Mapendekezo ya sheria mpya

Mapendekezo ya sheria mpya

Toka rais Magufuli aingie madarakani kumekuwepo na kelele nyingi sana hususan humu JF za kwamba eti yeye ni mkabila na mkanda.

Kwamba eti yeye serikali yake imejaa Wasukuma na watu wengine wa kanda ya ziwa. Nimejaribu kwa muda mrefu sasa na bila mafanikio kuomba nipewe takwimu zinazothibitisha hayo madai lakini wapi!

Sasa jana na leo yameibuka ya CCM kama chama kutuhumiwa hayo mambo. Kwamba eti CCM sasa ni chama cha kikanda kwa sababu mwenyekiti mpya wa UVCCM eti ni mpwa wa Magufuli.

Mimi sijui kama kweli huyo mtu ni mpwa wa Magufuli au la. Bado nasubiri uthibitisho na/au maelezo zaidi juu ya hilo.

Ila kwa sasa ningependa kupendekeza jambo moja au mambo kadhaa, kutegemea na mtu utavyolichukulia suala lenyewe.

Ni hivi, napendekeza iundwe sheria itayokataza viongozi wa serikali, kuanzia rais hadi viongozi wengine wenye madaraka na mamlaka ya kuteua watumishi, kuteua watu wa makabila yao, imani zao za dini, madhehebu yao ya dini, jinsia zifananazo na zao, watu watokao kanda watokazo wao, marafiki zao, majirani zao, jamaa zao, na mambo mengine kama hayo ili kuondoa haya manung’uniko ya upendeleo wa hiyo misingi katika utumishi wa umma.

Yaani kwa mfano kwa mfano, kama Magufuli ni Mkristo na Mkatoliki basi ni marufuku yeye kuteua watu wa imani ya Kikristo na Wakatoliki wenzie. Vilevile, itakuwa ni marufuku yeye kuteua watu wa kanda ya ziwa....yaani hakuna cha kuteua Mnyamwezi, Msukuma, Mkurya, Mhaya, Mjaluo na wengineo wote watokeao huko hata kama wana sifa nzuri namna gani. Pia hakuna kuteua wanaume.

Ateue Wachaga, Wagogo, Wandengereko, Wapagani, Waislamu, wanawake, na wengine ambao hafanani nao kwa namna yoyote ile ukiondoa labda rangi ya ngozi tu.

Naamini kwa dhati kabisa kuwa sheria kama hii italeta usawa, italifurahisha taifa, na itaondoa kabisa ubaguzi na upendeleo kwenye utumishi wa umma.
Hatumchagui mtu kwa kabila lake ,rangi wala dini yake. Kama ana sifa ruksa, hao watu kuchaguliwa kwao ni kutokana na kura za Uvccm, hakuna uteuzi uliofanyika hapo. Mkuu angalia dhambi ya ubinafsi na ubaguzi inakuzunguka.
 
Itakuwa shuguli. Inasemekana 25% ya watanzania ni wasukuma/wanyamwezi, ndo maana wanasemaga huwezi shinda uraisi nchini bila kura za Hawa jamaa. Watoto wamjini wanawaita wachina wa Tanzania. Hakuna utakako katiza bila kukutana nao. Na uzuri kwa vile wako nyuma kidogo kielimu, wanaendelea kuzaa kwa idadi na kasi ile ile ya mabibi zetu.

Kwahiyo hizi kelele za ukabila nadhani ni chama fulani kilichoundwa kwa misingi ya ukabila kinajaribu kusema kuwa sio wao tu, hata wale pia ni wakabila.

Hivi nisehemu gani Tanzania ambapo haipati teuzi? Mpaka Handeni kwa mara ya kwanza imetoa naibu waziri. Labda kwetu tu kule Nkasi.

Hivyo Kama takwimu za idadi ya Hawa watu ni sahihi, inamaana kwa kila wateule 4, 1 atakuwa msukuma/mnyamwezi. Haijalishi mteuzi ni msukuma au mchaga.

Hata kabla ya Magu walikuwepo japo hawakuvuma.

Uzuri wao ni wachapa kazi na hawana asili ya tamaa kama wale jamaa zetu. Tuache fikra potofu za kuendekeza ukabila. Tuwahukumu kwa matokeo ya kazi zao.
I concur!! Na makofi juu(claps not slaps)
 
Uteuzi wa General Mabeyo hauhusiani na upuuzi unaotajwa/unaosemwa.....isipokuwa ni kweli walikuwepo Senior Generals kwa Mabeyo...wao walipewa ubalozi
Ebu tutajie hao seniors wa Mabeyo, utasaidia sana. Usije ukachanganya na polisi
 
Toka rais Magufuli aingie madarakani kumekuwepo na kelele nyingi sana hususan humu JF za kwamba eti yeye ni mkabila na mkanda.

Kwamba eti yeye serikali yake imejaa Wasukuma na watu wengine wa kanda ya ziwa. Nimejaribu kwa muda mrefu sasa na bila mafanikio kuomba nipewe takwimu zinazothibitisha hayo madai lakini wapi!

Sasa jana na leo yameibuka ya CCM kama chama kutuhumiwa hayo mambo. Kwamba eti CCM sasa ni chama cha kikanda kwa sababu mwenyekiti mpya wa UVCCM eti ni mpwa wa Magufuli.

Mimi sijui kama kweli huyo mtu ni mpwa wa Magufuli au la. Bado nasubiri uthibitisho na/au maelezo zaidi juu ya hilo.

Ila kwa sasa ningependa kupendekeza jambo moja au mambo kadhaa, kutegemea na mtu utavyolichukulia suala lenyewe.

Ni hivi, napendekeza iundwe sheria itayokataza viongozi wa serikali, kuanzia rais hadi viongozi wengine wenye madaraka na mamlaka ya kuteua watumishi, kuteua watu wa makabila yao, imani zao za dini, madhehebu yao ya dini, jinsia zifananazo na zao, watu watokao kanda watokazo wao, marafiki zao, majirani zao, jamaa zao, na mambo mengine kama hayo ili kuondoa haya manung’uniko ya upendeleo wa hiyo misingi katika utumishi wa umma.

Yaani kwa mfano kwa mfano, kama Magufuli ni Mkristo na Mkatoliki basi ni marufuku yeye kuteua watu wa imani ya Kikristo na Wakatoliki wenzie. Vilevile, itakuwa ni marufuku yeye kuteua watu wa kanda ya ziwa....yaani hakuna cha kuteua Mnyamwezi, Msukuma, Mkurya, Mhaya, Mjaluo na wengineo wote watokeao huko hata kama wana sifa nzuri namna gani. Pia hakuna kuteua wanaume.

Ateue Wachaga, Wagogo, Wandengereko, Wapagani, Waislamu, wanawake, na wengine ambao hafanani nao kwa namna yoyote ile ukiondoa labda rangi ya ngozi tu.

Naamini kwa dhati kabisa kuwa sheria kama hii italeta usawa, italifurahisha taifa, na itaondoa kabisa ubaguzi na upendeleo kwenye utumishi wa umma.
Rais ukishaguliwa usiwe na mamlaka ya kuteua yeyote. Itakuwepo mamlaka ya kukuchagulia wasaidizi wako baasi> SO SELFISH!! khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!! hadi kutapika rubbish
 
Fact: Mabeyo alikuwa ndo mnadhimu mkuu wa JWTZ kabla ya kuteuliwa kuwa CDF.

Fact: Mabeyo alikuwa luteni jenerali alipokuwa mnadhimu wa majeshi.

Fact. Mabeyo alipandishwa cheo na kuwa jenerali alipoteuliwa kuwa CDF.

Fact. Mabeyo hakutoka kuwa meja jenerali na kuwa jenerali.
Duh. Yaani hawa jamaa wa propaganda wanavyopigia kelele na kuyakuza mambo ya uzushi hadi inasikitisha. Kwa akili zao hizi sishangai wanavyoshindwa kuyaona mapungufu makubwa ya chama chao!!
 
Thats nosense

Hujui hata maana ya kusema

Watu wote wana haki mbele ya sheria

(Equality before the law, that is a contitutional right)

huwezi hata siku moja ukatunga sheria ya kubagua watu

for sure your mind had gotta a serious P.
 
Back
Top Bottom