Maskini Kisiwa cha Saanane

The Hunter

JF-Expert Member
Dec 25, 2010
1,049
305
Nilipozuru Mwanza nilivutiwa sana na Beach zake safi na zenye mandhari nzuri kama pale Tunza Beach, Nyegezi pale SAUTI na nyingine nzuri tuu,
Lakini zaidi ya hapo lile jiji lina Kisiwa maarufu kwa jina la Saa nane, kipo ndani ya Ziwa Victoria, nikisiwa ambacho kama kingeendelezwa kingekuwa chanzo kizuri cha mapato kwa jiji lile, lakini ni wazi kimesahauliwa kama si kutekelezwa.
Lau kingeboreshwa kingevutia wageni na wenyeji wengi kwenda kupunzika pale siku za mapunziko, au hata wenzetu wanaoingia kwenye pingu za maisha kila siku pangekuwa sehemu bora kwao kufanyia fungate zao pale.
Je nikweli serikali haioni umuhimu wa kile kisiwa au kinatekelezwa kimakusudi mwisho wa siku wapewe wakoloni kama walivyopewa migodi?
 
ofcourse, kisiwa hicho kilikua kizuri sana. Nilikwenda mwaka 1998,kulikua kuna simba mmoja mzee sana, na mandhari mazuri sana,kwa sasa sijui palivyo kwani ni miaka mingi imepita. Ndugu yangu hakuna kingine tatizo ni ufisadi tu.
 
kwanini wasikikabidhi kwa wawekezaji wazalendo? pajengwe mgahawa mzuri na iwe na camp kama pale Tunza beach?
 
Hiki kisiwa sasa kipo chini ya TANAPA, yaani kimegeuzwa national park- so bila shaka umuhimu wa kuwa kivutio cha utalii umeshaonekana. Sijui mtoa mada unaongelea kwenda huko lini ?
 
lakini serikali yetu hainiridhishi namna inavyotenda katika kila sekta. ila hilo la utalii kisiwani saa 8 inabidi wadau waketi chini waweke mikakati. saa nyingine kukaa tu kwenye vijiwe vya kahawa na kulaumu serikali hakusaidii. tunapaswa ku-act na kisha ku-seek government support. nafikiri kwa mwendo huo tunaweza kufufua mengi tu yaliyolala. ata hao wawekezaaji nao huichombeza kwanza seirikali ndio wanapatiwa wanachotaka
 
I guess, this is what separate Tanzanians from the rest. As a responsible citizens, why do you wait for you government to step in? You have local leaders. You have private sector. But you still think that the government is responsible for babyseating a lion in the zoo.
 
Again, sijui mtoa mada hii alienda lini huko. Mikakati ipo na pia kuna opportunities ya yeye kutoa mawazo zaidi. Ingawa ni nadra sana kwa ntu kama mm kuifagilia serikali, kwa hili nadhani imechukua hatua nzuri maana bila ku-upgrade kisiwa hicho ktk status hiyo na NP, haitakuwa rahisi kufanya hayo mdau mtoa mada anayoyaongelea...
 
I guess, this is what separate Tanzanians from the rest. As a responsible citizens, why do you wait for you government to step in? You have local leaders. You have private sector. But you still think that the government is responsible for babyseating a lion in the zoo.

Mzuvendi,

Do you know the meaning of Leadership? Is to lead, aspire people and guide them in a proper and desired destinations. How can we be inspired to got to Saa Nane Island if our own leaders cherish and aspire to have their holidays outside the country? Now and then they are on the planes to go to New York, Brussels, London to mention but few.

No Leader has shown by action the desire to spend his time/his holidays in promoting local tourism . Of course, i am always inspired by my leaders to go to New York, Brussels, London as well...!
 
Dhiki imetujaa mpaka twasahau kuendeleza baadhi ya mambo kama haya.
Maana kama huna dawa maji umeme etc utawaza mambo kama haya ya utalii.
Ni mda mwafaka sasa kufikilia izi kama njia za kukuza mapato ambayo yatasaidia kununua dawa kuweka umeme vijijini kutandaza maji safi na salama
 
ofcourse, kisiwa hicho kilikua kizuri sana. Nilikwenda mwaka 1998,kulikua kuna simba mmoja mzee sana, na mandhari mazuri sana,kwa sasa sijui palivyo kwani ni miaka mingi imepita. Ndugu yangu hakuna kingine tatizo ni ufisadi tu.
Umenena,shida kubwa ni Ufisadi lkn ktk enzi hii ya Magufuli kitakumbukwa tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom