Ndoa ni kitu kizuri saana ktk maisha ya mwanadamu, tatizo la ndoa ni pale tunapokosea ktk teuzi za wenza wetu.
Kipi tunazingatia ktk teuzi zetu za kuwapata watu wa kushirikiana nao ktk jukumu la hadharani na sirini, hakika binadamu yeyote akifanikiwa hapa daima atakuwa ni MTU kwenye furaha.
Na akishindwa hapa hataona faida ya ndoa na kuna ni mikosi mitupu, maana lazima tukubali kuwa kuna wanaume wengine hawafai kuwa MUME.
Khali kadharika kuna wanawake wengine hawafai kuwa WAKE, si makosa yao ndivyo walivyo wanamapungufu mengi ya kuvumiliana yaani hawavumiliki.mdomo si mdomo, ulevi si ulevi.
Ukahaba ndo usiseme, umbeya ndo kwao uchoyo ndo kabisaa, usafii mama wee, kutwaa kushindwa nyumbani hapana, kujali familia kujua wamekula, wanaenda shule, wamerudi nn kinahitajika kwao ni pombe pombe na kuzurura tu.
Lkn ktk khali zenu za utajiri, Uwezo wa kati au umaskini mkikaa na kuvumiliana mapungufu yenu Yale yanayovumilika na kurekebishika hakika ndoa ni kitu cha faraja.
Baada ya baba/mama yako aliyekuogesha na kushika kila eneo la mwili wako bila KINYAA, anayefuatia ni mke/mume hawa ndo ktk khali ya utu uzima wanajaliana ktk shida na Raha.
Vinginevyo subiria siku umeumwa ugonjwa kwenye kinyaa jirani zako,ndugu zako watanunua sabuni ya MCHE na kushika wote huku wakikupaka na kukumwagia maji kwa kopo lenye mshikio mrefuu.
Tuithamini ndoa, ndio chanzo cha familia bora ktk jamii watoto wanaotoka kwenye familia vumilivu huwa bora miongoni mwa jamii