Matajiri wausiwa kudai nchi bora kutokana na ajali ya Anthony Joshua

Matajiri wausiwa kudai nchi bora kutokana na ajali ya Anthony Joshua

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,242
Reaction score
90,300
Haijalishi una utajiri kiasi gani binafsi kama Mnigeria, sote kwa pamoja ni maskini. Maskini sana.

Hili unalielewa tu wakati wa dharura. Moto unazuka lakini hakuna huduma ya zimamoto. Ajali inatokea lakini hakuna huduma ya kwanza, hakuna gari la wagonjwa, hakuna mfumo.

Leo, bingwa wa ndondi wa dunia kama Anthony Joshua alipata ajali ya gari na hata gari moja la wagonjwa halikuonekana. Mtu tajiri kiasi hicho na anayejulikana duniani kote. Watu walikusanyika tu kumzunguka kana kwamba ni tamasha. Hakukuwa na hatua za usalama. Hakukuwa na uokoaji wa kitaalamu. Kulikuwa na vurugu tu.

Ajali hiyo iligharimu maisha ya watu wawili.

Mwezi uliopita, msaidizi wa gavana aliyeko madarakani alichomwa kisu katika tukio la kisiasa. Mtu akabebwa juu ya mabega ya watu! Tukio la kutisha sana. Bado hakuna gari la wagonjwa. Hata kwa msaidizi wa gavana. Huo ndiyo umasikini wa kweli.

Nchini Nigeria, pesa hazikuokoi wakati wa dharura. Ushawishi haukulindi. Wakati inapokuwa muhimu zaidi, kila mtu ni maskini.

Kwa Mnigeria tajiri na mwenye ushawishi anayefikiri kudai nchi bora ni jukumu la maskini tu, siku moja utaelewa. Katika dharura, wewe ni maskini sawa na sisi wengine.

Nigeria ni maskini. Maskini sana.

Pumzika kwa amani kwa waliopoteza maisha, na tunamtakia Anthony Joshua apone haraka.

======
Ameandika The General Snow katika ukurasa wake wa X,

Screenshot_20251230_074719_X.jpg
 
Ukiangalia Ambulance Dar zinavyopambana na foleni wakati mwingine unatamani uwakamate watawala uwachape viboko.
Afrika tumelaaniwa yaani wote tupo hivyo hivyo ,familia ya kizigha na samuya wakikusanya magari yao ya bei mbaya unaweza kujenga barabara (za kuunganisha mitaa/rings roads) nchi nzima na pia kuweka emergency road za Ambulance kama ilivyo kwa mwendo kasi.
 
Ndiyo maana wengine tunajioiga self imposed exile nchi zenye mifumo going on 13 years now hata likizo kurudi Bongo mgogoro.

10 years and counting. My desire huwa ni kurudi bongo lakini issues kama hizi zikitokea zinanikumbusha nipo sehemu salama zaidi. Watu wengi wanapoteza uhai kwa ubovu wa services na si kwamba siku yao imefika. Ndio maana life expectancy ya mwafrika ipo kwenye 60s wakati mzungu anapiga 70+. Quality of life
 
Sikuona ambulance wala gari lingine lolote la uokoaji!

AJ aliishia kupandishwa kwenye gari ya polisi tena siti ya mbele.

Halafu nimeona picha za wale waliopoteza maisha yao.

Mmoja alikuwa hana kichwa. Miili yao iliachwa wazi tu na hakuna hata mmoja kati ya waliokuwepo ambaye alijaribu walau kuifunika hiyo miili.

Sijui AJ ata recover kivipi kutoka kwenye trauma aliyoipata.
 
Naunga mkono hoja,

Unaweza ukawa tajiri na una Gari kali ila utapita kwenye Barabara mbovu,risk ya ajali coz watu wengi hawafuati sheria za barabarani,huduma ya uokoaji wakati wa dharura,

Ndio maana watu wengi wanaoenda abroad sio tu kwamba wanaenda kutafuta maisha bali pia kufuata huduma bora.
 
Ukiangalia Ambulance Dar zinavyopambana na foleni wakati mwingine unatamani uwakamate watawala uwachape viboko.
Kwani bongo sheria za barabarani zinasemaje kuhusu magari ya kubebea wagonjwa?

Huku kwingine watu huwa tunafanya kila aina ya jitihada kuliacha gari hilo lipite endapo limewasha ving’ora vyake.
 
10 years and counting. My desire huwa ni kurudi bongo lakini issues kama hizi zikitokea zinanikumbusha nipo sehemu salama zaidi. Watu wengi wanapoteza uhai kwa ubovu wa services na si kwamba siku yao imefika. Ndio maana life expectancy ya mwafrika ipo kwenye 60s wakati mzungu anapiga 70+. Quality of life
Mimi uzuri wangu nilivyoondoka Tanzania nilijua naondoka kimoja, sikusema naondoka halafu nirudi.

Kurudi labda kuwe na msiba wa karibu sana nimelazimika, au jambo ka dharula kubwa kama hivyo.

Najua nikirudi nitaanza kugombana na watu tangu ubalozini hukuhuku kabla sijagusa Bongo.

Nikifika hapo huo ukiritimba wa airport tu najua nitagombana na watu.

Sasa kuondoa huo ugomvi ndiyo naona bora likizo niende Turks and Caicos tu 😂😂😂
 
10 years and counting. My desire huwa ni kurudi bongo lakini issues kama hizi zikitokea zinanikumbusha nipo sehemu salama zaidi. Watu wengi wanapoteza uhai kwa ubovu wa services na si kwamba siku yao imefika. Ndio maana life expectancy ya mwafrika ipo kwenye 60s wakati mzungu anapiga 70+. Quality of life
Tulidhani diaspora mlioona ulimwengu bora unafanyaje kazi mngerudi kutusaidia kurekebisha hali ya mambo nyumbani, sasa na nyie mnatokomea huko tena!😁
Rudini wakuu mtupe mambinu na mipango mtukwamue kutoka kwenye minyonyoro ya tawala duni.
 
Sikuona ambulance wala gari lingine lolote la uokoaji!

AJ aliishia kupandishwa kwenye gari ya polisi tena siti ya mbele.

Halafu nimeona picha za wale waliopoteza maisha yao.

Mmoja alikuwa hana kichwa. Miili yao iliachwa wazi tu na hakuna hata mmoja kati ya waliokuwepo ambaye alijaribu walau kuifunika hiyo miili.

Sijui AJ ata recover kivipi kutoka kwenye trauma aliyoipata.

Halafu huko Nigeria jamaa wanaokula kamba zao ni ndefu kishenzi.

Ndangote anadai kuna Jamaa mfanyakazi wa shirika la umma anasomesha watoto wake Swiss analipa mamillion ya USD kila mwaka.
 
Sikuona ambulance wala gari lingine lolote la uokoaji!

AJ aliishia kupandishwa kwenye gari ya polisi tena siti ya mbele.

Halafu nimeona picha za wale waliopoteza maisha yao.

Mmoja alikuwa hana kichwa. Miili yao iliachwa wazi tu na hakuna hata mmoja kati ya waliokuwepo ambaye alijaribu walau kuifunika hiyo miili.

Sijui AJ ata recover kivipi kutoka kwenye trauma aliyoipata.
Mimi nilikuwa nasikia neno trauma mara traumatized, siku nilipatwa tukio lakuvamiwa ilinichukua kipindi mpaka hii hali ikatoka kwenye kichwa changu, sasa kwa ajali ya namna hii sijui jamaa itamchukua muda gani kusahau hali hii
 
Back
Top Bottom