Kuna information ambazo hujadisclose ili uweze kupatiwa ushauri mzuri wa kisheria.
Kwanza huu mkataba wa mauzioano umefanyika lini na mbele ya nani nikimaanisha kwamba umeshuhudiwa na wakili au la.
pili,kama marehemu baba yako alikuwa na mke na mke wake hajasaini hayo makubaliano hilo ni tatizo lingine,
Tatu, wewe kama na ndugu zako pia wapo inaonekana hamkuwa na mahusiano mazuri kifamilia kwani kama ni kweli marehemu baba yenu aliuza kwaniani hakuwashirikisha?
Nne,ili kuchukua hatua zozote za kusheria kuhusiana na mali za marehemu inabidi kuwe na msimamizi wa mirathi ya marehemu. kwahiyo kama bado hamjaenda mahakamani kufungua shauri la mirathi inabidi mfanye hivyo kwanza. na kabla ya kwenda mahakamani mfanye kikao cha ukoo ili wote kwa pamoja mkubaliane ni nani katika familia mnayemuamini ili mmpendekeze jina lake na alafu ndo aende kortini kuidhinishwa kisheria.
hebu fanyia kazi hayo mamboo machache kwanza.