Matangazo ya dawa za nguvu za kiume"STOP"

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi amepiga marufuku kuweka barabarani matangazo ya biashara ya dawa za kuongeza nguvu za kiume.

Lukuvi amesema kufanya hivyo ni fedheha na kuwataka wanaotangaza biashara hizo, walipie katika mamlaka zinazohusika kama wana uhakika na dawa zao.

“Marufuku yangu itafanikiwa endapo viongozi wa Manispaa watalisimamia hili kwa umakini kwa kuzingatia sheria za mazingira zilizowekwa maana wao ndio wachangiaji wakubwa wa hili kutokana na kutoshiriki kwa umakini katika kuusimamia usafi wa mazingira,” alisema Lukuvi juzi katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa.

Aidha, uongozi wake umepiga marufuku matangazo yote ambayo huchafua mazingira yakiwemo ya vitambaa yanayodaiwa ni ya waganga wa jadi wanaotangaza kazi zao, ambayo hutundikwa pembeni mwa barabara badala yake imewataka wanaotaka kujitangaza kutumia vyombo vya habari.

Lukuvi alisema kitendo cha kutundika matangazo au kubandika mabango yenye kutangaza shughuli au bidhaa ni kukosa ustaarabu na ni uchafuzi wa mazingira.

Katika hatua nyingine, Lukuvi ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho, aliwataka Wakala wa Barabara (Tanroads) kuhakikisha wanafanya ukarabati na matengenezo katika barabara zilizoharibika kwa wakati badala ya kusubiri ziharibike sehemu kubwa ili kupunguza gharama na hasara kwa serikali.

Pia aliitaka Tanroads kuhakikisha inasimamia alama za barabarani na kupaka rangi katika michoro iliyofutika sanjari na kuweka matuta kila sehemu yanapohitajika ili kupunguza ajali zisizo za lazima.

Kwa upande mwingine, wajumbe wa kikao hicho walikubaliana kusimamia upandaji wa miti kando ya barabara inayoendana na hadhi ya barabara husika badala ya kupanda miti ya miarobaini ambayo haivutii katika barabara.
 
hehehehehehe
atahamishwa mkoa maana wapo mabosi wake wanazitumia sana hizo artificial jet.
 
hehehehehehe
atahamishwa mkoa maana wapo mabosi wake wanazitumia sana hizo artificial jet.
Mkuu hajapiga marufuku dawa ila mfumo wa matangazo na kwamba hayo mabango yao wayalipie au watumie vyombo vya habari.
 
angeenda mbali zaidi, angepiga marufuku na yale matangazo ya shule na vyuo vinavyoota kama uyoga.
 
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi amepiga marufuku kuweka barabarani matangazo ya biashara ya dawa za kuongeza nguvu za kiume.

Lukuvi amesema kufanya hivyo ni fedheha na kuwataka wanaotangaza biashara hizo, walipie katika mamlaka zinazohusika kama wana uhakika na dawa zao.

“Marufuku yangu itafanikiwa endapo viongozi wa Manispaa watalisimamia hili kwa umakini kwa kuzingatia sheria za mazingira zilizowekwa maana wao ndio wachangiaji wakubwa wa hili kutokana na kutoshiriki kwa umakini katika kuusimamia usafi wa mazingira,” alisema Lukuvi juzi katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa.

Aidha, uongozi wake umepiga marufuku matangazo yote ambayo huchafua mazingira yakiwemo ya vitambaa yanayodaiwa ni ya waganga wa jadi wanaotangaza kazi zao, ambayo hutundikwa pembeni mwa barabara badala yake imewataka wanaotaka kujitangaza kutumia vyombo vya habari.

Lukuvi alisema kitendo cha kutundika matangazo au kubandika mabango yenye kutangaza shughuli au bidhaa ni kukosa ustaarabu na ni uchafuzi wa mazingira.

Katika hatua nyingine, Lukuvi ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho, aliwataka Wakala wa Barabara (Tanroads) kuhakikisha wanafanya ukarabati na matengenezo katika barabara zilizoharibika kwa wakati badala ya kusubiri ziharibike sehemu kubwa ili kupunguza gharama na hasara kwa serikali.

Pia aliitaka Tanroads kuhakikisha inasimamia alama za barabarani na kupaka rangi katika michoro iliyofutika sanjari na kuweka matuta kila sehemu yanapohitajika ili kupunguza ajali zisizo za lazima.

Kwa upande mwingine, wajumbe wa kikao hicho walikubaliana kusimamia upandaji wa miti kando ya barabara inayoendana na hadhi ya barabara husika badala ya kupanda miti ya miarobaini ambayo haivutii katika barabara.


Inasemekana yeye mwenyewe ni mmoja wa watumiaji wazuri sana wa hizo aphrodisiacs na anapenda sasa totoz. Sasa sijajua kwanini anaziondoa mitaani na ili iweje!. Habari zake zinavuma sana kutokea Dodoma
 
Lukuvi mjanja kweli, yeye ameshajinunulia stock ya kutosha ametunza ndani then anapiga marufuku, sasa wengine tutapata wapi hizo dawa jamani?
 
Hawa wakubwaa wakishapata dawa zinazowatibu wanataka kufaidi wenyewe mbona wabinafsi hivi
 
Whats the problem with these medicines jama, leave people with their jobs na huyo mwenye tatizo naye apate tiba leave them
 
Kuongezeka kwa matangazo hayo kunaashiria wingi wa wateja wa dawa hizo na wala si hayo ya barabarani tu hajawahi kuona kuna kagazeti fulani ka sports kanatoka kila jumapili asilimia karibu 80 ya matangazo yake ni ya dawa za kiume?..,ningefurahi zaidi kama juhudi hizi zingeelekezwa kwenye kujua chanzo cha tatizo la upungufu wa hizo nguvu na kukifanyia kazi kuliko kupambana na matangazo wakati wagonjwa kibao.,au ana deal ya kuingiza hizo dawa sasa anaanza kujihami kwa kupunguza competition kwenye market?..mzee biashara matangazo waache jamaa wasaidie kuokoa ndoa za watu.
 
ningefurahi zaidi kama juhudi hizi zingeelekezwa kwenye kujua chanzo cha tatizo la upungufu wa hizo nguvu na kukifanyia kazi kuliko kupambana na matangazo wakati wagonjwa kibao.
Ushauri mzuri sana huu. Hawa watu wanataka ndoa za watu wengine zimeguke nini?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom