umoja wa afrika ukiimarishwa ukawa na nguvu na sauti moja basi umaskini utahamia amerika,ulaya na huko asia, lakini kama afrika ikiendelea kuwa disoganized kama ilivyo sasa basi itaendelea kuwa maskini forever. Inatakiwa tuwapate viongozi makini kama MAGUFULI,GADAFI,TRAORE,LUMUMBA,
Hili wazo la kutaka viongozi makini waje watumalizie matatizo yetu ndio tatizo la Afrika.
Yani hapo wewe ushamtegea kazi ya umakini kiongozi.
Umejitoa katika kazi ya umakini. Unaendeleza fantasy kwamba Gaddafi alikuwa kiongozi mzuri.
Umesoma "Gaddafi's Harem: The Story of a Young Woman and the Abuses of Power in Libya" by Annick Cojean?
Umesoma "The Return: Fathers, Sons and the Land in Between" by Hisham Matar?
Unam romanticize Lumumba?
Umesoma "The Lumumba Plot: The Secret History of the CIA and a Cold War Assassination" by Stuart A. Reid ?
Hao viongozi wote uliowataja wana mapungufu makubwa sana.
Magufuli, Gaddafi, Traore na Lumumba, wote ni populists wenye matatizo mengi sana.
Na bila ya kuwa na wananchi makini wa kuwasimamia hao viongozi, hata viongozi makini wa kweli watachoka na kuishia kuharibu tu.
Moja ya matatizo makubwa ya Afrika ni hii habari ya kutegeana umakini.
Wananchi wanawategea viongozi, viongozi wanawategea wananchi.
Wakubwa wanawategea "Gen-Z", "Gen-Z" wanawategea wanajeshi, wanajeshi wanawategea raia.
Mwishowe watu wanashangaa kwa nini bara lenye rasilimali nyingi bado linagubikwa na umasikini, maradhi na vita?