Mapungufu niliyoyaona mechi ya jana Tanzania VS Sudan

Binafsi hata mimi sioni maana ya kugawa fedha kwa mchezaji mmoja wakati wapambanaji ni wengi.
Sema hata anaefanya utumbo huo kichwani hakuna kitu, hata TFF wanashindwa kuelewa hii kitu inajenga ubinafsi uwanjani ili kila mtu aonekane mwamba.

Viongozi wa TFF wengi wao ni wanafiki wakubwa na halafu wanamuogopa na kumnyenyekea huyo Mkuu wa mkoa wakiamini kuwa kinachooekana ni ukaribu wake kwa JPM 'kutawasaidia' wao....Binafsi nasema kwa moyo wa dhati kabisa TFF wamefanya kosa kubwa mno la kimkakati kumteua huyo mkuu wa mkoa kwenye kamati inayoitwa sijui ya uhamasishaji wa Taifa stars...hana sifa hizo...anaigawa Taifa Stars....katika mazingira haya Taifa Stars haitafika mbali...uwepo wake kwenye Taifa stars unawafanya hata Watanzania kugawanyika katika kuishangilia timu...Kwa kuliona hilo yeye mwenyewe alipaswa kujiondoa kwenye Taifa Stars kwani TFF hawana ubavu wa kumuondoa kwani ni watu wa kujipendekeza....Wachezaji ni kitu kimoja ...ushindi wa timu ni wa wachezaji wote...huwezi kumpa mchezaji mmoja sh. milioni 10 eti kwa kuwa alidaka penalti...vipi kuhusu waliofunga penalti...kama unataka kumpa fedha fanya hivyo kisiri siri bila kutangaza...fanya hivyo personal...Binafsi nilipokuwa naongoza mpira nilikuwa nafanya hivyo lakini kimya kimya kwa wale wanaonesha juhudi kubwa uwanjani..Ukigawa fedha hadharani kwa mchezaji mmoja unawa=demotivate wengine...

Nakumbuka upo mwaka Yanga ilimsajili mchezaji mmoja aitwaye Elisha John kutoka Coastal Union ..alikuwa ni kiungo yule nadhani namba sita kama sijakosea na alikuwa timu ya taifa...viongozi wa Yanga wakawa wanammwwagia fedha waziwazi huyo Elisha John..wachezaji wengine wa Yanga wakaona isiwe noma...wakati wa mechi wachezaji wengine wa Yanga wakawa wanampasia mipira mingi huyo Elisha ili afunge yeye aliye kipenzi wa baadhi ya viongozi wa Yanga ...Mazingira yale yakamshinda Elisha kwani aliondoka Yanga baada ya kukaa pale nadhani siyo zaidi ya miezi sita..., ...

Poleni TFF kwa kutoona mbali kuhusu suala la uendeshaji wa Taifa Stars...poleni sana kwa kweli...TFF imejaza kwenye kamati watu wanaopenda sifa na wapigaji dili...wengine hawana hata sifa .
 
mechi karibu 6, hadi sasa zimechezwa pale lakini hakuna hata moja iliyotoka na ushindi ndani ya dakika 90... timu zetu si mbovu kiasi hicho, hadi kushindwa kupata ushindi kwenye uwanja wetu wenyewe, ukilinganisha na timu pinzani...
Huu sasa ushirikina
 
Nakubaliana na wewe kwenye namba 1, 2, 3 na 4
Napingana nawewe kwenye 5 sababu kubwa watanzania wengi ni watu wenye maumbo madogo na wenye maumbo makubwa hawana mobility nzuri uwanjani.

Tatizo la maumbo madogo tunaweza kulitatua kwa kudevelope philosophy ya mpira inayotufaa kwa maumbo yetu, badala ya kutumia muda na pesa kuwatafuta kina Mwaikimba ambao ni wachache sana kwa nchi yetu academy zetu zitrain vijana kucheza possession football ya pass fupi fupi kama wanavyocheza Japan, Korea kusini na Spain na south Africa.

Hizo nchi zote wachezaji wake wana miili inayofanana au kukaribiana na watanzania kiumbo lakini ubabe wao ni kumnyima mpira mpinzani wao.

Naona hata Ndayilagije ameliona hili kwa jinsi inavyocheza timu inamiliki mpira vizuri kilichobaki ni kuwafanya vijana wake kucheza objectively kutafuta matokeo.

Kingine timu yetu haitumii vizuri set pieces unapiga dead balls nyingi lakini hazitoi matokeo chanya hili walimu wetu wanapaswa kulifanyia kazi
Kwanza niwape pole wachezaji na Watanzania wote kwa ujumla kwa matokea ya kuumiza kidogo ambayo hatukuyatarajia japo mimi binafisi nilishaona tulichemsha mwanzo kabsa baada ya kuona timu ilitoitwa ikiwa na Striker mmoja. Baadhi walipingana na mtazamo wangu. km mnavyojua tena kuna tofauti kati ya shabiki na mpenzi wa mpira. Kuna mtu akishaona wachezaji anaowapenda wameitwa baaasi atakwambia timu imekamilika. Kwa mtazamo wangu Kamgomoli hizi ndio sababu za msingi zilizoighalimu timu yetu.
1.Timu ilikosa striker muuwaji( Terminator). Chilunda anahitaji kuendelea kujifunza. Ni striker mzuri lakn anakosa uzoefu na match Fitnes.
2. Wachezaji wetu bado hawezi kucheza OBJECTIVE FOOTBAL. Bado wachezaji wetu hawana uwezo wa kumsoma mpinzani wawapo uwanjani. Kubadili mbinu kulingana na vipindi vya dk 15 za mwanzo 30, au 15 za mwisho n.k . Huwezi cheza stail moja tu mwanzo mwisho kwa timu ngumu km Sudan. Kwenye Objective football mchezaji anatambua afanye nn katika eneo gani. Wachezaji wetu wanacheza vzr sn kuanzia nyuma mpaka eneo la katikati. Wanavyozidi kukaribia eneo la 18 mbinu ni km zinawaishia. Sehemu ya kutoa pasi atabutua jishutu na kinyume chake. Mtu anatakiwa aingie nayo zaidi ndani ya 18 au 6 anapiga cross au kutoa basi butu bila hata kuangalia wenzake wako wapi na wamejipanga vp mwishowe mpira unapotea kirahisi kabsa. Kwenye Objective footbal nafasi 2 moja goli. Sasa sisi nafasi 10 hadi 15 utakuta hakuna goli hata moja.
3. Timu ya taifa kwa sasa haina beki mzuri wa pembeni kulia ukimuondoa Shomari ambaye roho yake kwasasa haipo timu ya taifa kutokana na kutelekezwa na TFF baada ya kuumia na Simba wakabeba jukumu la kuhangaika nae hadi akapona. Huo ndio ukweli japo ni mchungu kuongea.
Bonifasi Maganga licha ya mapungufu yake mengi anatatizo kubwa la msingi km beki wa pembeni, kwanza hana speed,pili hawezi kupiga cross kabsa. Jana kapiga cross nje zaidi ya mipira 4 bila kubughudhiwa na mtu. Sielewi ni sifa ipi inayofanya Ndailagije aendelee kumuita timu ya taifa kwangu ni beki wa kawaida sn.
4.Kukosa umakini kwa Idi Nado. Idi ni mchezaji mzuri ila tatizo lake kubwa na ambalo sjui km kocha amewahi kumwambia ni kukosa utulivu. Papara nyingi mno!! Ni mchezaji mwenye juhudi sn akiwa uwanjani tatizo lake kubwa hana utulivu. Anapata chances nyingi sn lakni mipira mingi anapiga nje!
5. Km taifa lazma tutafte washambuliaji wenye maumbo ya kina Mwaikimba. Baada ya Afcon kupita yalisemwa mengi sn kuhusiana maumbo ya wachezaji wetu. Jana tuliwaona Wasudani jinsi walivyo warefu.Mipira mingi wa juu waliicheza wao. Scouting ya nguvu inatakiwa ili kuwapata wachezaji wa maumbo makubwa ili tuweze kupambana na adui wa kila aina la sivyo tutaishia kusema tumeupigwa mwingi huku tumepoteza mechi.
 
Hata Hawa wakiwepo huwa sioni la ajabu taifa stars
Ukiwaondoa Samatta + Msuva ebu tuambie nani angetubeba kwenda AFCON?
Kule Afcon timu yetu ilifunga magoli mawili (2) ambayo yalifungwa na Msuva + Samatta.
Ukiyatoa magoli ya Samatta + Msuva dhidi ya BURUNDI kufuzu makundi ya Kombe la dunia ebu tuambie hawana umuhimu kweli..?
 
Mi niliwahurumia wale waliokwenda Uwanjani huku makazi yao ni nje ya mji.

Itakuwa waliumia mara saba.
Walipata taabu sana.
Nilikwenda siku Tanzania inacheza na msumbiji. Tukapigwa kimoja dk ya 1 kipindi cha kwanza.

Tulikunja nyuso hadi dk 90 zinakwisha.
Nilitembea hadi ubungo kwa mguu toka uwanja wa Taifa.

Sijawahi kwenda tena uwanja wa Taifa.
 
Huu sasa ushirikina

si ushirikina kiongozi, bali huu ndio uhalisia wa mambo..
binafsi siamini katika kutafuta mafanikio kupitia mambo ya ushirikina, na nauogopa na siupendi kamwe, ila naamini kwamba mtu anaweza tumia ushirikina kukwamisha maendeleo yangu..

tutazidi kuwalaumu makocha na wachezaji wa timu zetu katika kila mechi itakayochezwa pale uwanja wa taifa, lakini kimsingi hawahtaji hizo lawama, hawastahili kabisa kwani wanajituma katika kuupata ushindi...

lakini ushindi wao upo kwenye giza, giza ambalo limewekwa na watu ambao wanaamini katika kufanikiwa kupitia ushirikina ndani ya uwanja wa taifa,
na kimsingi hawa ndio wameleta mikosi/nuksi/gundu ndani ya uwanja wa taifa...

kama huo ushirikina hauta ondolewa uwanja taifa basi hatutasikia habari ya ushindi ndani ya dakika 90 pale kwenye uwanja wa taifa, ni aidha kufungwa ama kutoa sare na timu pinzani, hii ni mashindano ya kisoka ya kimataifa, subiri uone..
 
Back
Top Bottom