Maskini dada wa watu ananipenda kimya kimya

Maskini dada wa watu ananipenda kimya kimya

DALA

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
2,259
Reaction score
4,691
Heshima mbele wanajamvi,

Kwa uzoefu wangu nimewahi kutongozwa na wanawake kama sijakosea wanne tofauti, wenyewe wanajuwa matokeo yake. Mwaka mmoja uliopita nilikwenda kurekebisha miwani yangu hapa mjini. Kwenye ile ofisi kuna mdada mzuri sana na mchangamfu tukawa tunapiga story wakati mafundi wao wananitengenezea miwani.

Nilishangaa aliponiuliza eti hivi si unapata shida na wanawake sana? Kwa urefu na muonekano wako hawakusumbui kukutaka kimapenzi? Mhhh nilishindwa kumpa jibu la moja kwa moja nikazuga tukapita hiyo topic kwani sikuelewa tafsiri halisi ya swali lake kwa upande wake.

Wiki iliyopita nilienda barbershop ninaponyoa siku zote yapata miaka miwili na nusu sasa kijitonyama alafu kila wiki lazima niende nikiwa hapa town maana mm nanyoa upara tu. Sasa wakati mhudumu ananifanyia scrab akaanzisha story japo mimi sijawahi kuwa nao free kivile maana nimewahi kusikia mikakati yao.

Kwenye maongezi akaniambia eti "dah! Kuna dada yupo kwenye fremu ya jirani yetu wanauza nguo yaani anakupenda hatari, kila akiliona gari lako utamsikia anasema 'mpenzi' wangu kaja" nilishangaa sana japo alijaribu kunielezea huyo dada alivyo ila sijawahi kumuona nikaipotezea.

Maskini wa watu kumbe kina dada nao wanaweza kupenda kimya kimya kama sisi wanaume.
 
Unamanisha nn sasa post kama hii kutuma mwaume lijali mmmmm:-(
 
----- kweli uyu. we utupiwi wazungu kweli?
 
Jf bhana, nimetoa experience na mtazamo wangu watu povu zinawatokaaaaa!

Badala ya kuwa objective mnaniseeeeeema haya wakuu nimewaelewa!
 
Watoto wa kiume hawajifichagi ,wenzako wanajisifia hela
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom