Nyanswe Nsame
Senior Member
- Jul 9, 2019
- 166
- 182
Baba ampa mimba mtoto wake, abaka wengine wawili
MTU mmoja, Meshack Michael mkazi wa eneo la Nyamakokoto mtaa wa Mbulumatare halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara anashikilia na Jeshi la Polisi mkoani Mara kwa tuhuma za kumpa ujauzito mtoto wake wa umri wa miaka 13.
Pia Michael anatuhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wa kuwazaa kwa nyakati tofauti ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi Balili wilayani humo.
Mama mzazi wa watoto hao Gaudensia Meshack amesema mmewe amekuwa akiwafanyia watoto wake vitendo hivyo kwa muda mrefu.
Amesema kuwa kuna kipindi alishawahi kunfumania akiwa kitandani na mtoto wake na alipomkuta mmewe aliomba msamaha.
"Nilishawahi kumkuta kitandani na mtoto wangu na nilipowakuta walishtuka na mme wangu huyu akaomba msamaha na mimi nilimsamehe kwa kuwa mimi ni mtu wa dini na namna tulivyolelewa.
"Ukiangalia hii amekuwa akiwafanyia watoto wetu watatu na mmoja alishampa ujauzito," amesema Gaudensia.
Gaudensia ameiomba Serikali kumchukulia hatua kali za kisheria mme wake ili kuwa fundisho kwa watu wengine hatua ambayo itasaidia kukomesha vitendo hivyo katika jamii.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea Haki za wanawake na watoto la KIVULINI ,Yassin Ally ameishauri Serikali kuwa, pindi shule zitakapo funguliwa ni vyema wanafunzi wakapimwa ujauzito na magonjwa mengine.
Amesema kuwapima ujauzito na magonjwa mengine itasaidia kuwabaini watoto waliopata mimba na kuweza kuwasaidia.
Afisa maendeleo ya jamii wa mji wa Bunda Bonji Bugeni ameiomba jamii kuwafichua wale wote wanaowafanyia vitendo vya ukatili watoto wadogo.
Amesema jamii inapaswa kuacha kufumbia macho vitendo hivyo na badala yake wanapaswa kutoa taarifa kwa vyombo husika ili kuwakamata na kuwachukulia hatua.
Mkuu wa wilaya ya Bunda ambae pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya humo, Lidya Bupilipili amekiri mtu huyo kushikiliwa na Polisi na kuitaka jamii kuacha vitendo vya ukatili wa kingono kwa watoto.
"Yaani kitendo hiki kimenisikitisha sana, baba anabaka watoto wake hadi na mwingine amempa mimba, hali hii haikubaliki tutamshughulikia ipasavyo," amesema Bupilipili.
Mkoa wa Mara wenye makabila 26 ni mkoa kinara unaoongoza kuwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kwa asilimia 78.
MTU mmoja, Meshack Michael mkazi wa eneo la Nyamakokoto mtaa wa Mbulumatare halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara anashikilia na Jeshi la Polisi mkoani Mara kwa tuhuma za kumpa ujauzito mtoto wake wa umri wa miaka 13.
Pia Michael anatuhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wa kuwazaa kwa nyakati tofauti ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi Balili wilayani humo.
Mama mzazi wa watoto hao Gaudensia Meshack amesema mmewe amekuwa akiwafanyia watoto wake vitendo hivyo kwa muda mrefu.
Amesema kuwa kuna kipindi alishawahi kunfumania akiwa kitandani na mtoto wake na alipomkuta mmewe aliomba msamaha.
"Nilishawahi kumkuta kitandani na mtoto wangu na nilipowakuta walishtuka na mme wangu huyu akaomba msamaha na mimi nilimsamehe kwa kuwa mimi ni mtu wa dini na namna tulivyolelewa.
"Ukiangalia hii amekuwa akiwafanyia watoto wetu watatu na mmoja alishampa ujauzito," amesema Gaudensia.
Gaudensia ameiomba Serikali kumchukulia hatua kali za kisheria mme wake ili kuwa fundisho kwa watu wengine hatua ambayo itasaidia kukomesha vitendo hivyo katika jamii.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la kutetea Haki za wanawake na watoto la KIVULINI ,Yassin Ally ameishauri Serikali kuwa, pindi shule zitakapo funguliwa ni vyema wanafunzi wakapimwa ujauzito na magonjwa mengine.
Amesema kuwapima ujauzito na magonjwa mengine itasaidia kuwabaini watoto waliopata mimba na kuweza kuwasaidia.
Afisa maendeleo ya jamii wa mji wa Bunda Bonji Bugeni ameiomba jamii kuwafichua wale wote wanaowafanyia vitendo vya ukatili watoto wadogo.
Amesema jamii inapaswa kuacha kufumbia macho vitendo hivyo na badala yake wanapaswa kutoa taarifa kwa vyombo husika ili kuwakamata na kuwachukulia hatua.
Mkuu wa wilaya ya Bunda ambae pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya humo, Lidya Bupilipili amekiri mtu huyo kushikiliwa na Polisi na kuitaka jamii kuacha vitendo vya ukatili wa kingono kwa watoto.
"Yaani kitendo hiki kimenisikitisha sana, baba anabaka watoto wake hadi na mwingine amempa mimba, hali hii haikubaliki tutamshughulikia ipasavyo," amesema Bupilipili.
Mkoa wa Mara wenye makabila 26 ni mkoa kinara unaoongoza kuwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kwa asilimia 78.