Mapenzi kwangu yamenikataa

Mapenzi kwangu yamenikataa

Habarin za usiku,

Kwangu jaman hali sio shwari hasa upande wa mapenzi. Nilikuwa na mahusihano na dada wakichaga wa Old Moshi kwa muda wa miaka mitatu sasa.

Sasa juzi nilimuomba meeting tukutane, akasema ana hamu ya ice cream basi nikamwambia tukutane hapo Azam ya Kariakoo yeye anakaa kigamboni. Basi mimi nikafika pale mapema piga simu hapokei, nikasema huyu atakuwa anaoga nikasema ngoja niende kwaza Mt. Joseph Posta nikasali kidogo.

Nilingia ibadani saa kumi nikatoka kumi na mbili kasoro hakupiga simu, nikaamua kuondoka nipo Fire kwenye gari ndiyo ananipigia. Eti nilikuwa mbali na simu naoga nakuja, saa moja hiyo, nikamwambia fanya mambo yako!

Nafika home namba ngeni inanicheki inaniambia wewe mshikaji najua unatembea na demu wangu, achana nae kabisa tena futa mazoea, nikaingalia ile namba WhatsApp nikakuta amewekwa dp.

Huyo demu ana mtoto na alimpata wakat mimi na yeye tuna mahusihano na siyo wangu but mapenzi yananguvu mimi nilizama wote, nikawa namhudumia mtoto aliniomb msamaha ndiyo maana kumbe yeye ananichora.

Sasa siwezi msahau halafu nampenda bado, japo nilienda kumpokonya vitu nilivyo mpa, sasa nifanyeje?
Mapenz yananguvu sana, lakin kudate na single mother ni hatari kwa afya yako, mda wowote anarudiana na baba wa mtoto wake, yan inshort kudate na singo mother ni sawa na kudandia mtumbwi wa vibwengo asee all in all accept the situation then move on, na umsahau kbsa
 
Back
Top Bottom