Kuna mwanamama aliwahi nipa ushuhuda kuwa matiti yake yalianza kuanguka akiwa na miaka 23 kutokana na mitomaso aliyokuwa anafanyiwa na mpenzi wake wa kwanza. Aliendelea kwa kusema kuwa, kabla ya kuanza michezo na wanaume alikuwa na chuchu dodo zilizosimama na kuchoma.
Hivi ni kweli kuwa matiti ya mwanamke yanapopapaswa na viganja vya mwanaume hupelekea kuanguka na kuwa ndala?
Hivi ni kweli kuwa matiti ya mwanamke yanapopapaswa na viganja vya mwanaume hupelekea kuanguka na kuwa ndala?
- Tunachokijua
- Binadamu kama walivyo wanyama wengine wanaopatikana kwenye Kundi la Mamalia huwa na sifa mbalimbali zinazowatenganisha na viumbe wengine. Baadhi yake ni;
- Kuwa na manyoya
- Kuwa na tezi za jasho
- Huwa na tezi maalum za kuzalisha maziwa, maarufu kama mammary glands
- Huwa na mifupa 3 kwenye sikio la kati
- Uwepo wa eneo la Neocortex kwenye ubongo
- Kuwa na meno yaliyotofautishwa muundo na muonekano
- Moyo wenye vyumba 4 pia chembe nyekundu za damu zisizo na kiini (Nucleus) katikati
Kuanguka baada ya kushikwa na wanaume
JamiiForums imepokea madai haya na kufanyia kazi kwa kuzungumza na wataalam wa afya. Katika uchunguzi wetu, tumebaini mambo yafuatayo;
- Ukuaji wa matiti ya mwanamke huongozwa na mfumo wa taarifa za urithi (Genes) pamoja na mfumo wa vichocheo vya mwili (Homoni)
- Hakuna mfumo mmoja wa ukuaji wa matiti unaofanana kwa wasichana wote. Baadhi hukua mapema na baadhi huchelewa
- Kushikwa matiti na wanaume hakuwezi kusababisha kudondoka (kuanguka) kwa matiti, au hata kuongezeka ukubwa wake.
Pia, kwa mujibu wa Taasisi ya Nemours Teens Health, kuvaa au kutokuvaa sidiria hakuwezi kusababisha kukua, kudumaa au kudondoka (kuanguka) kwa matiti. Nadharia hizi ni uzushi usio na uhalisia kisayansi.