Matapeli wa mapenzi humu JF

Matapeli wa mapenzi humu JF

Wandugu!
Tafadhali Chukueni tahadhari na watu (wanawake kwa Wanaume) wanaotangaza kuwa eti wanataka wake au waume huku jamiiforums kumbe wana agenda ya siri nasema haya kwa sababu yamenikuta jana nilimpata mdada humu humu Jamiiforums tukawa tunawasiliana na jana mwanzoni tulikubaliana tukutane MLIMANI CITY baadae akabadilisha akasema tukutane pale MWENGE (Maryland Bar) mi nikakubali akaja kweli muda tuliokubaliana saa 10:30 jioni (Maryland Bar Mwenge ghafla nikavamiwa na group la vijana wapatao wa 4 wanadai ati kwa nini namsumbua kwa kumtongoza kila siku mke wake duuh! kilichonisaidia ni mbio zangu maana jamaa walishuhudia vumbi tu! labda walichofaidi ni bia niliyokuwa nimebakisha hapo mezani lakini kama ndo mpango wao wanipore wamenoa!! KWA HIYO TAFADHALINI kuweni makini,vinginevyo MTALIA SIKU MOJA

Mkuuu funguka bwana, ulichat na ID gani humu JF, hio KUSEMA BILA KUMLIPUA MUHUSIKA SI DAWA! Ukute big name!!!! LOL! Sipati picha ukaona umejipatia BONG YA SHORIIIII!BURE BURE! USHAJIPANGA KUMUONJAAA!!!!LOL! Ndo dawa yenu waonjaji!!!!! Pale Maryland kuna guest kibao karibu ikiwamo Raibow Hotel Na Kebbys Hotel! Sijui ulilipia chumba ipi? LOL! Anyway siku zote BLIND DATES ni mbaya unaweza chat na mtu kumbe Mama/Dada yako, bora wewe mke wa mtu!! LOL!
 
Mkuu Andreakalima; huwezi kuuza utumbe halafu usinuke

Pole
 
Katika maisha yote yanawezekana kabisa, hili lililokutokea lisiichafue JF natetea kwa sababu kuna watu wamepatana JF na mpaka sasa wanaishi kwa amani. Mimi mwenyewe ni mfano wa watu waliopata mchumba JF... I swear sikutegemea kupata msichana wa namana hii popote pale katika maisha ya kawaida but JF imenipatia msichana like an angel vile.

Nina amani sana naye, I believe ana amani sana nami pia! Swala la msingi chunguza njia zako ulizotumia mpaka kutaka kuonana na huyo dada... kama ni mke wa mtu kakufanyia hivyo wewe na huyo mke kuna kasoro ambayo si lazima tupeleke lawama JF...!

Nitaitetea JF mpaka yanikute kama yako ila nahisi vigumu maana nilisha pata nilipohitaji mchumba na sasa naishi hapa kama uwanja wa nyumbani sijawah tongoza tena na haitatokea... kama kuna mtu kaingia hapa kwa kufanya JF ni uwanja wa Fisi tegemea zaidi ya hayo.

Mshukuru Mungu amekupa warning ya maisha.

MY TAKE:
Jambo analo lala mika mtoa mada lipo na linahitaji umakini sana hasa kwa wale ambao wanakutana hapa ndani na within a week wanakuwa wamefahamiana na kujuana this is too risky.
Haimaanishi watu wasiende MMU au Love Connect but you always have to take risk before you achieve.
Narudia kuwa nimepata msichana ambaye anafanana sana nami kwa mwenendo wake hapa JF... I hope ntampenda daima nilipokuwa natafuta sikutegemea kuwa ntaweza pata such a lady! So hili swala la mtoa maada lisipuuziwe na vilevile lisiwaondolee ujasiri wenye bahati zao kukutana hapa.

Ni vizuri ukimtaja huyo muhusika hapa.
 
Ungekuwa serious ungemtaja huyo memba ili Kongosho nae asibambwe manake hajui kukimbia.
That is why i dont believe in cyber love, lol
 
Last edited by a moderator:
umhh! hii kali.. nadhani mabazazi wa JF wamekusoma
 
aisee ww ulienda kichwa kichwa sana, mtu ambaye hamjaonana kwanza hutakiwi kumwambia umevaaje, pili isiwe sehemu open kama baani kituo cha gari kinafaa sana, tatu weka cm vibration na jikinge sehemu fulani nyeti ili akishuka na kukutafuta iwe rahisi kumuona yeye na nyendo zake, mwisho usimwamini sana
 
Hahaha! The imaginations itself is killing me! Dah... JF is never boring... Poleee...
I second that as well.

@Thread starter; To win a girls heart, it takes much more than money and good looks....I recall a wise man once said that, you can be the best looking person in the world, but if your personality is ugly then you're ugly too....Lazima wewe ujipende kabla ya kupendwa.


Vipi umfate yeye sehemu anayo taka yeye, wakati yeye ndo ailikuwa anatafuta mchumba, ilitakiwa yeye akufate tena sehemu unayo taka wewe.


Ushauri wa busara; wanaume wengine acheni kujidharaulisha mbele za wanawake :biggrin:
 
ingekuwa poa kama ungeiweka hewani id yake mana anaweza kuwa anaendela kuitumia!ila lakini hata ukiitaja hatujuani humu,na ukweli ni kwamba anaweza kuja na id nyingine na swaga zingine kabisa!all in all kupata mpenzi kwa njia hii one has to be more than mjanja i see!pole sana mkuu!
 
Sasa sitafuti demu tena labda fb maana mie sina mbio wala similiki AK47
 
acha uongo, pale maryland hamna wahuni wala wa kukufanyia fujo labda kama uliiba spanner za wale mafundi magari pale nje. Istoshe pale kuna ulinzi wa kutosha hata ukisahau simu kesho yake unaikuta. Ungesema Yenu bar ningekubali. Hata hivyo jf hamna mtu wa kukufanyia hivyo labda useme hii ni stori umetunga. Mia
naona umekasirika mkuu....jamaa kakipakazia kijiwe chako eh....!
Mwambie bana tena leo nitakuwa hapo mida ya saa kumi jioni, nina miadi, kama kikinuka nitaku PM tukisanue wote, si una namba ya IGP Mwema... Mwambie aweke Defender stand by pale maeneo ya njia panda ya ITV
 
Katika maisha yote yanawezekana kabisa, hili lililokutokea lisiichafue JF natetea kwa sababu kuna watu wamepatana JF na mpaka sasa wanaishi kwa amani. Mimi mwenyewe ni mfano wa watu waliopata mchumba JF... I swear sikutegemea kupata msichana wa namana hii popote pale katika maisha ya kawaida but JF imenipatia msichana like an angel vile.

Nina amani sana naye, I believe ana amani sana nami pia! Swala la msingi chunguza njia zako ulizotumia mpaka kutaka kuonana na huyo dada... kama ni mke wa mtu kakufanyia hivyo wewe na huyo mke kuna kasoro ambayo si lazima tupeleke lawama JF...!

Nitaitetea JF mpaka yanikute kama yako ila nahisi vigumu maana nilisha pata nilipohitaji mchumaba na sasa naishi hapa kama uwanja wa nyumbani sijawah tongoza tena na haitatokea... kama kuna mtu kaingia hapa kwa kufanya JF ni uwanja wa Fisi tegemea zaidi ya hayo.

Mshukuru Mungu amekupa warning ya maisha.

MY TAKE:
Jambo analo lala mika mtoa mada lipo na linahitaji umakini sana hasa kwa wale ambao wanakutana hapa ndani na within a week wanakuwa wamefahamiana na kujuana this is too risky.
Haimaanishi watu wasiende MMU au Love Connect but you always have be take risk before you achieve.
Narudia kuwa nimepata msichana ambaye anafanana sana nami kwa mwenendo wake hapa JF... I hope ntampenda daima nilipokuwa natafuta sikutegemea kuwa ntaweza pata such a lady! So hili swala la mtoa maada lisipuuziwe na vilevile lisiwaondolee ujasiri wenye bahati zao kukutana hapa.

Ni vizuri ukimtaja huyo muhusika hapa.

Wachaaaaaa! Wewe Huyo Paxxxxx! Ila ulionja kwanza!!! LOL! Weee Mbayaaaaaaaaaaaaaaaaa! (in Joti's voice) Kwa hiyo saa hivi tambarareeee! LOL! Nisamehee kwa upekupeku ila naomba kuuliza ULIVUTIWA NA NINI KWAKE? Au Comments? LOL! Ngoja nianze kucomment KICHURCH CHURCH, naweza bahatika MBUZI ALIENONA KWENYE GUNIA!!! LOL!
 
Weka ID yake anayotumia humu tupambane naye! Na wewe wanawake hawapatikani humu ipo siku utatongoza jini!
 
dah nimejikuta nacheka peke yangu kumbe watu wanaenda zaid ya kusend pm? Mie mkimbiaj mzur so warning taken mkuu
 
Jamni alichoandika huyu jamaa ni cha kweli mwaka janaa mwezi wa sita dada yangu alitapeliwa na kijana aliyemkuta humu sh milioni mbili bahati nzuri to cut it short jamaa alijitia nafanya kazi tume ya mipango viwanja vinatolewa sister ampe pesa akampa 2m mnajua tena watoto wa kike sasa sisiter kamkamata yule jamaana full contact anazo nshamwabia mara kibao tumtamngaze humu anasema tuvute muda kwanza kozi mambo yapo police nawaambieni kuweni makini humu hasa kina dada
 
mhh! Huyo sister ako naye zimo kwel? Sasa tume ya mipango na viwanja wapi na wapi? Kama ki2 hufaham muwe mnauliza cyo kwenda kichwakichwa
 
ID itasaidia nini na wakati mtu anaweza kubadilisha na kuja na ID mpya pengine hata yumo humu na kuchangia hoja anachangia
 
kwa ufupi inatakiwa kuwa makini na wapenzi wa kwenye mitandao.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom