SuperNgekewa
Member
- May 10, 2010
- 49
- 3
Katika stori ya "Marando ahamia Chadema" iliyoko Tanzania Daima ya 23 Jul 2010, Marando amewashambulia wabunge wa CCM wanaomuunga mkono Dr Slaa akiwaita "wadandia hoja" na kwamba lengo lao ni kutafuta umaarufu ndani ya jamii na kulalama kwamba walizua mtafaruku ndani ya CCM na kuhatarisha umoja wa CCM. Wabunge aliowashambulia ni pamoja na Fred Mpendazoe wa Kishapu, Dr Harrison Mwakyembe (Kyela), Lucas Selelii (Nzega), James Lembeli (Kahama) na Spika wa Bunge, Samuel Sitta (Urambo Mashariki), wabunge ambao ni kati ya wabunge walioonyesha uzalendo na ujasiri mkubwa kwa kuyatetea maslahi ya taifa dhidi ya wahujumu nchi hadi wengine wakakoswakoswa kuuwawa.
Fisi hawezi kubadili madoa yake. Japo ayafiche kwa ngozi ya kondoo yataonekana kwenye miguu au mkia au masikio. Kama bado kuna kipofu ambaye haoni malengo ya Marando kuhamia CHADEMA, huyo ni basi tena.
Fisi hawezi kubadili madoa yake. Japo ayafiche kwa ngozi ya kondoo yataonekana kwenye miguu au mkia au masikio. Kama bado kuna kipofu ambaye haoni malengo ya Marando kuhamia CHADEMA, huyo ni basi tena.