MATOKEO ya Kidato cha Nne a mjadala wa kuboresha Kufaulu

utafiti niliofanya kwa Ifm Iianonekana wengi from zenj(kwa asilimia), hata mwanafunzi bora Ifm 2007, 2008 walikuwa wazenj yaani first class na sio seminary. na hakutokea alieapta first class chuoni hapo kama sio hao vilaza wa zenj

nimekwambia tutor na tutorial assistants . Alaf mbona kama IQ inaleta utata,kwani kufundisha ifm mpaka uwe umesoma ifm? Pili kwani kutokea zenj mpaka uwe kama muhogo mchungu tatu,nitajie kwa majina walimu wapya tangu 2007 mpaka 2010. Tuangalie kama hamna waseminari,we vp? Alaf kama mwaka huo unaougang'ania hapakuwa na enrollment yoyote ya mseminari unataka ashindanishwe hata kama hayupo enrolled? Mi nimekupa range 2007-2010. Alaf katikati hapo ueleze bogus aliyepatikana kutoka kwenye taasisi unazozituhumu. Tulia mkuu tuendelee kujadili na mwisho tutaelewana!
 
unasumbuliwa sana na udini kuviita udsm,ifm mzumbe, sua vyuo vya kata.Hivi ni vyuo vya great thinkers backed by div 1 and 2 WANASEMINARI.VIPI HUKO TINISIA, MISRI,ALGERIA waislam wanadai nani kawanyanyasa?

Saizi inatakiwa Waislamu watoe tamko pia kuhusiana na matokeo ili wawe wanafaulu nusu kwa nusu maana kwenye matokeo ya form four wamenyanyaswa sana na wakristu
 
mwaka 2008, Shule moja inayoitwa High view sec school inayomikiwa na mmoja ya mfanya biashar mkubwa visiwani Zanzibar iliongoza Zanzibar kwa kufanya vizuri yaani ilitoa div 1 zaidi ya 15, div 2 za kumwaga kati ya watoto wsiozidi 50. hii ni mara ya kwanza kwa shule hiyo kutoa idadi kubwa wanafunzi. nadhani hata Baraza la Mitihani la Taifa Necta ilishtuka, iljihoji na ilitaka kujua haya ni matokeo ya Kweli?
Mwaka uliofuta NECTA ilituma ujumbe mzito katika shule hiyo, kwa maneno ya vijana iliwabana vijana sana vijana shule hiyo kwa kuweka Ulinzi mkali kwa usimamizi, ufanyaji wa mitihani, baadhi ya wajumbe kutoka NECTA Makao makuu Walishiriki kikamilifu kusimamia exam shuleni hapo. nasema walishiriki kusimamia, kuchunguza na kuzuia kila aina ya Ujanja, walifikia hata kuwasachi kabla ya exam. matokeo yake wanafunzi waliofanya Exam matukio yao sio mazuri.(naamini hata NECTA kwa hili hawatakanusha).
lKN sijui kama NECTA hufanya mkakati kama huu ktk shule ambazo huwa zinaongoza hasa za seminary? sijui kama wanshtuka kama walivyoshtuka High view? sijui hutumia mkakati kama walivyotumia huko Zenj?

LKN cha kujiuliza jee hawa ndio wanaopta first class Vyuo vikuu? au ndio bogas

Kwa kuwa NECTA hawajaenda huko shule za seminary kufanya hayo usemayo, hatuwezi kulizungumzia hilo kwa sasa. tuzungumzie tunayoyafahamu. shule zinazofanya vizuri ni kama vile tu timu za mpira zinazofanya vizuri, ni kama nchi zinazofaulu kiuchumi, ni kama hata akina wewe na mimi tunapojipanga vema mikakati, kimaisha unafanikiwa kwa namna fulani. haiwezekani baba mlevi, anatumia fedha ovyo, kuwe na amani na maendeleo nyumbani. nchi inayowekeza vizuri katika elimu, inakuwa na mipango mizuri na kuitekeleza, matokeo yataonekana. shule inayowekeza katika walimu wake, vifaa vya kufundishia, mipango makini inayotekelezwa, mafanikio yataonekana.

Lakini ni kweli pia kwamba shule ikishakuwa na historia ya kufanya vizuri, ni rahisi zaidi kuendeleza hali hiyo. kwa mfano, vijana wengi wanaofanya vizuri watakwenda kufanya interview katika shule zinazofanya vizuri, na kwa hiyo cream ya taifa inajazana sehemu hizo. kwa hiyo kama Interview wamefanya vijana 1,000 na wanaotakiwa ni 100, maana yake wakichukua the best 100, watakuwa wamechota cream tupu. sasa hapo kwa kuanzia vijana ni safi na kwa hiyo ukichanganya na mipango yao mizuri, kwa nini wasifanye vizuri? lakini ukianza kuwa na historia ya kufanya vibaya, basi hata wanafunzi unaopata ni wale walioshindikana sehemu nyingine, wavuta bangi, wakorofi, na hawana interest ya kusoma. hapo itakuwa ni vicious circle ya kufanya vibaya na vibaya zaidi. hapa shule itahitaji kufanya mkakati mkali sana wa kubadili mwelekeo huo. unaweza hata kuanza kwa kubadili jina, kubadili uongozi, kupaka rangi majengo, kuwekeza zaidi na kuleta vifaa zaidi, walimu wazuri zaidi kwa malipo mazuri zaidi. unaweza hata kwenda kukwapua walimu wazuri toka shule zinazofanya vizuri kwa malipo mazuri zaidi. hapo sasa ukianza kutoa matokeo mazuri, utapata vijana wazuri na utaanza mzunguko wa kuongezewa.

Kumbuka kwamba Seminari ni hasa kwa ajili ya Mapadri na wachungaji. lakini wanaojaa huko ni wale hasa wanaojiona kwamba wanao uwezo wa kufanya vizuri darasani na wanatumia seminari kama shule ya kawaida tu ili wasonge mbele. wanakwenda Seminari kwa sababu tu ya kufuata elimu nzuri na malezi mazuri. wazazi wengi wanapeleka watoto wao Seminari sio kwa sababu ya kutaka wawe wachungaji au mapadri, lakini ili wapate elimu nzuri ya huko.

nadhani tujikite kwenye mwelekeo kama huu, badala ya kunyooshea vidole wanaofaulu kwamba hawafai kufaulu, badala yake wale wanaofanya vibaya wajifunze kwa wale wanaofaulu kwamba wenzetu wanafanyaje? ili nao wafanye vizuri. kutafuta mchawi au visingizio haisaidii
 
utafiti niliofanya kwa Ifm Iianonekana wengi from zenj(kwa asilimia), hata mwanafunzi bora Ifm 2007, 2008 walikuwa wazenj yaani first class na sio seminary. na hakutokea alieapta first class chuoni hapo kama sio hao vilaza wa zenj

kwa iyo 2008 best student ifm Justus Mwemezi, ADB ni ustadh kutoka Pemba,au nachanganya? Unajua GPA yake utaumbuka mkuu Great Thinker wewe!
 
Leta ushahidi kutoka vyuoni ili tujadili.

Mimi sijasoma seminary ila watoto wangu wanasoma huko, bila ubishi kama mtoto ni kilaza kinachofanyika wazazi wanaamua kuwahamisha watoto wao vinginevyo anapewa nafasi ya kurudia na makisi zake zisipotosha njia ni nyeupe kuondoka shule hiyo, hapa namaanisha primary school, ile kusema kuwa kuna udanganyifu hoja hiyo naipinga kwa nguvu zote. Na ngoja nikuhakikishie kuwa usimamizi katika shule hizo ni balaa kuliko hata shule za kata na hizo unazoziita za madrasa. Pia ikumbukwe kama kuna mwanafunzi aliyetoka seminary akaenda chuo na matokeo yake yakawa si mazuri, hiyo inaweza changangiwa na mambo mengi. Pia kuna wanafunzi wengi wanafanya vizuri katika shule za serikali ila kwa sababu wao hawapembui pumba na mchele, utakuta wengi wamefaulu na wengi wamefeli pia, sasa wakija kuangalia wastani utakuta kuwa shule hizo haziongozi.
 
labda alikosea, mimi nakumbuka 2006-2005 ndio wapemba

uyu jamaa anaamua kuongea ongea tu hana facts anajisemea tu. Jameni tusijenge chuki kwenye jamii,anayefauli tumshangilie anayefeli tumpe moyo. Mwaka 2004 waislam walishafika hatua ya kuunda tume kuangalia kwa nini udahili wa waislam ni mdogo udsm! Yan ajabu! Kisha wakagundua kuwa huwa kila kozi ina cut off point wala hamna upendeleo. Imefika wakati tuache kuangaliana kwa dini,jaman binadamu wote ni sawa. Inatia shaka akina Muhogomchungu,ncha ya upanga na akina Zomba wanapoanza kuchokonoa wasiyoyajua.
 
Muhongo mchungu huwa balaa.
Ng'ombe akila majani ya muhogo mchungu anaweza kufa maana ni sumu. Naona huyu bwana kaamua kugawa sumu humu ndani! Mtasahau yote (EPA, Dowans, Katiba, Uchakachuaji wa Kura, Meya Arusha, Umeme na sukari kupanda, n.k)

Mbona shule kama Ilboru, Mzumbe, Kibaha zimekuwa zikifanya vizuri na hujasema ni za wakristo??

Ukiamua kutazama kila kitu kwa mlengo wa dini siku moja utakuja hapa na hoja ya "wenye daladala wanaonewa kwa kuwa ni waislam"
 
hawajaanza kufaulu leo . Ni toka zamani na Necta imekuwepo toka mitihani ilivyoanza
 
kinacho wasumbua ndugu zangu waislam ni inferiority complex kitaalamu.
kila kona wamepigwa bao sasa wamebaki kutafuta mchawi wao.
madrssa bana ahgrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
utafiti niliofanya kwa Ifm Iianonekana wengi from zenj(kwa asilimia), hata mwanafunzi bora Ifm 2007, 2008 walikuwa wazenj yaani first class na sio seminary. na hakutokea alieapta first class chuoni hapo kama sio hao vilaza wa zenj

muhogomchungu umekimbia. Nataka unieleze best student wa 2007/2008 uliosema umefanya tafiti na kukuta ni waZenji. Pia nipe jina hata moja la mseminary aliyesoma Ifm akakosa Upper Second. Ivi maneno ya 'no research no right to speak unaijua?' au unaleta dharau kwa maneno ya wanazuoni! Ivo ivo ndo mnavoenda mitaani mnawajaza waislam uongo kwa maneno ya kupika. Yani unasisitiza kabisa kuwa 2007/2008 hamna mseminari aliyepata First class ifm. Naombeni kitu kimoja,kama kuna ubishi wa kijiweni tuelezwe hapa tusije tukakuta tunaongea na watu wasio na uwezo wa kujenga hoja tukapoteza muda wetu. Muhogomchungu,kama huna facts we sema tu ili sie tuendelee na majukumu,tuendelee kuandaa material ili wadogo zenu wapate kumaliza vyuo na hatimaye taifa liongeze wataalam. Tusile chuki palipo na neema. Mfano mi wakati nasoma shule miaka 8 yote nilipanga nyumba 3 tofauti tofauti za Sikuwahi kuchukiwa na muislam,sikuwahi kusikia mwenye nyumba anawakebei wakristo,mpaka nyumba zinauzwa magomeni na kutufanya tuhame haikuwai kutokea kusikia uadui. Nenda vyuoni,ofisi serikalini,shule za mchanganyiko wote wanausoma udini kutoka HabariLEO, Mtanzania na redio Heri na Uhuru,bila kuacha vijarida flani. Mbaya zaidi njoo kwenye Media,siasa,ikulu ya kikwete,wote wanaongelea udini na chuki,kitu ambacho akipo kwenye jamii. Nyie endeleeni kutengeneza iyo sumu,siku itakapokuwa real ndo mtaona ubaya mlioutengeneza.
 
Na mtaumia saaaaaaaaaaaana tu. Sisi tunapeta endeelzeni chuki zenu na huku mnawanufaisha mafisadi papa.Waislamu wenye akili pelekeni watoto wenu shule za seminary waelemiki waacheni hao mavuvuzela wa CCM waliojivika uanaharakati wa kisalamu.
 
Saizi inatakiwa Waislamu watoe tamko pia kuhusiana na matokeo ili wawe wanafaulu nusu kwa nusu maana kwenye matokeo ya form four wamenyanyaswa sana na wakristu

Huku kwenye elimu hawaoni, na hawakuliona hilio tangu zama za kina tip tip! Uislam ilikuwa dini ya kwanza ya kigeni kwetu afrika (especially kwetu tz/tanganyika) kabla ya ukristu, Jiulize hadi tunapata uhuru, what did they do to take advantage of the earlier mover! Nadhani kama maendeleo yanahusu elimu hii dunia basi waache kuweka mambo ya udini! Naogopa kusema wasijewakadai wanaosahihisha mitihani ni wakristo!
 
ok, lkn bada ya necta kuona wazenj hawa wamefaulu na kukaribia tu kama seminary, necta iliruka, ikashtuka, ikavalia njuga. jee na huku smeinary ndio hivyo

Mkuu inategemea na historia ya shule, kama miaka yote ya nyuma ilikuwa ni mwendo wa Ziro za kumwaga, Four ndo usiseme, Three chache, Two kigogoo na One kiduchu n pocbly hakuna kabsa, afu nxt yr ndo matokeo yarise hivo, lazima mtu yeyote awe suspicious.
 
Halafu akili ya mwanafunzi darasani haina uhusiano wowote na dini yake unless it is bein filliped if not imposed on him. Tukumbuke kwamba "men are equal; it is not birth but virtue that makes the difference."- Voltaire
 
lkn pia wamepigwa mbao ktk mambo ya ufisadi, licha ya kusoma sana pia wanaongoza ufisadi huku wakiimarisha makanisa kwa pesa za walipa kodi. leo muumini anaiba mill19, anatoa sadaka mill 5. kanisa lisiwe juu?

mkuu ilo ni kweli ila ningeomba tusiutazame ufisadi kwa jicho la Dini. Akina Msabaha, nazir karamagi,RA,utawaweka wapi? Je akina EL,Yona,mkapa nao je!vp wapagani kama kingunge? Ufisadi hauna imani ni hulka tu. Pia ufisadi unakuja baada ya dini kuwepo,mfano mtu anakuwa tayari muislam au mkiristo anaishi maskini ila akiwa na age35,40 ,60 anakuwa fisadi,je apa dini yake itahusika? Kwa upande mwingne naelewa kuwa mafisadi wanatumia ela haramu kujenga nyumba za ibada,ni hatari. Mfano mwaka jana Rostam Aziz alitoa mamilion kwa KKKT bahati nzuri waliigomea ela haramu. Nakumbuka siku moja Sheikh machachari dsm aliulizwa swali na muumini wake,"sheikh mtu akitoa sadaka chafu inakubalika" akawajibu "sadaka haramu tutajengea choo". Haraka haraka hapa alimaanisha kuwa sadaka chafu itatumika kufanya vitu vichafu wala haitachanganywa na sadaka Safi. Anyway ni maoni yangu kwa ujumla.
 
Haya mambo ni ya kusikitisha kwani wanasema "mchuma janga hula na wakwao" hawa vijana kesho na keshokutwa ndio watakuwa kero mtaani kwa mambo mabaya kwa sabubu hawakupata elimu nzuri. Na madhara yake hayatakuwa na mipaka. kwa hiyo ni janga la Kitaifa
 
Back
Top Bottom