The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 305
Nilipozuru Mwanza nilivutiwa sana na Beach zake safi na zenye mandhari nzuri kama pale Tunza Beach, Nyegezi pale SAUTI na nyingine nzuri tuu,
Lakini zaidi ya hapo lile jiji lina Kisiwa maarufu kwa jina la Saa nane, kipo ndani ya Ziwa Victoria, nikisiwa ambacho kama kingeendelezwa kingekuwa chanzo kizuri cha mapato kwa jiji lile, lakini ni wazi kimesahauliwa kama si kutekelezwa.
Lau kingeboreshwa kingevutia wageni na wenyeji wengi kwenda kupunzika pale siku za mapunziko, au hata wenzetu wanaoingia kwenye pingu za maisha kila siku pangekuwa sehemu bora kwao kufanyia fungate zao pale.
Je nikweli serikali haioni umuhimu wa kile kisiwa au kinatekelezwa kimakusudi mwisho wa siku wapewe wakoloni kama walivyopewa migodi?
Lakini zaidi ya hapo lile jiji lina Kisiwa maarufu kwa jina la Saa nane, kipo ndani ya Ziwa Victoria, nikisiwa ambacho kama kingeendelezwa kingekuwa chanzo kizuri cha mapato kwa jiji lile, lakini ni wazi kimesahauliwa kama si kutekelezwa.
Lau kingeboreshwa kingevutia wageni na wenyeji wengi kwenda kupunzika pale siku za mapunziko, au hata wenzetu wanaoingia kwenye pingu za maisha kila siku pangekuwa sehemu bora kwao kufanyia fungate zao pale.
Je nikweli serikali haioni umuhimu wa kile kisiwa au kinatekelezwa kimakusudi mwisho wa siku wapewe wakoloni kama walivyopewa migodi?