Mapungufu ya Zitto kwenye Kampeni za CHADEMA ni yapi?

Acheni kumsakama zitto wanachadema. Kama zitto akija kuondoka kwenye chama hakika huo ndio utakuwa mwisho wa chadema.

Hapo napata tabu san kuona thinker kama wewe unaweza kuwa na mawazo kama haya hata kama zitto ataondoka CDM chama kitabaki na kitimarika zaidi na zaidi na kuhakikishia atakaye kufa kisiasa ni zito na wa si chadema.
 
jaman i do respect zitto n najua ana mchango mkubwa sana cdm na convicn power yake ni hakunaga so achen majungu yasiyokuwa na mpango
 
Tungejua kwanza intention yako mtoa mada, is it a perfomance assessment au????Majungu huwa ni ishara ya being a hater, stop hating, acha watu wafanye kazi za chama, unazoendeleza ni zile zile siasa za kuchafuana, ila ujue kuwa Zitto huwezi kumchafua maana wenye akili timamu wote wanafahamu kuwa Zitto ana mchango mkubwa sana kwenye Chadema. Yeye akiwa Mbunge na mwananchi pia, ana maisha yake binafsi ambayo yanamfanya associalize na watu wengine, yeye kumchangia mtu wa NCCR kipindi cha uchaguzi wa 2010 ilikuwa ni haki yake, ana utashi wake binafsi ambao unamfanya yeye awe hivyo unavyomuona leo. Tuache kuchafuana hivyo tutakuwa hatujengi bali tunabomoa.

Tupeane mbinu nzuri zaidi za kujenga chama na sio kubomoa na kupenyeza chuki. Tusijiandalie mazingira ya kuwa n na makundi maana makundi hayajengi bali yananbomoa.Baada ya kuyasema hayo, labda mtoa mada na wewe utuambie kwamba kwenye chama chako wewe binafsi umefanya nini? una mchango gani?

Sisi tunapoteza muda wetu ku-discuss this non-sense kwani huyo alieandika thread hii ni mtu wa CCM na ameandika hii thread kutaka tu kumchafua mheshimiwa Zitto, na kumgombanisha na wafuasi wa CDM.Let's ignore him, he doesn't deserve our valuable time!
 
Huu ni utafiti nilioufanya mwenyewe kuhusiana na harakati za zitto katika kukisadia chama
Kwanza naanza na swali
Je zitto ametoa mchango gani kwa kampeni zote za chadema?
Nikianzia historia ya karibu kwa bwana zitto, Mwaka 2010 hakutoa mchango wowote kwa chama ukianzia kigoma kwao wagombea wote wa chadema walishidwa lakini zitto alikuwa anato support kwa wabombea wetu wa ccm na NCCR

Chaguzi ndogo zote za mwaka 2011 zitto hakuwa na ushirikiano na viongozi wake pamoja na kuwa na ushawishi mdogo kwa watanzania. Uchaguzi mdogo wa busanda, kiteto etc zitto hakuwa na msaada wowote.

Uchanguzi wa madiwani Mwanza zitto ndo amechaguliwa na chama kama kamanda wa operetion shinda mwanza
lakini mimi nina uhakiki na Uchaguzi mdogo wa diwani MWANZA CCM itaibuka mshindi.

Najua Arumeru zitto hana mchango wowote


kwa maoni yako zitto ana mchango wowote kwa chadema?

umeshindwa hata kueleweka, ulikuwa unataka kusema nini?.
mbona unatumia nguvu kubwa sana na ushuhuda wa kuunga unga ili utengeneze kesi ambayo kimsingi haina tija?.
kwenye chadema hatujadili watu, tunajadili issues na sio tu kila issue tunaweza kujadili mpaka iwe na maslahi kwa umma wetu tunaojiandaa kuuongoza mapema 2015.
kwa hiyo wala hauna haja ya kuongea saana. you just go and ask watu wanasemaje kuhusu zitto then majibu utayapata.
kama ulikuwa na lengo la kutugombanisha hakika umekwama.
Go zitto GO...GO Slaa Go Go mbowe Go.
tumewapa majukumu na tunawaamini.
 
DR Kupe.nge Ni Die Hard Member wa CCM muwe munawajua watu wanakoingilia yeye anataka kuleta mtafaruku basiii
 
Zitto's mind might be embodying genuine intentions for his party and his country but the only Achilles' heel which largely condemn him is his arrogant disposition. Additionally, his informal marriage with CCM which has evidenced itself through his relationship with JK leaves people doubtful of his love of his own party. Judging by such circumstances, one should be entirely forgiven for accusing the young politician of puppetry and apple polishing.
 
mwanzisha topic ndiyo kusema ana uchungu sana na chadema, au?

maana.....
 
Walianza kuwachafua hawa siku chache zilizopita.
1.Dr w.p.Slaa

2.Freeman Mbowe

3.John Mnyika.

Hawajaishia kwa hao tu sasa wanahamia kwa Zuberi Zitto Kabwe.

Swali:
Je,Ni nani anayefuata?
 
Huu ni utafiti nilioufanya mwenyewe kuhusiana na harakati za zitto katika kukisadia chama
Kwanza naanza na swali
Je zitto ametoa mchango gani kwa kampeni zote za chadema?
Nikianzia historia ya karibu kwa bwana zitto, Mwaka 2010 hakutoa mchango wowote kwa chama ukianzia kigoma kwao wagombea wote wa chadema walishidwa lakini zitto alikuwa anato support kwa wabombea wetu wa ccm na NCCR

Chaguzi ndogo zote za mwaka 2011 zitto hakuwa na ushirikiano na viongozi wake pamoja na kuwa na ushawishi mdogo kwa watanzania. Uchaguzi mdogo wa busanda, kiteto etc zitto hakuwa na msaada wowote.

Uchanguzi wa madiwani Mwanza zitto ndo amechaguliwa na chama kama kamanda wa operetion shinda mwanza
lakini mimi nina uhakiki na Uchaguzi mdogo wa diwani MWANZA CCM itaibuka mshindi.

Najua Arumeru zitto hana mchango wowote


kwa maoni yako zitto ana mchango wowote kwa chadema?

Mbona sijawai kusikia mkifanya utafiti wa michango ya wabunge wakiwa bungeni kwa maslahi ya umma???
Then, wewe binafsi mbunge wa jimbo lako ni nani?? Kama ni profu majimarefu usinijibu tafathali.
 
Nenda mkaunde kamati teule ya kutathmini utendaji wa kikos kazi mlichounda kumchafua Zitto mmefanikiwa kwa % ngapi then ndo urudi,NB kwenye hiyo kamati usimsahau katibu wenu Saed kubenea pia mje na sababu zinazomfanya huyu dogo azidi kuwa maaruf huku mikoan as watu hawskii wala kuona kwa huyu dogo!
 
Nenda mkaunde kamati teule ya kutathmini utendaji wa kikos kazi mlichounda kumchafua Zitto mmefanikiwa kwa % ngapi then ndo urudi,NB kwenye hiyo kamati usimsahau katibu wenu Saed kubenea pia mje na sababu zinazomfanya huyu dogo azidi kuwa maaruf huku mikoan as watu hawskii wala kuona kwa huyu dogo!

Na bado wataipata,wana kiwewe sana ....Ukishaona watu wanapata hangover kabla ya tukio ujue tunastahili kufanya consolidation ya movement.Kuna watu watajuta kuingia kwenye siasa.
 
Jamani kumbukeni mtoa mada kajitanabaisha kwamba yeye ni gamba mwanzo mwisho hivyo sioni hata sababu ya kujadili thread yake,wewe ni ccm na ndo maana mchango wa zitto ndani ya chadema huwezi kuuona na wala haukuhusu.
 
Unaweza ukawa na hoja ila kwa uandishi na fikra zako watu wataanza kuhoji kama kweli wewe ni critical na umeenda shule kweli?. Binafsi nautambua mchango wa Zitto kwenye chama. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Unawezaje kupost wakati umepigwa BAN?
 
Huu ni utafiti nilioufanya mwenyewe kuhusiana na harakati za zitto katika kukisadia chama
Kwanza naanza na swali
Je zitto ametoa mchango gani kwa kampeni zote za chadema?
Nikianzia historia ya karibu kwa bwana zitto, Mwaka 2010 hakutoa mchango wowote kwa chama ukianzia kigoma kwao wagombea wote wa chadema walishidwa lakini zitto alikuwa anato support kwa wabombea wetu wa ccm na NCCR

Chaguzi ndogo zote za mwaka 2011 zitto hakuwa na ushirikiano na viongozi wake pamoja na kuwa na ushawishi mdogo kwa watanzania. Uchaguzi mdogo wa busanda, kiteto etc zitto hakuwa na msaada wowote.

Uchanguzi wa madiwani Mwanza zitto ndo amechaguliwa na chama kama kamanda wa operetion shinda mwanza
lakini mimi nina uhakiki na Uchaguzi mdogo wa diwani MWANZA CCM itaibuka mshindi.

Najua Arumeru zitto hana mchango wowote


kwa maoni yako zitto ana mchango wowote kwa chadema?

Huu si muda wa kujadili mapungufu ya mtu, kama wewe ni mwanachadema ongea na post vitu vinavyoweza isaidia chadema kushinda uchaguzi basi. Ila kwa vile nape anawatuma haya endelea na propaganda zako
 
unapoishia kuwaza wengine wanaanzia hapo.
ZITO ni mwanachama wa CDM kama wengine hata NYERERE alikuwa mwana CCM hayupo na inadunda,Chacha Wangwe alikuwa mwana CDM,KABOURU,KAFULILA,MKOSAMALI,AKWILOMBE,SHITAMBALA.
chama kipo wanasiasa wanapita tu.

Dk k umezungumza jambo ila sijui ndani yako unadhamira gani Je ni dhamaira ya kumjenga Zitto aau Kumboa Zitto.Kwa kuwa maneno yako kwa namna fulani yeye binafsi Zitto akiyafanyia kazi na kujiangalia pengine unaweza kumsaidia.Kwaa sasa baadhi ya wancdm humu ndani wanakuona wewe kama mnoko fulani,lakini kwa mwanasiasa makini [Ambako mpaka sasa Zitto ajafika kuwa mwanasiasa makini japo analazimisha kuonekana kuwa mwanasiasa makini] maneno yako yangekuwa tiba na yeye kuyatumia kama kioo chake cha kupima jinsi jamii ya waelewa wengine wanamuonaje.

Moja ya tatizo la Mwanasiasa asie makini ni kutokuwa mwepesi wa kusikia mambo hasi [Negative Issues] zinazomuhusu yeye binafsi na utendaji wa mambo yake mazima kwenye mambo ya kisiasa.Wanasiasa makini daima uwa awasikilizi sifa zao utendeaji wao ,kwa kuwa sifa kwao ndio sehemu ya wajibu wao,Mwanasiasa makini daima uwa mwepesi kusikia maadui zake wa kisiasa na wakosoaji [Critics] wake wanasemaje kumuhusu.Kwa kuwa daima wakosaji wanakuonyesha mapungufu yako na kisha mhusika kutumia nafasi hiyo kunyoosha kisha sifa zinaludi palepale kwake kwa kuwa sifa kwake yeye ni wajibu sio kiburi au ujivuni.

Mwanasiasa mashuhuri na waziri mkuu wa Uingereza haijapata kuona Sir Churchill,alikumbana na wakosoaji kibao ndani ya maisha yake wakati wa harakati zake za kisiasa ikiwemo kuwa hana kiingereza kizuri,pata picha mwingereza anaambia hana kiingereza kizuri,kwa kuwa Sir Chuchill mwanzo wa ujana wake aliishi India kama mwakilishi wa serikali ya kikoloni ya waingereza hivyo kuathirika kwenye matumizi ya kizungu chake,pamoja na yote ndiye waziri mkuu bora kupata kutokea ndani ya ardhi hiyo ya markia.

Hivyo yanayosemwa kuhusu Zitto,kama atachukulia kuwa ni majungu na kuwa yeye yuko sawa uwo wote unaosemwa ni wivu wa kike,hakika ndani ya miaka kumi ijayo itakuwa imekula kwake.Zaidi akitaka kuwa Mwanasiasa makini yampasa kweli kubadilika na kuwa REAL MAN,mtu anaetembe kwenye kile anachoamini na si kufanya mambo ndani yake kuna migongo ya watu fulani,yampasa kuwa FREE MAN,kwa kuwa mtu aliye wazi daima ujisimamia,yasemwayo yapo kama hayapo yaja.Kuna jambo moja ambalo daima sijaliona kwa zitto ni mahusiano yake na baadhi ya vijana na watendaji wenzie ndani ya CDM.Ndoto zake haziwezi kufika popote bila ya kujipanga toka chini ukiwa na watu ambao wenye macho [Anawajua] yao wanaweza kuingiza mkono kukusaidia wewe na timu yako kufikia dhamila ya ndani,ikibidi wanauwezo wa kumpa support ya watu kutumika ili kutimiza dhamila yako kama kweli wanaiona ni GENEUINE.


Lakini ili la kujifanya mimi ndio mimi,the youngest CDM .........P Material ndani ya Nchi hakika atatumika vibaya na mwisho wake uenda ukawa mbaya sana na kuathili maono [vision] za vijana wengi sana.Kuachwe kale kauarrogance na stubborness kwa chama chake.Miaka ya tisini na ushee [1994s] kulikuwa na mwanasiasa machachali sana kwa jina la Amani Waridi Kabul hakika leo ni simulizi kwa Watanzania,kiasi kuwa wananchi hata hawana kumbukumbu zake kuwa alichangia sana kuinua CDM.Lakini ndani yake kulikuwa na kale kale katabia ka arrogance na stubborness hatimae ndio hivyo sijua kama yupo Bongo au alishaludi Marekani kufundisha.

Zitto usije ukaludi vyuoni kufundisha watch out,sikia...............jitahidi sana kusikiliza.........Pia tabia ya yeye kuonekana wazi wazi na watu ambao kwa namna nyingine wananchi wa kawaida hasa wana CDM watapokea mwonekano wake huo na wahusika kama USALITI.Na hata mimi binafsi sipendi tabia hiyo kumuona mtu ambae upande wa pili namuona kama opponet [rival] kisha the other side ndani ya timu anaonekana wazi wazi anamawasiliano ya wazi na dhahiri basi ni vyema mhusika akaamua kucheza American Sytle "IF YOU CANT DEFEAT THEM JOIN THEM".

Zitto is to young na anaitajika sana kujipanga na haya mengine ya siju.............kiti na vingora avipe muda miaka ishirini toka sasa,ajipange hata vijana wenzie kwa sasa watamuelewa sana hapo na kumuona kweli kaiva.Hata JK hapo alipo hakufika hivyo amepikwa akapikwa pata picha graduate unatupwa Lindi polini kisha watu wanauchubua,wala hawana time na wewe,wanakutoa hapo wanakurusha sijui Zanzibar wanakupotezea.Hayo yote ndio uzoefu wenyewe uliomfikisha hapo na ndio kiongozi anavyopita na kufundwa.

Tusikulupuke na ujana na mengineyo,daima ujana unatufanya siku zote kuwa over ambitious na kuona kila jambo tunaweza na kumbe mambo mengine hayaitaji nguvu za ujana bali busara za ujuvi wa hali halsi ya Kidunia,ambayo mhusika uwa ameshajifunza kupitia misukosuko kadha wa kadha yakiwemo majaribu ya makusudi ili kumfanya imara na mwenye uwezo wa kuamua mambo muhimu juu ya mamilioni ya watu wanaotegemea uamuzi wake kama ndio jibu kila mwisho la utatuzi wa hatima ya jamii.

Hivyo yanayomjenga Zitto, yasichukuliwe kama chuki kwa baadhi bali kama nafasi adimu ya yeye kujijua na kuona kioo kingine kinamuonaje.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom