Mkuu nachokijua miye ni uhalisia. Ukinisoma vizuri utakuta matamshi yangu sii ya Ushabiki bali Uhalisia ambao watu kama nyie hamuwezi kukubaliana nami kwa sababu hamtaki kukubali makosa yenu ila siku zote hutafutwa mchawi..Mzee Mkandara, Tundu Antipas Mughwai Lissu alitamka hivi...."TUMESHAMALIZANA NA ZITTO" Ile ni kauli thabit, kutoka kwa mtu thabit, na kiongozi wa chama thabit. Wanachadema wote kwa ujumla wetu hatuna time na Zitto. Hata wewe unajua mzee wangu
Zitto ni mwiba unyayoni hamuwezi kumsahau kwa sababu alipokaa itakuwa donda ndugu na mtashindwa hata kutembea. nachopingana nanyi toka mwanzo ni maamuzi yenu wenyewe wakati ambao hamkutakiwa kabisa kushiriki ktk siasa za kujimaliza. Mimi najua chanzo cha yote haya na hivyo kama mngekuwa na weredi japo kidogo wa njama zilzosukwa, CDM leo ingekuwa confirmed IKULU wanaingia bila msaada wa Lipumba wala UKAWA.
Lakini kwa sababu hawa unaowaema wapo pale kwa maslahi yao, wengine vibaraka walokuja kwa kazi maalum sitoshangaa ukisema nawe kuwa tumeisha malizana na Zitto kwa sababu swala haikuwa Zitto bali kuahirisha safari ya CDM magogoni.. Na sasa hivi sura halisi za wasaliti zinajitokeza taratibu kwa majigambo na vifua mbele..Wakili ni mtetezi wa watu anaweza tetea hata jambazi, ndivyo sheria inataka..