Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

Matapeli wa miaka ya 90's walikuwa balaa sana

mpasta

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2011
Posts
919
Reaction score
2,007
Leo nimekumbuka Miaka ile ya 90's Nchini Tanzania kulibuuka utapeli wa ajabu sana mpaka mwanamuziki HEMEDI MANETI wa bendi ya CCM ya Vijana Jazz akatunga wimbo unaitwa "OGOPA MATAPELI".

Mwaka 1993 nikiwa mkoani nakumbuka kuna tapeli aliwaliza watu balaa. Timu ya SIMBA SC ilikuja Mkoani Mtwara kucheza na timu ya Bandari Mtwara. Sasa baada ya mechi usiku wake washabiki wa Simba wakaandaa hafla ya kuwapongeza Simba SC hasa ukichukulia mwaka huo Simba SC alikuwa anafanya vizuri kwenye mashindano ya CAF.

Tapeli mmoja mgeni machoni kwa watu nae akatinga kwenye sherehe na tracksuit zake nyekundu nadhifu, akajichanganya kwenye umati wa washabiki.

Dada mmoja mrembooo akajilengesha, maana alikuwa anamtafuta mchezaji wa SIMBA akiitwa DAMIAN KIMTI, alikuwa anampenda sana kwa uchezaji wake. Enzi zile hamna TV, hamna magazeti ya kutosha, Mastaa unawajua kwa jina tu kupitia Redio.

Jamaa akamdanganya dada wa watu yeye ndio DAMIAN KIMTI akala uroda wa bure kwa dada yule. Kesho yake asubuhi na mapema jamaa akaibukia sokoni na makapu yake akiwa amevalia tracksuit zake nyekundu anatembea kwa machejo kama mchezaji mpira kweli. Watu wanaonyesha kwa vidole KIMTI yuleeee anapita KIMTI yuleee, basi sokoni anapewa tu mchele, maharage na bidhaa zinginezo bure kwa jina la KIMTI kumbe KIMTI feki.

Sasa balaa likaibuka, Simba wameshasafiri kurudi DSM kuendelea na mechi zao,KIMTI feki bado anaonekana mtaani hasafiri, ndipo dada wa watu uzalendo ukamshinda akamchana hadharani, "Nimekupa uroda nikijua ninampa uroda DAMIAN KIMTI kumbe mshenzi tapeli tu wewe"....

Kila zama na kitabu chake, zama hizi za Kidigitali matapeli wanakutapeli kwa njia za kidigitali mara nyingi wala huwaoni ila zama zile lazima muonane uso kwa uso hivyo walikuwa wanatumia akili nyingi sana....

Je umeshawahi kutapeliwa na wewe mpaka ukajiona ni mjinga??
 
Kipind niko primary walikuja watu wawili kwa jirani wakamkuta housegal na mtoto wa mwenye nyumba wakawaambia mama yenu katuagiza vitenge anataka akashone.

Na yule mama alikua anapenda vitenge so alikua navyo vingii sasa kuuliza kitenge kipi wakasema tupe tu vyote ataenda kuchagua mwenyew vingine atarud navyo basi dada wa watu akakusanya vyote na begi akawapa kwa ajili ya kubebea.

Jioni maza house anarudi katika story dada akamwambia kuhusu wale wageni, mama akajua ashatapeliwa. Akampeleka yule h/girl polisi kutoa maelezo ila ikagundulika hahusiki dada akaachiwa na vitenge vikaenda.

Zamani watu walikua wanaiba kirahisi sio kama saivi
 
Kipind niko primary walikuja watu wawili kwa jirani wakamkuta housegal na mtoto wa mwenye nyumba wakawaambia mama yenu katuagiza vitenge anataka akashone.

Na yule mama alikua anapenda vitenge so alikua navyo vingii sasa kuuliza kitenge kipi wakasema tupe tu vyote ataenda kuchagua mwenyew vingine atarud navyo basi dada wa watu akakusanya vyote na begi akawapa kwa ajili ya kubebea.

Jioni maza house anarudi katika story dada akamwambia kuhusu wale wageni, mama akajua ashatapeliwa. Akampeleka yule h/girl polisi kutoa maelezo ila ikagundulika hahusiki dada akaachiwa na vitenge vikaenda.

Zamani watu walikua wanaiba kirahisi sio kama saivi
ila hapo tayari tapeli alishafanya HOME WORK yake mapema, akajua mama mwenye nyumba ni mpenzi wa kuvaa vitenge.....
 
Enzi hizo nikatinga mkoa flani nikajifanya mimi Prof J,enzi zile za zama za mawe,nikalamba advance payment,siku ya show kuna mwana akastukia chezo maana nilichokuwa nafanya kwa Stage hakifanani na mzee wa mitulinga,nikajifanya naenda chooni mazee hizo mbio nilizotimua Subaru haikamati,mbele kwa mbele nikadandia fuso la viazi ndiyo kimojaaa.
 
Leo nimekumbuka Miaka ile ya 90's Nchini Tanzania kulibuuka utapeli wa ajabu sana mpaka mwanamuziki HEMEDI MANETI wa bendi ya CCM ya Vijana Jazz akatunga wimbo unaitwa "OGOPA MATAPELI".
Mwaka 1993 nikiwa mkoani nakumbuka kuna tapeli aliwaliza watu balaa. Timu ya SIMBA SC ilikuja Mkoani Mtwara kucheza na timu ya Bandari Mtwara. Sasa baada ya mechi usiku wake washabiki wa Simba wakaandaa hafla ya kuwapongeza Simba SC hasa ukichukulia mwaka huo Simba SC alikuwa anafanya vizuri kwenye mashindano ya CAF. Tapeli mmoja mgeni machoni kwa watu nae akatinga kwenye sherehe na tracksuit zake nyekundu nadhifu, akajichanganya kwenye umati wa washabiki. Dada mmoja mrembooo akajilengesha, maana alikuwa anamtafuta mchezaji wa SIMBA akiitwa DAMIAN KIMTI, alikuwa anampenda sana kwa uchezaji wake. Enzi zile hamna TV, hamna magazeti ya kutosha, Mastaa unawajua kwa jina tu kupitia Redio.

Jamaa akamdanganya dada wa watu yeye ndio DAMIAN KIMTI akala uroda wa bure kwa dada yule. Kesho yake asubuhi na mapema jamaa akaibukia sokoni na makapu yake akiwa amevalia tracksuit zake nyekundu anatembea kwa machejo kama mchezaji mpira kweli. Watu wanaonyesha kwa vidole KIMTI yuleeee anapita KIMTI yuleee, basi sokoni anapewa tu mchele, maharage na bidhaa zinginezo bure kwa jina la KIMTI kumbe KIMTI feki.

Sasa balaa likaibuka, Simba wameshasafiri kurudi DSM kuendelea na mechi zao,KIMTI feki bado anaonekana mtaani hasafiri, ndipo dada wa watu uzalendo ukamshinda akamchana hadharani, "Nimekupa uroda nikijua ninampa uroda DAMIAN KIMTI kumbe mshenzi tapeli tu wewe"....

Kila zama na kitabu chake, zama hizi za Kidigitali matapeli wanakutapeli kwa njia za kidigitali mara nyingi wala huwaoni ila zama zile lazima muonane uso kwa uso hivyo walikuwa wanatumia akili nyingi sana....

Je umeshawahi kutapeliwa na wewe mpaka ukajiona ni mjinga??
Dah Damian Kimti R.I.P ticha wangu huyu wa primary
 
Kuna jamaa yangu anatoka Tanga likizo kipindi kile mabasi ya mikoani yanaanzia mnazi mmoja,alikuwa anakuja na begi la spear za magari kwao kulikuwa na magari mabovu kwa hiyo kufanya jambo ili aje tupige mpunga,kufika maeneo ya Kariakoo akakutana na wazee wa kanyaboya,likadondoshwa waleti mwana akaliokota jamaa mwizi akajifanya na ameliona waleti kama vipi wakagawane minoti,huku nyuma kuna jamaa analalamika kapotea waleti yake yenye mifeza kibao,jamaa yangu akaingia mazima,akaambiwa nipe begi nikushikie harafu tukutane maeneo flani tukafawane..jamaa akaachia begi akabaki na waleti yenye mikaratasi.
 
Enzi hizo nikatinga mkoa flani nikajifanya mimi Prof J,enzi zile za zama za mawe,nikalamba advance payment,siku ya show kuna mwana akastukia chezo maana nilichokuwa nafanya kwa Stage hakifanani na mzee wa mitulinga,nikajifanya naenda chooni mazee hizo mbio nilizotimua Subaru haikamati,mbele kwa mbele nikadandia fuso la viazi ndiyo kimojaaa.
 
Eeeh nasikia baada ya kustaafu soka akaanza kufundisha KIFARANSA mashuleni, alifariki nadhani miaka ya 2000 mwanzoni nadhani
Kafariki juzi juzi hapo 2020
Screenshot_20220424-100516_Samsung Internet.jpg
..........alikua pale st.mary ya tabata akifundisha kifaransa na hisabati
 
Na nyakati zile sura za wachezaji zikikuwa kwenye magazeti tu. Qureshi Ufunguo nilimuona kwenye gazeti Simba ile ya 2003 mara moja tu. Sura yake nishaisahau.
Kuna jamaa alikujaga mkoani kwetu enzi za chemsha bongo ina hit eti anajifanya Nigga J, basi watu wakawa wanamshobokea ananunuliwa mihogo ya kukaanga na kachumbari bure. Nigga J gani hana hata ela ya kununua mihogo. Kakalili mistari anawashushia rhymes wana.
Looking back nacheka sana.
 
Back
Top Bottom