Beauty Eva
Senior Member
- Jul 22, 2016
- 131
- 374
Sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana, hasa linapokuja suala la siasa.
Mapenzi yetu katika siasa yanatuondolea hata uwezo wa kufikiri.
Tazama jambo hili:-
Majuzi, serikali ilizuia mikutano ya vyama vya siasa katika maeneo ambayo vyama hivyo havikushinda. Wapo watu wamefurahia sana jambo hilo ingawa wao wenyewe wanakosa haki yao ya kupata habari na haki yao ya kukusanyika.
Jana, tumesikia Tundu Lissu kakamatwa na Polisi. Baadhi ya vijana, wamefurahia jambo hilo kwa kuwa tu Tundu Lissu amekuwa mwiba kwa Chama chao.
Kijana wa Kitanzania yupo tayari kupoteza maslahi yake, kwa ajili ya Chama chake. Si Taifa lake
Kijana wa Kitanzania, yupo tayari na anaombea vyama vya upinzani vife au viwe dhaifu bila kujua kifo au udhaifu wa vyama vya upinzani kutapelekea nchi kusinyaa ktk uchumi, maendeleo n.k
Kijana wa Kitanzania hajui kuwa Upinzani wenye nguvu, huifanya serikali iliyopo madarakani isilale. Na kutokulala kwa serikali ni faida kwa wananchi.
Wakati wenye hekima na ufahamu bora, kila wakilala wanaombea Upinzani uzidi kuimarika, vijana wa Kitanzania waliorogwa na siasa, wanaombea upinzani ufifie, ufubae au ufe kabisa, ingawa kufifia kwa upinzani kutamuathiri katika maisha yake.
Kijana wa Kitanzania anasahau kabisa kuwa, Uhuru anaouona (wa vyombo vya habari, Uhuru wa kuongea), uwazi wa Uendeshaji serikali, uwazi wa mikataba, mgawanyo sawa wa rasilimali za Taifa vyote ni matokeo ya Uwepo wa vyama vingi.
Ndo maana ninajiuliza: Tumelaaniwa au ni umbumbumbu?
Mapenzi yetu katika siasa yanatuondolea hata uwezo wa kufikiri.
Tazama jambo hili:-
Majuzi, serikali ilizuia mikutano ya vyama vya siasa katika maeneo ambayo vyama hivyo havikushinda. Wapo watu wamefurahia sana jambo hilo ingawa wao wenyewe wanakosa haki yao ya kupata habari na haki yao ya kukusanyika.
Jana, tumesikia Tundu Lissu kakamatwa na Polisi. Baadhi ya vijana, wamefurahia jambo hilo kwa kuwa tu Tundu Lissu amekuwa mwiba kwa Chama chao.
Kijana wa Kitanzania yupo tayari kupoteza maslahi yake, kwa ajili ya Chama chake. Si Taifa lake
Kijana wa Kitanzania, yupo tayari na anaombea vyama vya upinzani vife au viwe dhaifu bila kujua kifo au udhaifu wa vyama vya upinzani kutapelekea nchi kusinyaa ktk uchumi, maendeleo n.k
Kijana wa Kitanzania hajui kuwa Upinzani wenye nguvu, huifanya serikali iliyopo madarakani isilale. Na kutokulala kwa serikali ni faida kwa wananchi.
Wakati wenye hekima na ufahamu bora, kila wakilala wanaombea Upinzani uzidi kuimarika, vijana wa Kitanzania waliorogwa na siasa, wanaombea upinzani ufifie, ufubae au ufe kabisa, ingawa kufifia kwa upinzani kutamuathiri katika maisha yake.
Kijana wa Kitanzania anasahau kabisa kuwa, Uhuru anaouona (wa vyombo vya habari, Uhuru wa kuongea), uwazi wa Uendeshaji serikali, uwazi wa mikataba, mgawanyo sawa wa rasilimali za Taifa vyote ni matokeo ya Uwepo wa vyama vingi.
Ndo maana ninajiuliza: Tumelaaniwa au ni umbumbumbu?