Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Joined
Apr 20, 2013
Posts
15
Reaction score
424
WanaJF

Nilikuwa mmojawapo wa viongozi tulioandamana na Mhe Rais katika ziara yake ya majuzi nchini Singapore. Ninawaletea sehemu ya Master Plan ya mji wao mpya unaojengwa kutokana na kuokoa ardhi baharini (reclamation). Unaona kila kipande cha ardhi mpya kimeshapangiwa matumizi yake na kuwekewa malengo ya majengo yanayotakiwa.

Kupanga ni kuchagua. Kunahitaji nidhamu na hakuna mchezo wala utani. Huwezi kuwa na mji uliopangwa kama unapenda na kuendekeza uholela na vurugu (chaos). Kinachotakiwa ni kushirikisha wadau wote kupanga malengo na viwango baada ya kupata maoni ya wataalam. Wanaoarithirika na kulazimisha kuhama kupisha maendelezo mapya wanalipw fidia stahiki na endelevu.

Anayedai vinginevyo si msema kweli. WaSingapore wamehaidi kutusaidia katika ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni. Ninakaribisha maoni yenu hasa nyie mlio nje na mnaishi katika miji iliyopangwa? Je uholela unavumiliwa au kuendekezwa? Tupe habari.

Singapore.JPG

Mama Tibaijuka
 
kamchina kangu kamegoma kufungua hyo picha,ila sasa lengo la kuja na master plan ya huo mji ni nini muheshimiwa au nasi tuna mpango wakujenga kitu kama hcho?

na kwan uje na master plan ambyo ardhi yake imetokana na reclamation wakati sisi bado tuna hadhina kubwa ya Ardhi?

Binafsi cdhan kama ina tija wala kama inatufaa.
 
Lakini mh. Kwanini mumeshindwa kuboresha huu mji tulionao sasa hivi na munaanza kutafuta mpya wakati bado hamjachelewa? Tunahitaji tuone mabadiliko hapa tulipo sasa, Hizi sheria ndogondogo za miji zinafanya kazi?

Mtu kuweka maeneo ya mjini vibanda, parking ziko ndani ya barabara ukipita maeneo yote ya mjini sehemu za kupita watu na magari zimepakiwa gari na barabara inakua finyu. Majumba mjini yamekua kama magovu je hakuna sheria ya kuwaagiza wamiliki kuyarekebisha kila kipindi inapofika?
 
tatizo kila siku zinakuja master plans ila utekelezaji ndo hamnaaaa
 
Mbona mlishafanya huo mpango angalia hapa kwenye link (Kigamboni New City) au mnataka kupiga hela nyingine za ili mtutengenezee video nyingine?

Mkuu Mohamed Hussein asante sana kwa hiyo link iko wazi kabisa,hawa ndio mawaziri wetu hawajui kuna kitu gani kiliwahi kufanyika katika wizara zao hiyo link inajieleza.. hapo wanataka kuandaa master plan upya ili wapige 10%, mimi nasikitika sana kuwa tuna wasomi ambao hawajaelimika na wasio na uzalendo!!
 
Mimi mawazo na maoni yangu ni

1. Endelezeni huo mji wa Dar es Salaam kwanza uwe wa kisasa kwani unatia aibu hasa mvua ikinyesha.

2. Tumieni huo msaada kuendeleza miji mingine mipya kwani kigammboni tayari mna kila kitu in place.

Mengine naona ni siasa na ufujaji wa pesa tu hapo tutakuwa na mi masterplan kibao kwenye makabati.
 
Profesa shida ya nchi yetu ni kutokutii sheria zilizopo na kutojali mipango tuliyojiwekea. Inasikitisha kuona miji mingi nchini ikikua kwa kasi-holela...kila mtu anajenga anavyotaka na hakuna mamlaka inayojishughulisha kuzuia hali hiyo.

Kama ulivyosema kupanga ni kuchagua. Nyie mliopewa nafasi ya kusimamia miji yetu ndiyo mnapaswa kuhakikisha sheria zilizopo zinafuatwa na kila raia. Pia wizara yako na halmashauri au manispaa zijitahidi kupima, kuuza na kusimamia uuzaji ardhi hasa za mijini kwa wananchi kuliko kuachia kila mtu auze kiholela hali inayopelekea ujenzi holela kuendelea kuwa tatizo kwenye miji yetu.
 
69177_157820217583469_4081295_n.jpg
na hii ndio plani ya miji ya Tanzania, sasa mama kwa nini angalau usiunde vikosi jamii kwenye kila kata kama mfano inavyoanzishwa vikundi vya polisi jamii vitavyohakikisha kuwa kila kiwanja kina access the barabara na kuweka kipimo cha chini cha kiwanja. hamuwezi kukaa mnajivunia miji ya wenzenu huku yakwetu inazidi kuhabirika
 
Tangu miaka ya tisini Chuo kikuu cha ardhi kimekuwa kikizalisha wataalamu wengi wa mipango miji na ma arctect wengii, achilia mbali mainjinia wanaograduate vyuo mbalimbali duniani, resource hizi hazitumiwi ipasavyo kwa sababu za SIASA imeshaharibu kilakitu tanzania.

Tanzania tumezoea makazi ya watu yanatangulia kabla ya plan, makazi then mipango inafuata nyuma, badala ya kuanza kutengeneza mipango kabla ya makazi ya watu.
 
Mama Tibaijuka, tukubali kwamba tulikosea sana huko nyuma, ni miaka mingi mno wananchi wamekuwa wakienda kuvamia maeneo yasiyopimwa na kuweka makazi yao ya kudumu sababu serikali imekuwa haiweki kipaombele upimaji wa ardhi.

Jiji lote la Dar es salaam lipo shaghala balaga; wananchi tunahaha kutafuta viwanja bila mafanikio; kiwanja kilichopimwa cha sq 600 kinafikia hadi 30million. Hili nalo unaliongeleaje Mh waziri ?

Kuhusu kigamboni mimi nina heka zangu 2 kibada na nimeziendeleza, nimeshajiorodhesha kwamba nataka kuwa part of that project sababu najua thamani ya ardhi. mpango uje lakini wananchi wapate stahiki zao bila dhuruma wale ambao watapenda kuyauza maeneo yao.
 
Profesa shida ya nchi yetu ni kutokutii sheria zilizopo na kutojali mipango tuliyojiwekea. Inasikitisha kuona miji mingi nchini ikikua kwa kasi-holela...kila mtu anajenga anavyotaka na hakuna mamlaka inayojishughulisha kuzuia hali hiyo.

Kama ulivyosema kupanga ni kuchagua. Nyie mliopewa nafasi ya kusimamia miji yetu ndiyo mnapaswa kuhakikisha sheria zilizopo zinafuatwa na kila raia. Pia wizara yako na halmashauri au manispaa zijitahidi kupima, kuuza na kusimamia uuzaji ardhi hasa za mijini kwa wananchi kuliko kuachia kila mtu auze kiholela hali inayopelekea ujenzi holela kuendelea kuwa tatizo kwenye miji yetu.

Tatizo hapa liko pande zote mkuu i.e raia kutotii sheria na pia hao viongozi kushindwa kusimamia sheria kwa haki na ueledi wa mambo(wanasimamia sheria pasi na ujuvi wa mambo wala kutenda haki)...viongozi wetu wengi si wataaluma wa mambo ni siasa na abrakadabrah nyingi kwenye mambo ya msingi.

Viongozi na wasomi wengi wametuangusha sana kwenye utendaji kazi na kulisababishia taifa hasara na aibu kubwa...pia ni waoga sana kufanya maamuzi magumu lakni yenye tija kwa taifa....hapa nam_exclude mzee Lowassa yeye kwa hili anaweza.
 
Mh.Mbona wakati unafungua mpango wa ujenzi wa mji wa Kigamboni mulitoonyesha master-Plan au sasa tueleweje bado ni ile ile au munabadili ,halafu mulituambia fedha zipo na tayari wajenzi wamepatikana munangoja wananchi waridhie tu ,Kwanza mulisema itakuwa mamlaka kamili halafu mukabadiri na kusema itakuwa chini ya Temeke ,Mh.tunaomba tuelezwe ukweli huu mpango ni mzuri lakini je mumefikiria kuboresha the old Dar es salaam,kutengeneza sewerage system ya milele kama ilivyo kwenye miji kama ya Londoni,Newyork nakadharika,kununua maeneo Fulani kama wanavyofanya Adis-ababa sasa hivi ili kutokomeza slums , kila la heri
 
Heshima kwako mama Anna Tibaijuka,

Tafadhali japa kazi na tuonyesha mfano kwa kufanya development ya Kigamboni modern city, tunakutegemea.

All the best mamaaa..
TzPride
 
Mimi nashauri Mjenge makao makuu ya Tanzania inakuwaje nchi haina mji mkuu Mnazidi kujibana Dar??Jengeni Dodoma fumueni miundo mbinu ya CDA anzisheni miundombinu mipya!!Kigamboni nisawa kwa swala la ustawi wa nchi lakini kwa heshima ya nchi Makao makuu yanahitaji kujengwa pia!!
 
@ kakakiiza hivi unadhani Dodoma ni makao makuu ya nchi?
Dodoma ni makao makuu ya CCM, hivi unadhani chama kingine kikichukua nchi Dodoma itaendelea kuwa makao makuu?
Mimi nashauri Mjenge makao makuu ya Tanzania inakuwaje nchi haina mji mkuu Mnazidi kujibana Dar??Jengeni Dodoma fumueni miundo mbinu ya CDA anzisheni miundombinu mipya!!Kigamboni nisawa kawa swala la ustawi wa nchi lakini kwa heshima ya nchi Makao makuu yanahitaji kujengwa pia!!
 
1:Muheshimiwa Prof Anna Tibaijuka vipi kuhusu lile ghorofa la kariakoo uliloahidi kuwa litavunjwa kutokana na kutokukidhi vigezo, mbona kimya kimetanda na jengo bado lipo tu?

2: Serikali inamipango gani makini juu ya upangaji miji kwenye mikoa mingine tofauti na Dar ambayo imeanza kuonyesha dalili za kupanuka kwa haraka kutokana na ongezeko la watu au kutokana na kuongezeka kwa vivutio vya kiuchumi ili kuepuka hapo baadae mikoa hiyo isijekuwa na poor planning kama Dar es salaam?


 
kakakiiza hivi unadhani Dodoma ni makao makuu ya nchi?
Dodoma ni makao makuu ya CCM, hivi unadhani chama kingine kikichukua nchi Dodoma itaendelea kuwa makao makuu?
Daha napata wakati mgumu kukujibu kwani hata mimi sijui hatima ya hii kitu kinaitwa makao makuu ya Nchii inamaana kikija chama kingine kinaweza kikaamua makao makuu yawe LINDI!
 
Back
Top Bottom