Tatizo viongozi wetu ccm sio wasikivu,sisi kama washabiki wafurukutwa tulitoa angalizo hapa,kwamba Lowassa asipewe nafasi ya kushiriki kampeni,kina Nape wakao humu kila siku hawakutaka kutusikiliza tuliwakumbusha uchaguzi wa ubunge arusha mjini jinsi lowassa na mgombea wake yule mama walivyotukosesha ushindi kutokana matatizo ya ufiasadi,tumerudia kosa lile lile leo arusha ambako husemekana ndio ngome ya arusha chama kinapoteza jimbo la pili huku kina millya wakitazama,siasa sio pesa ni strategies maana huwezi kuwanunua waoiga kura jimbo zima.Hili liwe fundisho kwa ccm lowassa atakicost chama zaidi huko tuendako,mwenyekiti ichukue hii kama changamoto even if unampenda rafiki yako ambae anadai hamkukutana barabarani kiasi gani,jamaa ni mzigo,iweje kila anapotia mkono na kuweka mgombea wake tunaanguka,hizo ni hasira za wananchi dhidi ya mafisadi na ufisadi.
Tatizo viongozi wetu ccm sio wasikivu,sisi kama washabiki wafurukutwa tulitoa angalizo hapa,kwamba Lowassa asipewe nafasi ya kushiriki kampeni,kina Nape wakao humu kila siku hawakutaka kutusikiliza tuliwakumbusha uchaguzi wa ubunge arusha mjini jinsi lowassa na mgombea wake yule mama walivyotukosesha ushindi kutokana matatizo ya ufiasadi,tumerudia kosa lile lile leo arusha ambako husemekana ndio ngome ya arusha chama kinapoteza jimbo la pili huku kina millya wakitazama,siasa sio pesa ni strategies maana huwezi kuwanunua waoiga kura jimbo zima.Hili liwe fundisho kwa ccm lowassa atakicost chama zaidi huko tuendako,mwenyekiti ichukue hii kama changamoto even if unampenda rafiki yako ambae anadai hamkukutana barabarani kiasi gani,jamaa ni mzigo,iweje kila anapotia mkono na kuweka mgombea wake tunaanguka,hizo ni hasira za wananchi dhidi ya mafisadi na ufisadi.
KIM,
..tatizo ni kwamba CCM imekuwa madarakani kwa muda mrefu lakini rekodi yake ya utendaji siyo nzuri.
..Lowassa amekwenda Arumeru wiki ya mwisho ya kampeni, sasa mnataka kumbebesha zigo la lawama za kushindwa.
..pia mgombea wa CCM hakuwa mzuri/sharp kulinganisha na yule wa CDM.
NB:
..waelekezeni Tume ya Uchaguzi wa-update daftari la kupiga kura sasa hivi. kinyume chake mnajenga kundi kubwa lenye hasira ya kupiga kura ya chuki dhidi ya CCM come 2015.
we unajua part aliyoplay toka kwenye mchakato wa ndani wa kura za maoni?
kama ni mfuatiliaji wa thread mbalimbali humu utakumbuka ushindi huu wa chadema niliuona mapema mimi, kuna thread niliiweka mapema hapa ndani baada ya sioi kupitishwa kuwa mgombea,nilisema japo watu waliichukulia kama utani,"chadema mkishindwa safari hii mjinyonge"
watu wa chadema walinishambulia sana wakijua nawasanifu lakini nilikua nimeouona mkono wa lowassa ulivyokigawa chama arumeru,lowassa is a disaster!
Mjadala upewe uzito unaostahili. Tusianze kutetea na kusafisha CCM hapa kwa kisingizio cha kumshughulikia Lowassa. Aliyeshindwa ni CCM na mfumo mzima wa chama hicho. Mkapa, Lowassa, Kikwete, Msekwa, Wassira, Nape, Nchemba, Lusinde na wote walioshiriki siasa hizo ndani ya chama. Naogopa tukim-single out Lowassa tunajikuta tunatuma ujumbe nusu nusu kwa jamii. La msingi ni hili hapa: Ushindi huu wa Chadema ni wake up call kwa CCM nzima!
..hata Kigamboni kura za CUF + CDM ni zaidi ya kura za mgombea wa CCM aliyeshinda.
Nilimshauri hakusikiliza!. Pia nitamshauri aachane na ndoto za urais 2015, Chadema inachukua nchi!.
Hili la Arumeru lime conclude kwamba huyu Bwana pamoja na tambo na mbwembwe zote hana mvuto kiasi hicho tunachotaka kuaminishwa. Hata Urais anaotaka kugombea ataangukia pua,, hili ndilo litakuwa pigo lake la mwisho na pengine litamuathiri kabisa kiafya. Wako wanasiasa wengine wenye umri mzuri tu wa kugombea urais,, ila si huyu tia maji tia maji
Sasa unapokuwa na nguvu huku unapigwa mchana kweupe maana ya nguvu zako ni nini? Ni kwamba wako wenye nguvu kuliko wewe. Mtoto wako anaporefuka,,, anakuona wewe umekuwa mfupi.Kuwa na nguvu!! Nguvu anazo, na ndio maana hata wewe leo unamjadili. Hapa ukweli ni kwamba nguvu zake zitaiponza CCM na Arumeru ni ishara tosha kwamba nguvu za fedha zina mwisho wake,