Mapinduzi yaja Tanzania

Daah! siku zote ukweli unauma sana,hii thread imenitia machungu sana,i can feel a burning sensation in my heart,kwa nini watanzania hatuna hata upeo mdogo wa kuona mapungufu lukuki ya hii serikali ya kisanii,saizi anatalii tu wananchi hatuna umeme tangu asubuhi halafu bila aibu anatoa majibu mepesi bila kujali.

Anyway mwishoni naikumbuka siku ile Dr Slaa anafanya mkutano wa kutafuta wadhamini pale jangwani mwezi wa nane mwaka jana alituambia na hapa namnukuu 'KAMA MNATAKA KUENDELEA KUISHI MAISHA MAGUMU YASIYO NA MATUMAINI CHAGUENI CCM' mwisho wa kunukuu,hapa tunavuna kile tulichopanda sina hakika kama tumejifunza kwa hili!!!
 
nakubaliana nawe kuhusu swala la kiburi kama uliyasikiliza mahojiano yake na mtangazaji wa BBC utakijua kiburi cha JK. Yaani anatoa majibu
ya kihuni na kijeuri kwa maswali mazuri na maana na anajua fika kiu ta watanzania kwenye swala la umeme lakini anajibu kiuni kama vile "serikali haina uwezo wa kuleta mvua" huku akijua wazi kuwa tatizo hili ni la muda mrefu na wataalamu wengi wamekuwa wakipiga makelele kwa miaka
mingi kuachana na umeme wa kutegemea mvua na hata alipopewa suggestions zinginena mtangazaji kuhusu jua alisema "kachukue hilo jua
uzalishe umeme kama utaweza" na "asifananishe kununua mitambo kama kununua koti ulilovaa" yaani ni majibu ya kishenzi ambayo utegemei yatolewe na mtu anayejiita Rais.
 
Yameshaanza, ile hali ya jamii ya ki -tz kuanza kuhoji masula muhimu ni hali tosha kabisa kuonesha sasa kinachosubiriwa ni kichokoo kidogo
 
najua unaipenda maana roho yako imejaa matumaini ya ukombozi, ila zilishapita nyingi km hizi, na hii itapita bila action, ngoja utaona.
Ni kweli mtanzania yeyote mzalendo wakati huu ni lazima awe na njaa ya ukombozi wa nchii hii,tatizo watanzania tumejazwa woga wa kufanya mabadiliko,eti tutakosa amani,hivi kweli kuna amani saizi bila umeme,wafanyakazi wana amani kweli na mishahara midogo,wanafunzi wa vyuo je ama wale wakulima kule vijijini wana amani kweli saizi? stupid minds,WE HAVE TO GET RID OF THIS CORRUPT GOVERNMENT AND REGAIN OUR RESOURCES@
 
Wendawazimu ninyi mlinyonya wiki ngapi? Mtu aliyenyonya vizuri hawezi kufurahia machafuko. Mbona mnafikiri kwa kutumia kamasi?
Jamani mrudisheni mirembe huyu mtu atakuwa ametoroka bado hajapona.
 
kama rostam kaondoka, basi ameona kitu kikubwa sana, the guy was very comfortable hapa nchini

this thread will live to realise its facts

Inshallah
 
Hii nchi ina usalama wa taifa wa kutosha tu, hakuna kitu kama hicho.

Mkuu kumbuka wana usalama wa taifa, wafanyakazi wa magogoni etc wote hao ni binadamu pia. So itategemea mkubwa wao anawa-handle vipi. Kama anawadharau kama mchangiaji mmoja alivyosema hapo juu; ni rahisi sana kuangusha serikali hii. Kumbuka one of the inner circle akiwa- traitor then everything is possible (Your employees can make or break you). Tuseme tu hao waliopo sijui kama kuna wazalendo wa kweli.

Wasije wakachukua hatua kama hiyo wakaingia uchu wa madaraka wakaongoza nchi kijeshi tukaingia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Ni ukweli suiopingika kwamba sasa hizi siri za Ikulu zinatoka mno na hii ni ishara either usalama wa taifa nao wamechoka na hawathamini kazi yao tena, or wanaofanya magogoni na usalama wa taifa kwa ujumla umeingiliwa na watu wasio na ujuzi. That being said katika mazingira haya mapinduzi ni very possible.

Binafsi huwa najiulizaga ni nini kingine kifanyike hawa viongozi waelewe nchi iko ICU? Watu wameshateseka saana sijui nini tena kifanyike ujumbe ueleweke kwa hawa watawala. Binafsi ningekua kiongozi kwenye serikali ya Kikwete hatua ya kwanza ningestaafu kwa manufaa ya umma na kuji-distance kabisa na yeye ili siku ikifika nisije nikabebeshwa mzigo usio wangu. Lakini sijui hawa mawaziri nao wanafikiria nini?

Kukaa kwao kimya kunatufanya tuwaone wote tu ni Jairo type.
 

Ben, democracy haijatushinda, ila tumeishinda na sasa tunaiabuse... think about it

ila kinafurahisha ni kwamba demokrasia imeanza kuamka, imegundua tunaiabuse,
...na imeanza kuwapa nafasi wanyonge wajue tunavyoibaka tena kwenye kitanda chake tena pia kwa kutumia jina lake...

demokrasia imeamka... imeamka na yeyote anayeichezea, hata awe chadema..... tunakwenda kuunda mfumo wa umma,

Umma utashikana mkono na demokrasia, na utachapa bakora za matak0 wote watakaibeza
mwisho wa siku, mabazazi wa siasa watapiga deki kwenye entrace ya democracy
wezi wa maskini watakua bize wanafuta vumbi viatu vyam amskini

siku si nyingi kwani hata mwanangu anajua dhulma, utapeli na uongo tunaofanyiwa, na haanza hata kusoma siasa/civics
 
Wendawazimu ninyi mlinyonya wiki ngapi? Mtu aliyenyonya vizuri hawezi kufurahia machafuko. Mbona mnafikiri kwa kutumia kamasi?

Ndugu hakuna anayependa machafuko. Nukuu maneno ya Mahatma Gandhi " Poverty is the worst form of violence"
 
So sad@
 

Tanzania inflation hits double digits, seen rising

Tanzania's inflation touched double digits in June for the first time since January last year, and analysts expect rising food and fuel prices to push the rate even higher in the coming months.

The country's year-on-year inflation rate was up for the eighth successive month to 10.9 percent in June from 9.7 percent in May, the National Bureau of Statistics (NBS) said in a statement on Friday.

"I was actually anticipating that the inflation rate would reach something like 12 percent in June. The rate will likely continue to rise all the way up to December because of food shortages, rising fuel prices and the ongoing power crisis," said Haji Semboja from the University of Dar es Salaam's Economic Research Bureau.

UPDATE 2-Tanzania inflation hits double digits, seen rising | News by Country | Reuters
 

Mkuu, hii ndio inanifanya nijiulize kila siku ni mtu gani mwenye uchungu na nchi hii kweli ana-msupport JK from the heart? Honestly, I just can't get it. Ukweli ni kwamba JK ame-loose touch na reality. Hana empathy ndio maana anashindwa hata ku-fake kwamba anauzunishwa na hali iliyopo. Haonyeshi humility yeyote anapo- address hizi issue; na hii ni signal kwa watanzania kwamba raisi anaelewa tatizo na ameamua kutokufanya kitu about it then what? Yaani hata juhudi kidogo yakuonyesha kwamba ana work on something hamna. I guess it is up kwa wananchi kuamua wanafanya nini for the remaining 4yrs.
 
Jk alikua na ndoto ya kuingia ikulu tu, na si kuwaletea maendeleo watanzania.
 
JK hana sapoti ya raia wema, ana sapoti ya walioshika mapoti ya chakula cha wote
 

Watanzania tuko waoga mno, inflation rate inakuwa kama Zimbabwe bado tunapiga domo! Ingekuwa kwa wachimba mafuta, tungeisha mkimbiza Vasco da Gama II siku nyingi.

Nchi imemshinda, uchumi umeporomoka vibaya na maisha yamekuwa magumu yeye anakata mawingu na sisi tunaendelea kujipa moyo-tuchukue hatua kali za nguvu ya umma!
 
Wekeni Strategies hapa kuwa sasa tunafanyaje na tuna anzia wapi tuweke record mpya sasa kila ataye andika sasa na aweke ushauri wa kusonga mbele siyo simulizi za kale.
  1. Moja Kuanzia sasa tunataka kuona wenzetu katika dola wanashirikiana nasi kwa kuanzisha sabotage kwa viongozi wote walioshiriki kuhujumu hili Taifa wanajulikana kunzia baba yao hadi watoto wao, waanze sasa wala wasingoje kesho.
  2. Kila Mtanzania mwenye uchungu na nchni hii arudishe kadi za CCM kuanzia leo wabaki hao Mafisadi tu huko, ukimjua mtu yeyote ambaye ni mwana chama wa CCM husishirikiane naye kwa lolote muone kama adui yako namba moja.
  3. Tuanzishe mfuko wa Saidi Tanzania dhidi ya Mafisadi na tuteuwe watu wapereke azimio Umoja wa Mataifa (UN) juu ya Kilio cha Watanzania na njinsi serikali iliopo madarakani inavyoendesha nchni kwa maslahi ya watu wachache huku raia wengi wakiwa katika hali ngumu, tukajenge hoja juu ya madhara ya tawala kama hizi kwa africa kwa muda mrefu sana jinsi yanavyochangia uvunjaji wa amani katika ukanda huu.
  4. Tutume watu wengine kukutana na makundi ya Libya na Misri kupata experince wao wameweza na kwanini sisi tunashindwa, lengo ni kuwa na makundi rafiki katika nchni kama hizi ambazo tuna fanana kwa matatizo, kujifunza si ujinga.
  5. Tuwaombe wabunge wote wa Upinzani wagome kuingia Bungeni hadi hii serikali yote ijiuzulu.
  6. Kama watakataa kujiuzulu ndani ya siku 60, basi wananchni wote kugome kwenda makazini nchni nzima kwa siku saba hakuna Daladala, taxi, wala mama ntilie wala ofisi za Umma; lazima wote waingie katika mgomo wa siku saba, Madereva wote waombwe wapaki Malori tote barabarani na kuyatelekeza huko.
  7. kama bado wataendelea kukatalia ndani ya ofisi za Umma tuombe kukutana na makamanda wa Jeshi la Ulinzi na tuwaeleze nia yetu njema juu ya nchni na tuwaombe ulinzi wakati wote tutakapo tumeziba barabara zote na viwanja vya ndege kwa kutoa shinikizo la mwisho.
  8. Baada ya hapo sasa tuingie Barabara sasa.
Nashauri kazi hii iratibiwe na kusimamiwa na hiyo kamati tutakayoituma kwenda UN, ambapo na mambo mengine kule UN watatakiwa pia kuelezea lengo letu la kudai uhuru kamali na kuomba kuungwa mkono. Katika kuunda kama tunaweza kupendekeza hata waliopo CCM kama wapo tunaowajuwa kuwa wanakerwa na hili jambo.
 
najua unaipenda maana roho yako imejaa matumaini ya ukombozi, ila zilishapita nyingi km hizi, na hii itapita bila action, ngoja utaona.

Nakubaliana na wewe mkuu. Thread kama hizi tunaishiaga kwenye "Problem identification" na inafungwa bila kuwa na strategy/plan yakufanya. A good strategy/plan is necessary ili wale wanaofuata upepo wasije waka-surrender before time. Kilichowasaidia Egypt ni jinsi walivyoji-organize na kukataa ku-surrender mpaka kieleweke. Niwe wazi tu kusema hili; Nionavyo mimi watu wa mikoani wana-moyo mgumu zaidi ya Dar. I have a feeling watu wa Dar watakuwa wepesi sana ku-surrender. Hata wa vijijini ni rahisi kuwa- organize kuliko Dar (ni mawazo yangu tu I might be wrong on this).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…