Mapenzi yanauma jamani

Jun 2, 2016
20
27
Yaan nimeachwa kwenye mataa mapenzi yanauma jamani yaani nimekaa na huyu mwanaume kwa miaka mitano nimekataa wanaume kibao ambao alikua wanani-approach wakiwa na nia njema nahisi nimechanganyikiwa sielewi wapi pakuanzia.

Nimelia hadi sauti imekauka i regret the day i said yes to him. Wanaume shikamooni sikuwai kudhani kuwa alikua na mahusiano nje, kha nimepata life time lesson wanawake wa humu muwe macho hapa nawaza ningekua nimemzalia daaah ningekua na hali gani nahisi ningechizi.

Hebu wanajammii nishaurini ntamsahauje huyu maana naona kama siwez siku ya nne leo am not myself. Yaan kadiriki kumpa simu mwanamke wake mpya waniambie kuhusu uhusiano wao mapenzi yauma jamani najiuliza nina tatizo gani jaman jaman nitamsahauje huyu.........
 
pole,ni jambo la kawaida katika mapenzi,
 
Pole sana na hakuna namna ya kuweza kujua moyo wa mtu ndani hata ukae naye miaka 10 kuna watu wana-pretend mbaya...Na usijilaumu sana kwa hilo kwani ndo changamoto za maisha hizo cha msingi usichukie wanaume wooote kwa kosa la mmoja..Piga moyo konde vumilia kaza buti tulia kidogo bila kuwa na mtu then tafuta Mr.Right wapo tena wengi mno..
 
Yaaan uzi kama huu nikiuona natamani nitoe somo lakini mda wa kuandika siupati. Natamani niongee rala akaandike!

Hivi dada una umri gani kutojua hawa wanaume? Kwanza ukipata mtu from now vaa ngozi ya kondoo tumia vizuri miezi miwili ya kwanza kiasi kwamba likiondoka huna hasara! Jutu unalionesha kulipenda kuliko hata mama yako? Vaa ngozi ya kondoo fanya mambo yako likiondoka lipe na nauri ya kulisafirisha.
 
Pole sana bibie, ila hakuna kitokeacho bila sababu kuna kitu utakuwa umemfanyia akaona hamuwezi kuendana. So bora kila mtu atafute watakayewezana japo nahisi atakuwa hajakuambia tatizo nini.

Kuna wanaume wengine huwa hatupendi kukomandiwa,kuendeshwa hata kupayukiwa na wenza wetu yawezekana ukawa na moja kati ya hayo.
 
Pole sana. Huwezi jua mungu kakuepusha na nini. Kubali na move on. Wapo wengine bora zaidi yake ni suala tu la muda
 

Kwa hii post lazima PM ijae Meseji...kazi kwako kupitia
 
Ulimnyima nn ulimsema kitu gani ulimtania nn ulifanya kitu gani mpaka akaamua hivyo?
 

Naona hekma yako ni ndogo dada,usioneshe hasira jinsi hii,matatizo huwa yapo pande zote,hata kwetu wanaume tunakutwa na changamoto kama hizi!Mshauri ajiangalie tu na ajipime!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 

Mshukuru Mungu u mzima na hamna mtoto! Sukuma maisha! Ila unakuwaje kwenye mahusiano miaka mi 5 bila ndoa? Hukuona tu dalili...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…