Karibu Mae!
Yap, Tunawaza sawa kwenye hili.... Haipaswi kuwa hivi kabisa... acha upendo uhamue katikati yenu.... si kujitolea au zawadi ndio ziamue uelekeo wa upendo wa mmoja wapo.... hii kusaidia kwa kigezo cha kuja kuoana ndio mara nyingi inasababisha watu wanaolewa au kuoa wasiowapenda.. ila kwa sababu anamuonea mwenzake huruma.. au pengine kwa kuhesabu gharama alizoingia kwa ajili yake.
Ndio maana haishauriwi kabisa kufanya kitu chochote cha kipamoja(partnership) kama biashara, kujenga, kununua kiwanja au vinginevyo wakati wa uchumba kwa kuwa wanajua baadae mawazo ya mmoja yanaweza kubadilika the hivo vitu vikawa ndio kinachomshikilia kwenye huo uhusiano (sio mapenzi tena)
Ukitaka uishi maisha yasiyokuwa na majuto na kuumia roho kirahisi rahisi.... Jitahidi kufanya vitu kwa moyo na jitahidi kupunguza matarajio (expectations) maana kinachowaumiza wengi ni matarajio yao kutofikiwa na wale wanaotegemewa kufikia.