Akademician
Senior Member
- May 20, 2015
- 143
- 36
Habari zenu wakuu.
Pamoja na kuhamasika na kazi za waandishi mbalimbali kama vile Kezilahabi, Shaaban Robert, Mohamed Said, Andanenga, Penina Mhando, Haji Gora, Charles Mloka, Theobald Mvungi n.k,
Mimi ni kijana niliyebahatika kuwa na kipaji na mapenzi ya dhati katika uandishi wa kazi za kifasihi, hasa utanzu wa Ushairi
Mapenzi yangu kwenye uwanja wa fasihi ni makubwa sana kiasi kwamba siwezi kupoteza siku bila kuandika beti kadhaa (za kimapokeo &/ za kisasa/mamboleo) zenye maudhui yenye tija kubwa kwa jamii yetu,
zikiangazia nyanja mbalimbali za maisha.
Hii imepelekea watu wengi wa karibu wanaonizunguka kuona kuwa ni hasara kubwa kwa kazi za fasihi zilizoandikwa kwa umahiri kuishia kimyani,
Na hivyo wakanishauri nifanye haya, au kimoja kati ya haya yafuatayo;
1. Nifanye jitihada za kuonana na kampuni za uchapishaji wanisaidie kutoa diwani(kitabu cha mashairi kwa makubaliano fulani.
Au
2. Nionane na wamiliki/wahariri wa magazeti nizungumze nao vema ili nipate fursa ya kuchapisha shairi 1 lenye beti 8 au 10 gazetini kila wiki, kwa makubaliano fulani pia.
Nimeona ni mawazo mazuri kuyafanyia kazi,
Ila kutokana na kutokuwa na 'channel' pana ya masuala hayo,
Nimeona nilifikishe hili hapa JF labda naweza kupata msaada wa mawazo, mwongozo au mchango wa aina yoyote uwezao kusaidia ufanikishaji wa hili.
Nipo Dar,
Ahsante.
Pamoja na kuhamasika na kazi za waandishi mbalimbali kama vile Kezilahabi, Shaaban Robert, Mohamed Said, Andanenga, Penina Mhando, Haji Gora, Charles Mloka, Theobald Mvungi n.k,
Mimi ni kijana niliyebahatika kuwa na kipaji na mapenzi ya dhati katika uandishi wa kazi za kifasihi, hasa utanzu wa Ushairi
Mapenzi yangu kwenye uwanja wa fasihi ni makubwa sana kiasi kwamba siwezi kupoteza siku bila kuandika beti kadhaa (za kimapokeo &/ za kisasa/mamboleo) zenye maudhui yenye tija kubwa kwa jamii yetu,
zikiangazia nyanja mbalimbali za maisha.
Hii imepelekea watu wengi wa karibu wanaonizunguka kuona kuwa ni hasara kubwa kwa kazi za fasihi zilizoandikwa kwa umahiri kuishia kimyani,
Na hivyo wakanishauri nifanye haya, au kimoja kati ya haya yafuatayo;
1. Nifanye jitihada za kuonana na kampuni za uchapishaji wanisaidie kutoa diwani(kitabu cha mashairi kwa makubaliano fulani.
Au
2. Nionane na wamiliki/wahariri wa magazeti nizungumze nao vema ili nipate fursa ya kuchapisha shairi 1 lenye beti 8 au 10 gazetini kila wiki, kwa makubaliano fulani pia.
Nimeona ni mawazo mazuri kuyafanyia kazi,
Ila kutokana na kutokuwa na 'channel' pana ya masuala hayo,
Nimeona nilifikishe hili hapa JF labda naweza kupata msaada wa mawazo, mwongozo au mchango wa aina yoyote uwezao kusaidia ufanikishaji wa hili.
Nipo Dar,
Ahsante.