Hata kampuni moja ya ndege iliyokuwa inakwenda Chato, mara moja kwa wiki, sasa imesimamisha safari zake.
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Sarah Reuben akijibu swali la Mwananchi “kwa nini safari za Chato zimefutwa,” anasema “hazijafutwa” isipokuwa kuna mabadiliko katika mpangilio wa safari kwenye viwanja kadhaa.
“Kutokana na baadhi ya ndege zetu kupaki (kuwa katika matengenezo), tumepunguza safari katika baadhi ya viwanja (njia) na sio kwamba tumesitisha,” anasema Reuben alipoulizwa na Mwananchi Juni 21.
Anafafanua kuwa hatua hiyo inatokana na mahitaji ambapo baadhi ya viwanja vimeongezewa safari.
Kwa mujibu wa tovuti ya ATCL, kwenye ukurasa wa kununua tiketi, hakuna ndege kwa abiria wanaosafiri kutoka au kwenda Chato hadi Agosti 3, 2023.
Wakati ATCL inaanza kutua katika uwanja huo, Januari 2021 ilikuwa inafanya safari tatu kwa wiki yaani Jumatatu, Alhamisi na Jumamosi.
Lakini sasa safari zimebaki mbili (Alhamis na Jumamosi) ambazo nazo kiuhalisia hazipo kwani katika tovuti ya shirika hilo ukitaka kununua tiketi kwa ajili ya safari za kutoka au kuelekea Chato unaambiwa hakuna nafasi au hakuna ndege.
Hii ina maana kwamba ndoto za Rais John Pombe Magufuli mwasisi wa wazo na mipango ya kujenga uwanja wa ndege wa Chato kama bado zipo basi zimetatizwa. Dk Magufuli aliingia madarakani Novemba 5, 2015 na miezi tisa tu baadaye, Agosti 31, 2016, Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) ilisaini mkataba na Kampuni ya Mayanga Contractors Co. Ltd kujenga uwanja huo unaotajwa kuwa ni wa tatu kwa ukubwa baada ya wa Juliua Nyerere na (JNIA) na wa Kilimanjaro (KIA).
Katika bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ya mwaka wa fedha 2023/2024, zimetengwa Sh1 bilioni kwa ajili ya kuendeleza uwanja huo.
Kabla ya bajeti kulikuwa na tetesi miongoni mwa wafuatiliaji wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, kuwa wizara ingekuja na bajeti maalumu ya kukamilisha moja kwa moja uwanja huo wa ndege ambao mpaka hapo ulipofikia unakadiriwa kugharimu zaidi ya Sh 50 bilioni.
Akiwasilisha bajeti hiyo bungeni, Mei 22, 2023, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria na mnara wa kuongozea ndege.
Hayo yanajiri wakati Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Geita, Japherson Nnko anasema kukamilisha awamu zote za ujenzi wa uwanja kutategemea uwezo wa Serikali kifedha na umuhimu wa kugharimia mradi husika.
Nnko alikuwa akihojiwa na Mwananchi, miezi mitatu iliyopita aliposema ujenzi wa uwanja wa Chato ni endelevu na kwamba “mchakato unaoendelea sasa ni ujenzi wa uzio ambao ni muhimu kwani ndiyo unavutia kampuni za ndege kuja kwa kuwa wanakuwa na uhakika wa usalama,” anasema Nnko.
Mtumishi mwandamizi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini anasema, kuna “umuhimu mdogo” wa kuendelea kuwekeza katika uwanja huo. “Baada ya ujenzi wa uzio itakuwa imetosha. Uwanja wenyewe hautumiwi ilivyotakiwa na hata safari za ATCL hivi sasa zimesimamishwa. Hakuna haja ya kuendelea kufanya uwekezaji pale,” amesema.
Mtumishi huyu asiye na matumaini anahoji, “Uwanja ujengewe jengo la abiria? Kwa ndege zipi? Ngapi? Hili jengo la watu mashuhuri lililopo ambalo sasa linatumiwa na watu wote ni kubwa kuliko mahitaji ya sasa. Jingine la nini?” Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), anayehusika na usimamizi wa viwanja vya mikoa, Hamis Amiri aliliambia gazeti hili Februari mwaka huu, kuwa mamlaka yake haina mpango wa hivi karibuni wa kuuongezea uwezo zaidi uwanja wa ndege wa Chato.
Amesema hiyo ni kutokana na a uwezo wake wa sasa ni mkubwa kuliko huduma inayotolewa. “Wakati huo uwanja ulikuwa unatumiwa na shirika moja tu la ATCL kwa safari zilizoko kwenye ratiba na rubani aliongozwa kwa msaada kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza uliopo kilomita 235 kutoka Chato. Ndege kubwa kama Dreamliner (Boeing 787-8, zenye kubeba abiria 248 zinaweza kutua hapa.
Takwimu za TAA zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miezi sita (kuanzia Julai 2022 hadi Desemba 2022), idadi ya ndege zilizotua na kupaa katika uwanja huo zilikuwa 112 zikiwa na abiria 2,111. Pia hakuna mzigo wowote uliosafirishwa kupitia uwanja huo katika kipindi hicho. Mzigo ni kifurushi chochote kinachoanzia uzito wa gramu 500 ambacho husafirishwa kibiashara katika eneo la mizigo (sio sehemu ya uzito ambao abiria anapewa kwenye tiketi yake).
Mmoja wa maofisa wa uwanja wa Chato aliyekutwa uwanjani Februari 2, 2023 aliiambia Mwananchi kuwa tangu kuanza kutumika kwa uwanja huo Januari 9, 2021, ni ATCL pekee inaoutumia na idadi ya nafasi zilizotengwa kwa abiria zilikuwa 30.
Amesema mara ya mwisho uwanja huo kuhudumia ndege nyingi ni wakati wa msiba wa Rais John Magufuli. “Siku moja kabla na siku ya mazishi tulipokea ndege kubwa zaidi ya 20 na ndogo zilizokuwa zimebeba waombolezaji. Kuna muda ndege nane zilikuwa zinaegesha kwa wakati mmoja,” alisema ofisa huyo.
“Watu waelewe kwamba Uwanja wa Chato tunautumia kama mmbadala uwanja wa Mwanza ukipata shida. Chato kuna ndege zinatua kupitia Mwanza kuna ndege ya Air Tanzania inatua Chato kupitia Mwanza,” amesema.
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Sarah Reuben akijibu swali la Mwananchi “kwa nini safari za Chato zimefutwa,” anasema “hazijafutwa” isipokuwa kuna mabadiliko katika mpangilio wa safari kwenye viwanja kadhaa.
“Kutokana na baadhi ya ndege zetu kupaki (kuwa katika matengenezo), tumepunguza safari katika baadhi ya viwanja (njia) na sio kwamba tumesitisha,” anasema Reuben alipoulizwa na Mwananchi Juni 21.
Anafafanua kuwa hatua hiyo inatokana na mahitaji ambapo baadhi ya viwanja vimeongezewa safari.
Kwa mujibu wa tovuti ya ATCL, kwenye ukurasa wa kununua tiketi, hakuna ndege kwa abiria wanaosafiri kutoka au kwenda Chato hadi Agosti 3, 2023.
Wakati ATCL inaanza kutua katika uwanja huo, Januari 2021 ilikuwa inafanya safari tatu kwa wiki yaani Jumatatu, Alhamisi na Jumamosi.
Lakini sasa safari zimebaki mbili (Alhamis na Jumamosi) ambazo nazo kiuhalisia hazipo kwani katika tovuti ya shirika hilo ukitaka kununua tiketi kwa ajili ya safari za kutoka au kuelekea Chato unaambiwa hakuna nafasi au hakuna ndege.
Hii ina maana kwamba ndoto za Rais John Pombe Magufuli mwasisi wa wazo na mipango ya kujenga uwanja wa ndege wa Chato kama bado zipo basi zimetatizwa. Dk Magufuli aliingia madarakani Novemba 5, 2015 na miezi tisa tu baadaye, Agosti 31, 2016, Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) ilisaini mkataba na Kampuni ya Mayanga Contractors Co. Ltd kujenga uwanja huo unaotajwa kuwa ni wa tatu kwa ukubwa baada ya wa Juliua Nyerere na (JNIA) na wa Kilimanjaro (KIA).
Katika bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ya mwaka wa fedha 2023/2024, zimetengwa Sh1 bilioni kwa ajili ya kuendeleza uwanja huo.
Kabla ya bajeti kulikuwa na tetesi miongoni mwa wafuatiliaji wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, kuwa wizara ingekuja na bajeti maalumu ya kukamilisha moja kwa moja uwanja huo wa ndege ambao mpaka hapo ulipofikia unakadiriwa kugharimu zaidi ya Sh 50 bilioni.
Akiwasilisha bajeti hiyo bungeni, Mei 22, 2023, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria na mnara wa kuongozea ndege.
Hayo yanajiri wakati Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Geita, Japherson Nnko anasema kukamilisha awamu zote za ujenzi wa uwanja kutategemea uwezo wa Serikali kifedha na umuhimu wa kugharimia mradi husika.
Nnko alikuwa akihojiwa na Mwananchi, miezi mitatu iliyopita aliposema ujenzi wa uwanja wa Chato ni endelevu na kwamba “mchakato unaoendelea sasa ni ujenzi wa uzio ambao ni muhimu kwani ndiyo unavutia kampuni za ndege kuja kwa kuwa wanakuwa na uhakika wa usalama,” anasema Nnko.
Mtumishi mwandamizi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini anasema, kuna “umuhimu mdogo” wa kuendelea kuwekeza katika uwanja huo. “Baada ya ujenzi wa uzio itakuwa imetosha. Uwanja wenyewe hautumiwi ilivyotakiwa na hata safari za ATCL hivi sasa zimesimamishwa. Hakuna haja ya kuendelea kufanya uwekezaji pale,” amesema.
Mtumishi huyu asiye na matumaini anahoji, “Uwanja ujengewe jengo la abiria? Kwa ndege zipi? Ngapi? Hili jengo la watu mashuhuri lililopo ambalo sasa linatumiwa na watu wote ni kubwa kuliko mahitaji ya sasa. Jingine la nini?” Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), anayehusika na usimamizi wa viwanja vya mikoa, Hamis Amiri aliliambia gazeti hili Februari mwaka huu, kuwa mamlaka yake haina mpango wa hivi karibuni wa kuuongezea uwezo zaidi uwanja wa ndege wa Chato.
Amesema hiyo ni kutokana na a uwezo wake wa sasa ni mkubwa kuliko huduma inayotolewa. “Wakati huo uwanja ulikuwa unatumiwa na shirika moja tu la ATCL kwa safari zilizoko kwenye ratiba na rubani aliongozwa kwa msaada kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza uliopo kilomita 235 kutoka Chato. Ndege kubwa kama Dreamliner (Boeing 787-8, zenye kubeba abiria 248 zinaweza kutua hapa.
Takwimu za TAA zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miezi sita (kuanzia Julai 2022 hadi Desemba 2022), idadi ya ndege zilizotua na kupaa katika uwanja huo zilikuwa 112 zikiwa na abiria 2,111. Pia hakuna mzigo wowote uliosafirishwa kupitia uwanja huo katika kipindi hicho. Mzigo ni kifurushi chochote kinachoanzia uzito wa gramu 500 ambacho husafirishwa kibiashara katika eneo la mizigo (sio sehemu ya uzito ambao abiria anapewa kwenye tiketi yake).
Mmoja wa maofisa wa uwanja wa Chato aliyekutwa uwanjani Februari 2, 2023 aliiambia Mwananchi kuwa tangu kuanza kutumika kwa uwanja huo Januari 9, 2021, ni ATCL pekee inaoutumia na idadi ya nafasi zilizotengwa kwa abiria zilikuwa 30.
Amesema mara ya mwisho uwanja huo kuhudumia ndege nyingi ni wakati wa msiba wa Rais John Magufuli. “Siku moja kabla na siku ya mazishi tulipokea ndege kubwa zaidi ya 20 na ndogo zilizokuwa zimebeba waombolezaji. Kuna muda ndege nane zilikuwa zinaegesha kwa wakati mmoja,” alisema ofisa huyo.
“Watu waelewe kwamba Uwanja wa Chato tunautumia kama mmbadala uwanja wa Mwanza ukipata shida. Chato kuna ndege zinatua kupitia Mwanza kuna ndege ya Air Tanzania inatua Chato kupitia Mwanza,” amesema.