The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,425
Alianza lugha ya economic diplomacy au diplomasia ya uchumi.
Aliongelea demokrasia, maridhiano na mambo mengi mazuri bila kujua kuwa kumbe nyuma pazia na rohoni alimaanisha vinginevyo1
Alimwagia sifa hakuna mfano tusijue ataishia kulaumiwa hadi kufananishwa na kuitwa Idii Amina Mama!
Tulianza kusikia nyimbo, pambio na sifa lukuki za mama.
Ghafla bin vu, mambo yakaanza kubadilka japo si wengi waliogutuka. Si ni pale alipokujana falsafa ya uchawa ambayo imetuharibia taifa.
Taratibu Samia akaanza kutoa lugha za. kujisifu hadi kujiona bora baada ya kulewesha na sifa za kinafiki.
Mama mama mara mama kafanya hili. Mama kafanya llie hadi kufikia kuambiwa kuwa pesa ya miradi alikuwa aktioa mama na siyo serikali wala rais kwa niaba ya wananchi.
Ni mengi kusema ukweli. Ilifikia mahali Samia akawa Tanzania na Tanzania ikawa Samia sawia.
Toka kuvutia wawekezaji na kutafuta pesa nje na kujigamba kuwa tuna raslimali za kutosha.
Hivyo, wafadhili tuliokuwa tukiwafuatafuata na kuwarai hawatutishi tena. Who are they?
Kwa ufupi, naona kakigeugeu katika yote.
Sijui tutaishia wapi yarabi!!