Sina siasa za mlengo wowote zaidi ya mimi kuwa mwanamabadiliko. Navutiwa na siasa za upinzani ili kuiondoa CCM, tufanye nashawishika na chama kipya ACT WAZALENDO na hususan kiongozi wake ZITTO ZUBERI KABWE.
Ila naomba anijibu au viongozi wenzie wanijibu maswali haya 21 kuhusu Zitto
1.Kwanini kila sehemu ukianzisha mjadala lazima wengine wamuite yeye msaliti?
2.Kwanini anatetewa na kupendwa na wana CCM mitandaoni na mitaani kuliko wanamabadiliko?
3.Kwanini vyombo vya habari na mitandao isiyo penda vyama vya upinzani kama Clouds Fm,Jambo
leo,uhuru,mzalendo,na jamii forum vinampa upendeleo sana.?
4.Kwanini wakati alipokuwa chadema alikuwa apigi ziara kama sasa ACT, kutafuta wanachama hadi kwenye malori na barabarani....?
5.Nijuavyo mimi ACT hawapati ruzuku yoyote kama vyama vingine vya siasa ambavyo vinauwakilishi je Zitto amepata wapi pesa ya kujaza magari 15 mafuta kila siku.kulipa posho watu 31 kwenye msafara wake,kulipa waandishi wahabari 9 kwenye msafara wake,kulipia P.A.system na music kwenye mikutano yake.kulipia vyumba(guest haouse wa msafara wote huo leo siku ya 8,wakati kwenye akaunti alikuwa ana millioni 18 tuh?
5.Millioni 150 za mkutano mkuu pale diamond jubilee na mabasi matano kutoka kigoma na mwanza,na zile costa 15.kwa muda wasiku 4.kusambazia wajumbe wake Dar es salaam alizitoa wapi na hawana ruzuku? Ikiwa tangu ahamie alikuwa ana siku 4
6.Kwanini huko anakopita kwenye mikutano yake hawaisemi vibaya serikali ya ccm?
7.Kwanini huko kwenye mikutano wanayofanya waongeaji ni wengi ila anasikika yeye tuh?
8.Kwanini mauzo ya kadi za ACT WAZALENDO, yanamwitikio hafifu na yeye anajua hilo.badala chama kikae sehemu moja hata siku tatu kusimika uongozi badala yake anapita kama mbio za mwenge tuh?
9.Kwanini mikutano yake yote anaruhusu viongozi wake na wapambe kama afande sele kuitukana chadema.ila yeye haitukani chadema?
10.Kwanini pia hao wabunge 50 anaosema wanakuja ACT.kwamba wanaohofia kukosa mafao yao.asiwafundishe njia haliyo tumia yeye kujiuzulu na bado mafao anapata.ili nao wajiuzulu muda huu ila mafao wapewe kama yeye Zitto.
11.Kwanini wale wabunge ambao siku nyingi wanatuhumiwa kwa usaliti na kuvujisha siri za chama chao kama LETICIA NYERERE,(rejea gazeti Tazama Tanzania). ndiyo wanaotajwa kuja ACT Na siyo wabunge kama JOHN MNYIKA AU VICENT NYERERE
12.Wakina mchange na mtemelwa walio kuwa wanadai kwenye television mbalimbali kuwa wao bado ni chadema hata kama chadema imewafukuza kwa nini sasa hivi wamepewa ujumbe kamati kuu na hatujawaona kupewa kadi hadharani?
13.Kwanini unajiita mjamaa wakati kwenye mali zako ulizohorodhesha unamiliki kitalu cha gesi?
14.Unaurafiki gani na Ramadhani Dau?
15.Ulipo kuwa mwenyekiti Pac na Ramadhani Dau angali yupo NSSF.mahusiano yenu hayakuhathiri utendaji wako.hata kupata nyumba za NSSF na tenda za kutangaza NSSF?
16.Kwanini uliposhindana na cheyo uenyekiti wa PAC wabunge wa CCM walipewa agizo na mwenyekiti (KIKWETE) Kupitia waziri mkuu pinda wakupigie wewe badala ya cheyo?
17.Kwanini kikwete alipoenda SUDANI KUSINI kwenye sherehe za uhuru aliambatana na wewe na familia yake.akiacha viongozi wenzie wa CCM.?
18.Watanzania amu kuwa aliyepambana na escrow mpaka akitwa tumbili na kutishiwa kuuwa ni KAFULILA na si wewe,lakini wewe unawaaminisha watu kuwa escrow ndiyo uliyeibua na kuipigania?
19.Unazungumziaje mahusiano yako na viongozi wa CCM na serikali kama mwigulu nchemba,LUDOVICK UTTOH?
20.vipikuhusu sakata lako la kutaka kuacha siasa ili urudi chuo au ende kuajiriwa TPDC umeshaghairi?
21.Kwanini Tangu uanze harakati zako za siasa za upinzani ujawahi kunyimwa kibali cha mkutano wala
kufanyiwa vurugugu na ccm au kupata mshimshike wa kukamatwa na kuwekwa ndani kama wapinzani wengine akina lipumba,mbowe,slaa, lisu,lema,au mnyika.?
Tafadhali naomba nijibiwe maswali, nampenda sana Zitto ila kila ninapomuongelea nakutana nayo nashindwa kujibu.
Hayo maswali , nampenda sana Zitto ila kila ninapo muongelea nakutana nayo nashindwa kujibu.