Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,712
- 22,296
Jana Jumatano 04/10/2023 basi la Marangu Coach liliondoka Dar es Salaam asubuhi kama kawaida na abiria wakiwa na matarajio ya kufika Moshi kwenye saa 10 hivi bila kujua lililo mbele yao, basi lilipofika wilaya ya Bagamoyo likaharibika ikabidi spea iagizwe toka Moshi iletwe Bagamoyo! Akili mbovu.
Spea haikuletwa kwa ndege wala ungo, Moshi siyo Dar masaa yalipita Mungu Mkuu ikafikishwa na basi likatengenezwa na kuendelea na safari, likaingia mkoa wa Tanga likaharibika tena na likatengenezwa na kuendelea na safari, mpaka saa nne usiku basi lilikuwa wilaya ya Same! Usingizi ukanipata nikazimika na sijui Moshi liliingia saa ngapi ila lilifika salama, hiyo ndiyo Marangu Coach.
Spea haikuletwa kwa ndege wala ungo, Moshi siyo Dar masaa yalipita Mungu Mkuu ikafikishwa na basi likatengenezwa na kuendelea na safari, likaingia mkoa wa Tanga likaharibika tena na likatengenezwa na kuendelea na safari, mpaka saa nne usiku basi lilikuwa wilaya ya Same! Usingizi ukanipata nikazimika na sijui Moshi liliingia saa ngapi ila lilifika salama, hiyo ndiyo Marangu Coach.