Katiba mpya ni lazima iyakinishe vyeo vya watendaji wakuu wa serikali, suala la awepo makamu wa raisi ama la, litemegemee umuhimu wa kiutendaji, katiba ni lazima iweke majukumu kamili ya kiutendaji, kwa sasa yupo yupo tu kama kumwakilisha raisi kwenye mambo ya kiitifaki hana mamlaka kamili kiutendaji kiserikali hata kama yapo hayaonekani kwa madaraka aliyonayo sasa sidhani kama anaweza hata kumfukuza kazi mkurugenzi wa wilaya. Hii nafasi ina umuhimu wake sana kumsaidia raisi kiutendaji tatatizo lilipo ni kuwa raisi wetu si rahisi kukubali kupunguza madaraka yake, labda katiba iweke wazi kama makamu wa raisi ni lazima atoke Zanzibar, hivi sasa tuna mgongano wa katiba zetu iweje raisi wa Zanzibar awe waziri kwenye muungano? Je mkubwa kimadaraka ni nani; ni lazima siasa za kiccm tuweke pembeni na tuangalie maslahi ya Taifa, suala la mgombea mwenza atoke wapi viachiwe vyama vyenyewe viamue, ili kuboresha muungano wazinzibar wapewe nafasi ya kuujadili kama wanautaka au la; inaonekana tunawalazimisha wameshasema Zanzibar haitachangia gharama za katiba mpya; hiyo itakuwa ni jukumu la serikali ya muungano; sasa kama sio kujichanganya wao ni kitu gani? je wao hawamo kwenye muungano tunaoungelea?
Chama
Gongo la Mboto DSM.
Chama
Gongo la Mboto DSM.