Mapungufu ya Taarifa ya Utendaji wa siku 78 za Rais Samia Ikulu

MenukaJr

Member
Apr 24, 2021
50
128
Maoni yangu:

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ametoa taarifa ya utendaji wa Serikali kwa siku 78 za Rais Samia Suluhu ofisini-Ikulu. Pamoja na mambo mengi mazuri, taarifa hiyo ina mapungufu kadhaa kwa maoni yangu, kama ifuatavyo:

1. Mkataba wa Gesi Da'slam-Mombasa

Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali imekosa kueleza jambo moja muhimu sana kutokana na ziara ya Rais Samia Suluhu nchini Kenya. Akiwa Kenya Rais Samia Suluhu akizungumza nyuma ya Rais Kenyetta wa Kenya alisema kuwa Serikali ya Tanzania imeingia mkataba na Kenya kwa ajili ya kusafirisha gesi kutoka Da'slam kwenda Mombassa. Gharama za Mkataba ule hazifahamiki hadi sasa.

Baada ya taarifa ile, watu wengi walihoji uhalali wa mkataba ule na haraka ile. Kwa vyovyote vile taarifa ya Serikali ilipaswa kuingiza jambo hili kwa ajili ya wananchi na kuondoa utata. Kukosekana kwake kunaendelea kuzua utata na kuimarisha tetesi kwamba tumepigwa tena!!

Ushauri: Msemaji wa Serikali afanye anavyoweza kutoa taarifa hii kwa maana ni kati ya mambo makubwa yaliyofanyika katika siku 78 za Rais na yalitegemewa kutolewa taarifa kwa umma.

2. Kodi na Mapato

Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali inasisitiza kuhusu uwiano wa makusanyo ya kodi kabla ya March na baada. Lakini ukweli takwimu zinaonesha tofauti kati ya wakati wa ubabe na wakati wa lipa kwa hiari. Mtu anayelenga kukusanya 1.99 trion akakusanya 1.67 sawa na 84.1% (March) hawezi kulingana na mtu aliyelenga kukusanya 1.61 trion halafu akakusanya 1.34 trion sawa na 83.2 (April). Tofauti ya malengo na makusanyo ni kubwa, deficit hii ikitokea kila mwezi kwa mwaka mzima tumepoteza pesa nyingi.

Ushauri: Hakuna kodi inayokusanywa kwa hiari Duniani kote. Ulipe kwa hiari usalimike au usilipe ufungwe na kufilisiwa (ubabe). Ni principle!

3. Utegemezi

Asilimia zaidi ya 70 ya taarifa ya Serikali imeonesha utegemezi. Ni kama nchi yetu imejiandaa kukopa zaidi na kutegemea misaada. Hizi dalili sio nzuri, tunaweza kurudisha nyuma jitihada zetu za kujiomboa na hatimaye kujitegemea.

Ushauri: Hatuwezi kujenga nchi kwa kutegemea misaada na mikopo. Ile spirit ya kwamba nchi yetu ina uwezo wa kujitegemea iendelee. Taifa lenye kutegemea hisani kwa kila kitu ni rahisi sana kupoteza uhuru wake.

4. COVID-19

Taarifa inaeleza kwamba Kamati iliyoundwa na Rais kwa ajili ya kufanya tathmini ya kuishauri Serikali juu ya namna ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona.

Aidha, taarifa imesema kuwa kamati hiyohiyo ya wataalam wa afya imekabidhi mapendekezo yenye mpango wa kutafuta rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa mkakati wa kukabiliana na Corona.

Ushauri:
1. Kamati ya wataalam wa afya haiwezi kufanya kazi ya kufikiria na kupendekeza kwa ufanisi mambo ya rasilimali (pesa) kwa ajili ya mkakati wa kupambana na korona. Ile timu imejaa watu wa afya, Rais aunde kamati nyingine ya wataalam wa uchumi na diplomasia ya Dunia kwa ajili hiyo.

2. Imeelezwa kuwa Baraza la Mawaziri litaketi hivi karibuni kujadili ripoti ya Kamati ya corona. Uwezekano wa kukubaliwa chanjo ni mkubwa. Kimsingi jambo hili halina maana yoyote zaidi ya kutii ITIFAKI ya Dunia, Baraza la Mawaziri likikubaliana lijenge hoja ya kuanza kufanya utafiti na kujitengenezea chanjo yetu wenyewe ili kunusuru kuifilisi nchi kwa kuiingiza katika madeni makubwa ya kughalamikia chanjo.

5. Ndoto za Idara ya Habari Maelezo

Msemaji Mkuu wa Serikali amesema anayo ndoto ya kuanzisha Televisoni (kwenye king'amuzi) kwa ajili ya kufanya vipindi vya taarifa za Serikali 24/7. Amesema pia uamuzi huo utaambatana na kufungua Redio na Gazeti la Habari Maelezo.

Kwa maoni yangu hizi ni fikra mbovu sana. Serikali yenye Televisheni ya Taifa, Redio ya Taifa na Magazeti ya Serikali haiwezi kufikiria kuanzisha Televisheni nyingine, Redio nyingine na Gazeti jingine kwa kazi hiyohiyo. Huu utakuwa upotevu wa pesa za Serikali bila sababu.

Ushauri: Pale TBC kuna vipindi vingi vya kipumbavu. Msemaji wa Serikali apendekeze maboresho pale, achukue vipindi kwa namna anayoona inafaa. Hotuba za Viongozi anazotaka kurusha zitarushwa pale, utekelezaji wa Serikali vitatangazwa pale na kila kitu. Kadhalika Redio na Magazeti. Hiyo ndio kazi vya Vyombo vya Habari vya Serikali. Hatuwezi kuwa na utitiri wa vyombo vya Serikali kwa kazi zilezile katika nchi maskini kama hii.

#TutakukumbukaDaimaJPM.
MenukaJr,
Da'slam.
 
Magufuli anaweza kweli kua alifanya blandazi nyingi ile kwenye kodi alikua sahihi zaidi ya 95%, labda hizo 5% or less ndio hizo za uonevu na mambo kama hayo. By the way Duniani hapa hakuna fairness ya 100%, haipo.

Samia yeye anakuja na mbinu ya kuwabembeleza walipa kodi, Duniani hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, hayupo. Ndio maana hata facebook pamoja na kua wanapata faida nyingi sana kwa mwaka lakini bado wamehamishia shughuli zao nchi za ulaya ambapo kodi iko kidogo. Hakuna mfanya biashara atakae lipa kodi kwa kubembelezwa, hayupo.

Mama yeye labda ata compasate na misaada na mikopo lakini tukumbuke pia hata hiyo misaada na mikopo ni kodi wa wanachi wa hizo nchi na hawajalipa kwa kubembelezwa. Nchi za ulaya zina sheria ngumu sana za kodi, ngumu sana. Ajabu sisi tunataka tubembelezane kisha tukaombe misaada ulaya.
 
Magufuli anaweza kweli kua alifanya blandazi nyingi ile kwenye kodi alikua sahihi zaidi ya 95%, labda hizo 5% or less ndio hizo za uonevu na mambo kama hayo. By the way Duniani hapa hakuna fairness ya 100%, haipo.

Samia yeye anakuja na mbinu ya kuwabembeleza walipa kodi, Duniani hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, hayupo. Ndio maana hata facebook pamoja na kua wanapata faida nyingi sana kwa mwaka lakini bado wamehamishia shughuli zao nchi za ulaya ambapo kodi iko kidogo. Hakuna mfanya biashara atakae lipa kodi kwa kubembelezwa, hayupo.

Mama yeye labda ata compasate na misaada na mikopo lakini tukumbuke pia hata hiyo misaada na mikopo ni kodi wa wanachi wa hizo nchi na hawajalipa kwa kubembelezwa. Nchi za ulaya zina sheria ngumu sana za kodi, ngumu sana. Ajabu sisi tunataka tubembelezane kisha tukaombe misaada ulaya.
Waambie bwana japokua ni wachache tutakuelewa,huwezi kuwaacha wanao washinde wanaranda randa tu mtaani bila kufanya kazi kisha utegemee kuzunguka kwa majirani kuomba misaada ya chakula ni ujuha.
 
Mleta nada , hatuna utamaduni wa kuweka mikataba wazi tangia Nchi hii ipate uhuru.
HIVI hiyo gesi Toka kule mtwara mikataba yake ipoje Kabla hatujaanza kujadili mikataba ya DAR to MOMBASA
 
Mimi nakupongeza sana, tena sana kwa mtindo wako wa kutoa hoja (udhaifu) na kutoa ushauri (nini kifanyike). Bila shaka ushauri wako utasikilizw na ikiwezekana kufanyiwa kazi maana serikali unayoiambia ni sikivu sana. Hata hivyo ulitakiwa kushukuru kwa kitendo cha kitengo husika kwa niyaba ya serikali kutoa taarifa ya utendaji kwa kipindi hiki kifupi, jambo ambalo hapo kabla hatukulizoea.
 
Kiukweli baadhi ya mambo ambayo Raisi wetu Mamá SSH hatakiwi kurudi nyuma basi ni hili la kodi

Hakuna nchi duniani ambapo mfanyabiashara anabembelezwa kulipa kodi

Tumeona Spain kwa watu mashuhuri kama wachezaji Messi na Ronaldo kwa nyakati tofauti walishafunguliwa mashtaka ya ukwepaji kodi na mamlaka za Serikali ya Spain

Sasa how come kwa Taifa letu ambalo linataka kujitegemea eti tuanze kutegemea kubembelezana kulipa kodi na wakati huo huo tukizidi kujiingiza kwenye Mtego wa utegemezi wa kimasaada na mikopo kutoka nje ktk budget ya nchi.!???

Kwanini wafanyakazi nchini wanalipa kodi (PAYE) kwa mujibu wa sheria lakini upande wa wafanyabiashara wabembelezwe!??.. Iwapi fairness hapo!??

Mamá Samia naomba usiingie ktk huu Mtego, nchi za ulaya na USA zimeendelea kwa kuweka mifumo sahihi ya ukusanyaji kodi na kuweka adhabu kali kwa wale wakwepao kodi kwani KODI NDIO MSINGI WA MAENDELEO
 
Ndio maana hata facebook pamoja na kua wanapata faida nyingi sana kwa mwaka lakini bado wamehamishia shughuli zao nchi za ulaya ambapo kodi iko kidogo.
Nchi za ulaya zina sheria ngumu sana za kodi,ngumu sana.
Sasa Facebook watasurvive vipi huko ulaya walikokimbilia?
Nalog off
 
Kwani Baba wa TAIFA letu, hayati mwalimu J.K.Nyerere alisemaje kwa nchi isiyoweza kukusanya kodi kwa watu ?

Lakini Bwana wangu Yesu Kristo alipoulizwa kuhusu Kodi alijibu Kaisari apewe yake na Mungu apewe yake yaani kodi ya Musa !

Historia ya Biblia inatufundisha mwanafunzi wa Yesu aliyeitwa Petro alikamatwa na askari wa kukusanya kodi na kukimbilia kwa Bwana Yesu naye akamwambia nenda kavue samaki na mtoe shekeli ulipe kodi kwa ajili yako Petro na mimi pia !

Hitimisho haiwezekani kukusanya KODI bila task force na kupata mafanikio kwa kizazi cha sasa kinachopenda Pesa kuliko Mungu tena cha Watanzania waliojaa roho ya umaskini !
 
Ngoja tuone style za kubembelezana kama itafanikiwa.

Binafsi kubembelezana haitotufikisha popote
 
Back
Top Bottom