1, zimeharibika 2..." kwa njia ya sms.

muongo wewe!! Kura bado hazijaanza kuhesabiwa unaanza uchimvi na kutaka kuleta vurugu!! Matoke ni mpaka kura zihesabiwe!!!
 
Mara nikaona mwanga na usiku ukawa mchana....
...na mchana huo huo Jukwaa likaandaliwa, Mkurugenzi wa NEC akafungua jalada, akaanza kusoma matokeo, huku sauti yake ikiwa na kitetemeshi, jasho jingi likimtoka, akavuta pumzi ndefu iliyoashiria kutojiamini na mashaka aliyokuwa nayo...!
 
Morogoro mjini yupo yule Myemen anaitwa Abood, sio rahisi kumshinda.

Waluguru bana kazi kweli kweli!
 
muongo wewe!! Kura bado hazijaanza kuhesabiwa unaanza uchimvi na kutaka kuleta vurugu!! Matoke ni mpaka kura zihesabiwe!!!

Hivi mzima wewe, saaa kumi ni mwisho wa kupanga mstari, na kama hakuna foleni ina maana hiyo saa kumi kituo ndio kinakuwa kimemaliza kazi yake, sasa hebu tuambie muda wa kuhesabu kura ni saa ngapi?, ina maana hao jamaa wakae hapo bila kufanya kitu chochote mpka wewe Zubeda useme?
 
mie nasubiri matokeo ya mwisho bana,by the way its a good sign kama ni kweli
 
inabidi utaratibu uwekwe ili kila matokeo yanayokuja yawekwe sehemu moja na iwe raisi kupata total
 
...na mchana huo huo Jukwaa likaandaliwa, Mkurugenzi wa NEC akafungua jalada, akaanza kusoma matokeo, huku sauti yake ikiwa na kitetemeshi, jasho jingi likimtoka, akavuta pumzi ndefu iliyoashiria kutojiamini na mashaka aliyokuwa nayo...!

...aliangaza pande zote asione msaada aliohitaji. Inavyoonekana alikuwa akimkumbuka Kivuitu. Alishituka toka lindi la mawazo baada ya kuguswa bega na Makame. Kwa hofu na unyonge alivaa miwani yake na kutakasa koo. Hakuwa na jinsi zaidi ya kuutangazia umma...
 
Back
Top Bottom