Mapenzi ni matamu ila ni gharama

Mapenzi ni matamu ila ni gharama

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,156
Reaction score
55,651
Mapenzi ni matamu ila ni gharama. Nimelithibitisha hili baada ya kipindi fulani kwenda kwenye mapumziko ya siku saba na mrembo wangu mwenye chura matata.

Kabla ya kuanza safari nilikuwa nimeweka bajeti na nikaiamini bajeti ile ingeweza kutosha, baada ya kufika eneo la tukio na mashamsham ya hapa na pale, mitego ya hapa na pale nikajikuta matumizi yanazidi bajeti.

Mrembo akisema baby nataka kile unajikuta unatekeleza tu, hata kama huna utajitahidi ufanikishe ili siku iende vizuri.

Mwisho wa siku nikajikuta nimetumia zaidi ya kile nilichokipanga, kweli mapenzi yanavuruga bajeti hasa kwa mtu umpendaye.
 
Daah utakuta bi mkubwa anashindia nyanya
Kweli mkuu usipokuwa makini unaweza kuharibu kila kitu;kwa upande wangu 3/4 ya mapato yangu anakuwa nayo bi mkubwa inayobaki ndio matumizi yangu binafsi
 
Kwa hiyo anapenda kusalitiwa?
ha ha ha unajua mkuu,haya maisha ya ndoa yanachangamoto zake...unaweza ukawa unahitaji tendo mara kwa mara,ila mwenzio hizo nguvu za kustahimili hiyo mikiki mikiki akawa hana;sasa ili udumishe ndoa na usilete maudhi ndani inakulazima kutafuta wa pembeni kwa ajili ya fire tu.
 
ha ha ha unajua mkuu,haya maisha ya ndoa yanachangamoto zake...unaweza ukawa unahitaji tendo mara kwa mara,ila mwenzio hizo nguvu za kustahimili hiyo mikiki mikiki akawa hana;sasa ili udumishe ndoa na usilete maudhi ndani inakulazima kutafuta wa pembeni kwa ajili ya fire tu.
Sidechick sio shida, shida ni kuwa kama mwenzi wako haridhii inakuwa tabu tena
 
Sidechick sio shida, shida ni kuwa kama mwenzi wako haridhii inakuwa tabu tena
Hii huwa ni siri ya baharia hutakiwi kumuambia aliye ndani ingawa atahisi kwa sababu ule usumbufu wako utapungua
 
Mapenzi ni matamu ila ni gharama. Nimelithibitisha hili baada ya kipindi fulani kwenda kwenye mapumziko ya siku saba na mrembo wangu mwenye chura matata.

Kabla ya kuanza safari nilikuwa nimeweka bajeti na nikaiamini bajeti ile ingeweza kutosha, baada ya kufika eneo la tukio na mashamsham ya hapa na pale, mitego ya hapa na pale nikajikuta matumizi yanazidi bajeti.

Mrembo akisema baby nataka kile unajikuta unatekeleza tu, hata kama huna utajitahidi ufanikishe ili siku iende vizuri.

Mwisho wa siku nikajikuta nimetumia zaidi ya kile nilichokipanga, kweli mapenzi yanavuruga bajeti hasa kwa mtu umpendaye.

Ivi mkuu umewahi ku note kwamba hela za kutumia na mchepuko hua hazikosekani? Yaani hata uwe umeishiwa kiasi gani, demu akijilengesha utashangaa jinsi ambavyo utatafuta hela kwa namna yoyote ile ili ukajivinjari.
 
Ivi mkuu umewahi ku note kwamba hela za kutumia na mchepuko hua hazikosekani? Yaani hata uwe umeishiwa kiasi gani, demu akijilengesha utashangaa jinsi ambavyo utatafuta hela kwa namna yoyote ile ili ukajivinjari.
Nakubaliana na wewe mkuu,utajikuta unatumia kila njia ili uweze kufanikisha lengo
 
Back
Top Bottom