Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

Matokeo Kidato IV: Utata mtupu!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Kikao cha kupitisha Viwango Vipya vya Ufaulu vilivyotumika kwa Kidato cha Nne kilihusisha Wizara ya Elimu na Ufundi,NECTA na TCU. Nyaraka za kikao hicho kilichofanyika Disemba mwaka jana,zinaonesha kuwa kikao husika kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dr.Shukuru Kawambwa na Katibu wa Kikao alikuwa Naibu wake Bwana Phillipo Mulugo.

Kwa upande wa NECTA,waliwasilishwa na Mwenyekiti wake Prof.Rwekaza Mukandala na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Dr.Joyce Ndalichako.Pia alikuwepo Mjumbe kutoka Mamlaka ya Vyuo Vikuu nchini-TCU ambaye alikuwa ni Prof. Sifuni Ernest Mchome (ambaye baadaye akawa Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Ufaulu wa Kidato cha Nne!)

Kikao hicho kiliidhinisha kutumika kwa viwango hivyo vipyakwa kidato cha nne na cha sita. Wajumbe wote wa Mkutano walikubaliana na viwango vipya na matumizi yake kwa kidato cha nne 2012.

Habari zaidi zimeripotiwa katika Mwananchi la leo

Je, kuchunguza na kutaka kubadili matokeo haya si dharau zilizopitiliza kwa watanzania? Je, ni halali kwa Prof.Mchome kuhudhuria kikao na halafu kuongoza Tume ya Kuchunguza? Watanzania tumedharauliwa,sasa tuchukue hatua gani? Nani mtanzania muungwana atawaamini watu hawa kwasasa?
 
issue hap nikifikiria mikopo ninayokatwa kila mwezi kwa ajili ya watoto wangu hawa waliomaliza 2012 na kupata Div iv na zero du nashindwa hata kusimamia ukweli jamani wa standardize tu ili hata tugawane hasara wajameni.... please naombeni msamaha..
 
Je, ni halali kwa Prof.Mchome kuhudhuria kikao na halafu kuongoza Tume ya Kuchunguza? Watanzania tumedharauliwa,sasa tuchukue hatua gani? Nani mtanzania muungwana atawaamini watu hawa kwasasa?
Alikuwa na majibu kabla ya kuanza kazi ya uchunguzi kwenye tume.
In fwakt, iyo tume ilitakiwa iwe na mtu mmoja tu!
Huyohuyo mwenyekiti, huyo katibu, huyo mjumbe, huyohuyo nafasi zooooote.!
Na Mtu huyo ni Prof. Mchome (I doubt huu uprofesa wa kibongo, bora hata maji marefu aliamua kujipa)
 
Kama ni kweli walikubariana na wakabadiri viwango ni haki ya wanafunzi kurejeshewa viwango vya mwanzo maana vya sasa ni kweli vipo juu. Lakini wahusika wote waliokaa na kukubariana maamuzi haya ya kipuuzi ambayo yamelisababishia taifa aibu na hasara ya muda na pesa bila kusahau roho za vijana wetu zilizopotea wanapaswa wajipime kama bado wanastahili kuwa viongozi.
 
Kumbe walikubaliana Wonders Never End in Tanzania

Mbaya zaidi wakaamua kumpa shavu Prof Mchome wakati yeye ni sehemu ya matokeo
 
Kama ni kweli walikubariana na wakabadiri viwango ni haki ya wanafunzi kurejeshewa viwango vya mwanzo maana vya sasa ni kweli vipo juu. Lakini wahusika wote waliokaa na kukubariana maamuzi haya ya kipuuzi ambayo yamelisababishia taifa aibu na hasara ya muda na pesa bila kusahau roho za vijana wetu zilizopotea wanapaswa wajipime kama bado wanastahili kuwa viongozi.

Obwato hakuna haki yoyote kwa mwanafunzi kuwekewa kiwango kidogo cha ufaulu huu ni udhalilishaji kwa mwanafunzi mwenyewe, na kama kweli tunataka kutengeneza taifa la watu washindani kwenye nyanja za ajira na kujiajiri ni bora tukamaintain viwango hivyo vikubwa ili tutoe mazao bora! kuwawekea viwango vidogo vya ufaulu ni kuwadanganya wanafunzi wenyewe kuwa wao ni bora na wanapofika kwenye ushindani na wengine wanaonekana vilaza tu! Just thinking outside the Box!
 
kama walikubaliana kwanini mwenyekiti wa tume ya kuchunguza tatizo la kufeli ndio awe anapinga yale yale ambayo walikubaliana kwenye kikao cha kupitisha alama mpya? Ilikuaje Pinda amchague mtu yuleyule aliyehusika katika kikao cha kupitisha alama mpya ambazo zimeleta utata?
Ninaamini maamuzi ya awali yalikua na mantiki,kufeli huku kumetokana na sababu lukuki ambazo wengi wamezijadili ukitoa hii ya kisiasa iliyoingizwa
 
Hakuna wakati taifa letu limechanganyikiwa kama sasa. Fikiria walioidhinisha matokeo ndio wanaotengua wakingali madarakani. Ilikuwaje Lukuvi atoe tamko la wizara ya elimu wakati waziri husika na naibu wake wako. Mimi nilidhani walishajiuzulu. Mwenyekiti wa NECTA na Katibu mtendaji kama wanajiamini na elimu zao na wangependa kutunza heshima zao waondoke madarakani kabla matokeo mapya hajatangazwa vinginevyo wote ni wahuni 2
 
Huu kweli ni utata! Yaani muongoza tume alikuwa na majibu kabla ya utafiti.
 
Hii ndiyo made in Tanzania, huwezi kuipata sehemu yoyote duniani.
 
Hii nchi utadhani haijawahi ongozwa na kiongozi kama Mwl. Nyerere!!!
 
Kama ni kweli walikubariana na wakabadiri viwango ni haki ya wanafunzi kurejeshewa viwango vya mwanzo maana vya sasa ni kweli vipo juu. Lakini wahusika wote waliokaa na kukubariana maamuzi haya ya kipuuzi ambayo yamelisababishia taifa aibu na hasara ya muda na pesa bila kusahau roho za vijana wetu zilizopotea wanapaswa wajipime kama bado wanastahili kuwa viongozi.
Samahani Mkuu.Umemaliza kidato cha Nne mwaka gani? Viwango vya juu! Umetumia vigezo gani? Umewahi hata kuona moja ya mtihani wa NECTA mwaka jana? USPUMBUZIKE NA HOJA ZA WANASIASA. Heri yao ambao hawajashikiwa akili zao na wanasiasa uchwara!
 
Hii ndiyo made in Tanzania, huwezi kuipata sehemu yoyote duniani.

Hahaaa.... grafani11 Umeonaee....Hii ndiyo nchi yetu bana, nchi ya asali na maziwa... Namkumbuka Mkapa aliwahi kusema anaona raha saana kuongoza nchi kama Tanzania. Sikuelewa maana yake lkn sasa naelewa kwanini alijinasibu hivyo.

Nakumbuka pia kuna mtu tulibishana naye sana humu nikamwambia endapo ni kweli wizara ingekuwa haijui kilichotokea amini usingemkuta Ndalichako ofisini...sasa nashukuru unabii wangu umetimia, Kuwa Wizara ndiyo muhusika mkuu wa kutoa maelekeo kuwa Viwango vipya vitumike kuanzia 2012 na ndiyo yule yule gesimba aliyeliagiza baraza la mitihani ndiye huyo ananukuu tamko la kina lukuvi eti wadau hawakuhusishwa!!
 
Hahaaa.... grafani11 Umeonaee....Hii ndiyo nchi yetu bana, nchi ya asali na maziwa... Namkumbuka Mkapa aliwahi kusema anaona raha saana kuongoza nchi kama Tanzania. Sikuelewa maana yake lkn sasa naelewa kwanini alijinasibu hivyo.

Nakumbuka pia kuna mtu tulibishana naye sana humu nikamwambia endapo ni kweli wizara ingekuwa haijui kilichotokea amini usingemkuta Ndalichako ofisini...sasa nashukuru unabii wangu umetimia, Kuwa Wizara ndiyo muhusika mkuu wa kutoa maelekeo kuwa Viwango vipya vitumike kuanzia 2012 na ndiyo yule yule gesimba aliyeliagiza baraza la mitihani ndiye huyo ananukuu tamko la kina lukuvi eti wadau hawakuhusishwa!!
Eti wanajifanya hawajui kilichosababisha watoto kufeli mpaka wakaunda tume wakati hata mwenyekiti mwenyewe wa tume huyo anayejiita Profesa Mchome anajua na alikuwepo kwenye kikao kilichobadilisha viwango vya madaraja.
 
Samahani Mkuu.Umemaliza kidato cha Nne mwaka gani? Viwango vya juu! Umetumia vigezo gani? Umewahi hata kuona moja ya mtihani wa NECTA mwaka jana? USPUMBUZIKE NA HOJA ZA WANASIASA. Heri yao ambao hawajashikiwa akili zao na wanasiasa uchwara!
Mkuu taratibu, hasa hapo kwenye rangi ya maji bahari.
 
Hii serikali haina authority ya kutuongoza hata dakika moja iliyoko mbele yetu inapaswa kuwa dissolved na uchaguzi mwingine kuitishwa hivi kweli itakuwaje tuendelee na serikali ambayo kila mtu ni muongo,waongo hawana legitimacy ya kutawala how comes Waziri na naibu wake walioshiriki katika maamuzi ya kubadilisha mfumo wa kuweka maksi leo wanageukia maamuzi yao kisiri na kuyakataa halafu mbele ya umma wakadanganya wanaandaa tume ya kutafuta sababu wakati hata mwenyekiti wa kamati yeye mwenyewe pia anahusika ghosh what an imbarrasement
 
Back
Top Bottom