Mashabiki wa Yanga wengi wanaamini timu yao ni ya chama na serikali

Mashabiki wa Yanga wengi wanaamini timu yao ni ya chama na serikali

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Mashabiki wengi wa Yanga hata hawa ambao siku za hivi karibuni wamekengeuka na kupinga kitendo cha klabu yao kujiingiza katika shughuli za siasa, wanaamini kabisa kwamba klabu yao ina historia, mashirikiano na ukaribu na chama tawala pamoja na serikali.

Yanga ni kitengo cha michezo ndani ya UVCCM. Mashabiki wa Yanga toka wakiwa wadogo wanajifunza na wanafundishwa kuwa Yanga ni "klabu dola" na hauwezi kuwabadilisha hawa watu wakishakuwa wakubwa. Wanaona, wanafundishwa na kuamini Simba ni vibaraka wa nje. Huu siyo utani, ni jambo lililo ndani ya fikra zao.

Labda itokee mtu apate maarifa binafsi ya kutosha na afahamu ni jinsi gani klabu yake inatumika katika shughuli za siasa na apate upeo wa kufahamu ni jinsi gani maendeleo ya uchumi na kijamii yanakwamishwa na mahusiano hayo ndiyo hapo anaweza kufanya maamuzi mengine ila bila hivyo ndiyo unakutana na hawa wasiojitambua wanatamka "No Reform No Election" na "Free Lissu" halafu ni Yanga lia lia.



Anyway, nimekutana na hii video hapo juu. Msikilize huyu binti. Anachokisema ni mentality iliyopo ndani ya kila mwanayanga, wakubali au wakatae. Na wameikata hii video hapo mwisho, najua amesema mengi zaidi ambayo yapo vichwani mwa wanayanga wengi.

Kuitenganisha Yanga na CCM siyo jambo lililo rahisi kama mnavyodhani. Hata wasipoonyesha wazi, mafungamano haya yana mizizi mirefu sana. Magufuli alitambua nguvu ya Yanga ndani ya CCM ndiyo maana aliipiga pini na alijua inaweza kutumika na maadui wake ndani ya chama kumtikisa.
 
Huu upumbavu usirudie tena. Yanga hatuna akili za kuvukia barabara tu kama wewe.
Watu kama nyie ndiyo nimewaoongelea ambao hamjui mnashabikia timu ya aina gani. Mmepewa makuzi ambayo mlipokuja kupata akili mmekuja kukuta hayaendani na mnachoamini sasa, kwa hiyo mmebaki njia panda.

Inabidi kila mmoja wenu mkae muamue kipi ni muhimu zaidi, mapenzi ya mpira au hayo mengine. Msipofanya hayo maamuzi mtaendelea kuumiza sana mioyo yenu.
 
Mashabiki wengi wa Yanga hata hawa ambao siku za hivi karibuni wamekengeuka na kupinga kitendo cha klabu yao kujiingiza katika shughuli za siasa, wanaamini kabisa kwamba klabu yao ina historia, mashirikiano na ukaribu na chama tawala pamoja na serikali.

Yanga ni kitengo cha michezo ndani ya UVCCM. Mashabiki wa Yanga toka wakiwa wadogo wanajifunza na wanafundishwa kuwa Yanga ni "klabu dola" na hauwezi kuwabadilisha hawa watu wakishakuwa wakubwa. Wanaona, wanafundishwa na kuamini Simba ni vibaraka wa nje. Huu siyo utani, ni jambo lililo ndani ya fikra zao.

Labda itokee mtu apate maarifa binafsi ya kutosha na afahamu ni jinsi gani klabu yake inatumika katika shughuli za siasa na apate upeo wa kufahamu ni jinsi gani maendeleo ya uchumi na kijamii yanakwamishwa na mahusiano hayo ndiyo hapo anaweza kufanya maamuzi mengine ila bila hivyo ndiyo unakutana na hawa wasiojitambua wanatamka "No Reform No Election" na "Free Lissu" halafu ni Yanga lia lia.


View attachment 3455331
Anyway, nimekutana na hii video hapo juu. Msikilize huyu binti. Anachokisema ni mentality iliyopo ndani ya kila mwanayanga, wakubali au wakatae. Na wameikata hii video hapo mwisho, najua amesema mengi zaidi ambayo yapo vichwani mwa wanayanga wengi.

Kuitenganisha Yanga na CCM siyo jambo lililo rahisi kama mnavyodhani. Hata wasipoonyesha wazi, mafungamano haya yana mizizi mirefu sana. Magufuli alitambua nguvu ya Yanga ndani ya CCM ndiyo maana aliipiga pini na alijua inaweza kutumika na maadui wake ndani ya chama kumtikisa.


Huo ni ukweli usiopingika. Kama hutaki ni kiburi tu kimekujaa. Hii ni Team Dola.
 
Kuna kipindi Yanga walikuwa wakishangilia kwa kuimba CCM CCM wanapopata goli. Ilitokana na nini?
 
Mashabiki wengi wa Yanga hata hawa ambao siku za hivi karibuni wamekengeuka na kupinga kitendo cha klabu yao kujiingiza katika shughuli za siasa, wanaamini kabisa kwamba klabu yao ina historia, mashirikiano na ukaribu na chama tawala pamoja na serikali.

Yanga ni kitengo cha michezo ndani ya UVCCM. Mashabiki wa Yanga toka wakiwa wadogo wanajifunza na wanafundishwa kuwa Yanga ni "klabu dola" na hauwezi kuwabadilisha hawa watu wakishakuwa wakubwa. Wanaona, wanafundishwa na kuamini Simba ni vibaraka wa nje. Huu siyo utani, ni jambo lililo ndani ya fikra zao.

Labda itokee mtu apate maarifa binafsi ya kutosha na afahamu ni jinsi gani klabu yake inatumika katika shughuli za siasa na apate upeo wa kufahamu ni jinsi gani maendeleo ya uchumi na kijamii yanakwamishwa na mahusiano hayo ndiyo hapo anaweza kufanya maamuzi mengine ila bila hivyo ndiyo unakutana na hawa wasiojitambua wanatamka "No Reform No Election" na "Free Lissu" halafu ni Yanga lia lia.


View attachment 3455331
Anyway, nimekutana na hii video hapo juu. Msikilize huyu binti. Anachokisema ni mentality iliyopo ndani ya kila mwanayanga, wakubali au wakatae. Na wameikata hii video hapo mwisho, najua amesema mengi zaidi ambayo yapo vichwani mwa wanayanga wengi.

Kuitenganisha Yanga na CCM siyo jambo lililo rahisi kama mnavyodhani. Hata wasipoonyesha wazi, mafungamano haya yana mizizi mirefu sana. Magufuli alitambua nguvu ya Yanga ndani ya CCM ndiyo maana aliipiga pini na alijua inaweza kutumika na maadui wake ndani ya chama kumtikisa.
Acha kutusemea. Yanga haijawahi kuwa na haitokuja kuwa timu ya chama na serikali. Kinachotokea kwa miaka nenda ni kwa baadhi tu ya watu kuzitumia Yang na Simba kama madaraja ya kufikia malengo yao ya kisiasa na kiuchumi.

Ila ukija kwenye ukweli ni kwamba Yanga na Simba ni vilabu vikongwe vinavyobeba mashabiki wenye rangi, umri, itikadi, na jinsia tofauti.
 
Back
Top Bottom