Marufuku kubeba petroli kwenye vidumu

Mtumiabusara

JF-Expert Member
Nov 18, 2009
473
40
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), imepiga marufuku matumizi ya chupa za plastiki (vidumu) kuhifadhi au kubebea mafuta jamii ya petroli, kwa kuwa zina uwezo mkubwa wa kulipuka.

Pia imewataka wauzaji wa nishati hiyo katika vituo vyote vya mafuta nchini, kukataa kuhudumia wateja watakaohitaji petroli bila kuwa na magari yao vituoni kama njia ya kuwaelimisha juu ya athari za matumizi ya chupa au vidumu hivyo

Source: Habari leo


Maoni yangu

  1. Sisi tunaotumia magenereta kwenye biashara zetu na majumbani tufanye nini?
  2. Sheria hii inataka kutuaminisha kwamba mwenye gari akiishiwa mafuta ghafla basi ni mzembe. Tuchukulie mazingira kwamba umebakiwa na mafuta kidogo kwenye gari, lakini yanatosha kufika sheli iliyo umbali wa kama KM 25, then unafika na gari yako kwenye sheli hiyo, unakuta mafuta wameishiwa au hawa operate. The next sheli ni KM 25 zingine, uliskume gari mpaka huko?
 
Ukiishiwa mafuta kwenye foleni utafanyeje? Vitz yangu geji ya mafuta haisomi
 
nimemsikia akihojiwa clouds fm asubuhi hii, nilichopenda kasema kuwa:-

wenye majenereta ni vyema wakaenda nayo kujazia petrol station( hapa najiuliza haya majenereta makubwa utabeba?)

wenye magari mhakikishe magari yana mafuta ya kutosha( so dada nazjaz na vitz yako ndo ujaze mafuta sasa)
 
Wameshindwa kazi na sasa wanaanza kufuatilia 'non issues' kwenye sector ya nishati na mafuta!

Anyway, wakikomaaa itabidi tutafute zile cans za chuma!
 
nimemsikia akihojiwa clouds fm asubuhi hii, nilichopenda kasema kuwa:-

wenye majenereta ni vyema wakaenda nayo kujazia petrol station( hapa najiuliza haya majenereta makubwa utabeba?)

wenye magari mhakikishe magari yana mafuta ya kutosha( so dada nazjaz na vitz yako ndo ujaze mafuta sasa)


Kakurupuka huyu!
Kasoma kwenye vitabu badala ya kuangalia mazingira halisi
 
Wameshindwa kazi na sasa wanaanza kufuatilia 'non issues' kwenye sector ya nishati na mafuta!

Anyway, wakikomaaa itabidi tutafuti zile cans za chuma!
EWURA ni genge la wahuni na watu wanaokurupuka, eti wanasema wamefanya hivyo kwa kurejea mlipuko uliotokea DRC miaka iliyopita. hivi generator kubwa kama injini ya scania unaambiwa ulibebe mpk petrol station inakuwaje?
 
nimemsikia akihojiwa clouds fm asubuhi hii, nilichopenda kasema kuwa:-

wenye majenereta ni vyema wakaenda nayo kujazia petrol station( hapa najiuliza haya majenereta makubwa utabeba?)

wenye magari mhakikishe magari yana mafuta ya kutosha( so dada nazjaz na vitz yako ndo ujaze mafuta sasa)

Kwani siku ya Wajinga (April Fools) huwa ni mwezi mzima wa NNE? Jenereta ibebwe kupeleka Petrol Station kwa ajili ya ku-refill? Kuna watu wanatumia kufikiri!!!
 
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), imepiga marufuku matumizi ya chupa za plastiki (vidumu) kuhifadhi au kubebea mafuta jamii ya petroli, kwa kuwa zina uwezo mkubwa wa kulipuka.

Pia imewataka wauzaji wa nishati hiyo katika vituo vyote vya mafuta nchini, kukataa kuhudumia wateja watakaohitaji petroli bila kuwa na magari yao vituoni kama njia ya kuwaelimisha juu ya athari za matumizi ya chupa au vidumu hivyo

Source: Habari leo


Maoni yangu


  1. Sisi tunaotumia magenereta kwenye biashara zetu na majumbani tufanye nini?
  2. Sheria hii inataka kutuaminisha kwamba mwenye gari akiishiwa mafuta ghafla basi ni mzembe. Tuchukulie mazingira kwamba umebakiwa na mafuta kidogo kwenye gari, lakini yanatosha kufika sheli iliyo umbali wa kama KM 25, then unafika na gari yako kwenye sheli hiyo, unakuta mafuta wameishiwa au hawa operate. The next sheli ni KM 25 zingine, uliskume gari mpaka huko?

Bila kuogopa naweza kusema kwamba waliotoa tamko ni wapumbavu na hawana uhalisia wa hali ya mtanzania wa kawaida.... itabidi sasa majenereta tuyabebe kwenye bajaji kuyapeleka petrol stations

hivi hawa watu wanafikiria kwa kutumia nini?
 
Kwani siku ya Wajinga (April Fools) huwa ni mwezi mzima wa NNE? Jenereta ibebwe kupeleka Petrol Station kwa ajili ya ku-refill? Kuna watu wanatumia kufikiri!!!
afadhali umewachana live

mapumba kabisa
 
Hivi kuna marufuku iliyowahi kutekelezeka bongo? The likes of basi leny7e abiria lisiingie nao kujaza mafuta 'sheli", marufuku kuchimba kokoto kunduchi salasala, marufuku kuvuta sigara hadharani, marufuku kujtembeza bidhaa mitaani etc. etc. Just uwendawazimu.......... Kesho mtasikia JK ansema wapunguze spidi!
 
Hili ndilo tatizo la watendaji wetu kutoa maamuzi bila utafiti, kama inavyooneka kuna huko kuishiwa mafuta kwa sababu geji hazisomi ingawa hili si tatizo sana. Lakini tatizo ni kwa hao wenye majenereta makubwa.

Lakini kuna milipuko mingapi ambayo imesababishwa na hivyo vidumu? Nadhani ambacho wangezuia ni kupanda kwenye gari hasa la abiria ukiwa na hicho kidumu. Kama mtu unakaa karibu na kituo cha mafuta, ukaenda na kidumu chako kununua mafuta kwa ajili ya jenereta yako kuna tatizo gani hapo?
 
EWURA ni tooth less Dog tusiwaogope, vidumu vimesaidia majuha wa vituo vya mafuta nao wanaminya sana ujazo wa mafuta bila kuwa na vidumu tena vinavyoonyesha mafuta yamefika ujazo gani.
 
Hawa jamaa hawajaaanngalia uhalisia wa nchi yetu.

Vijijini wanatumia mashine za kukusaga nafaka zitumiazo mafuta je wabebe hizo mashine au jenereta (Angalizo jenereta nyingi hazichukui zaidi ya lita tano hizi zetu ndogo ndogo ila ni nzito kweli)
Watu kama mimi natembea na dumu la lita 20 kwenye gari yangu na mara zote najaza lita 20 kwa kidumu kisha nikifika home ndio najaza kwenye gari hii huwa naifanya ili kuepusha jamaa kuchinja mafuta yangu maana wamebobea ukitaka ya elfu 10000 una wekewa ya elfu 7000
Gari likiishiwa mafuta maana yake inabidi usukume mpaka petrol station?
 
Hivi kuna marufuku iliyowahi kutekelezeka bongo? The likes of basi leny7e abiria lisiingie nao kujaza mafuta 'sheli", marufuku kuchimba kokoto kunduchi salasala, marufuku kuvuta sigara hadharani, marufuku kujtembeza bidhaa mitaani etc. etc. Just uwendawazimu.......... Kesho mtasikia JK ansema wapunguze spidi!

Mnakumbuka level seat kwenye daladala, na speed governor je?
 
bila kuogopa naweza kusema kwamba waliotoa tamko ni wapumbavu na hawana uhalisia wa hali ya mtanzania wa kawaida.... Itabidi sasa majenereta tuyabebe kwenye bajaji kuyapeleka petrol stations

hivi hawa watu wanafikiria kwa kutumia nini?

wanatumia ile kitu kyabushaija ametwambia!!!
 
Ukiishiwa mafuta kwenye foleni utafanyeje? Vitz yangu geji ya mafuta haisomi
Ukiishiwa mafuta kwenye VITZ cc 1000 utakuwa mzembe wa mwaka na utastahili bakora kwa ubahili wako. Wapelekee mafundi watengeneze geji uwe huru.
 
EWURA nao kwa kutoa matamko watakayoshindwa kuyasimamia tumewachoka. Hivi hawajui kila dereva taxi na bajaj ana kidumu cha kuwekea mafuta kwa kuwa wanajaza lita mbili au wakijitutumua mafuta ya elfu tano ie 2.55 lts
 
Sipati picha unafika kituo cha mafuta unakuta foleni ya majenereta kama 100, bajaj 80, pikipiki 120 ongeza na magari 60. Hivi kweli huko EWURA hakuna hata mtu mmoja mwenye akili timamu kweli ?
 
Back
Top Bottom