Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,615
- 40,163
Benki ya CRDB imetangaza kufunga huduma katika matawi yake yote kwa siku tatu kuanzia Septemba 5 hadi 7 mwaka huu.
Kufungwa kwa matawi hayo kunalenga kutoa nafasi kwa wataalamu kufanya maboresho na kuweka mifumo ya kisasa ili kuongeza ufanisi huduma zinazotolewa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo kwa umma, ndani ya kipindi husika, huduma zote za benki hazitapatikana kwa namna tofauti ambapo Ijumaa ya kuamkia Septemba 5, 2025 watu hawatakuwa na uwezo wa kupata huduma kwa saa mbili.
Pia, wateja hawatakuwa na uwezo wa kupata huduma usiku wa kuamkia Ijumaa kuanzia saa 6:00 usiku hadi saa 8:00 usiku.
Usiku wa kuamkia Jumapili ya Septemba 7, 2025, huduma zote hazitapatikana kwa saa sita kuanzia saa 6:00 usiku hadi saa 12:00 alfajiri.
Mbali na hilo, CRDB imesema huduma zitakazopatikana nje ya vipindi vya kusitishwa huduma ni ATM ambapo watu wataweza kutoa fedha na kuhamisha fedha.
Kufungwa kwa matawi hayo kunalenga kutoa nafasi kwa wataalamu kufanya maboresho na kuweka mifumo ya kisasa ili kuongeza ufanisi huduma zinazotolewa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo kwa umma, ndani ya kipindi husika, huduma zote za benki hazitapatikana kwa namna tofauti ambapo Ijumaa ya kuamkia Septemba 5, 2025 watu hawatakuwa na uwezo wa kupata huduma kwa saa mbili.
Pia, wateja hawatakuwa na uwezo wa kupata huduma usiku wa kuamkia Ijumaa kuanzia saa 6:00 usiku hadi saa 8:00 usiku.
Usiku wa kuamkia Jumapili ya Septemba 7, 2025, huduma zote hazitapatikana kwa saa sita kuanzia saa 6:00 usiku hadi saa 12:00 alfajiri.
Mbali na hilo, CRDB imesema huduma zitakazopatikana nje ya vipindi vya kusitishwa huduma ni ATM ambapo watu wataweza kutoa fedha na kuhamisha fedha.