Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 6,318
- 8,228
Mawaziri na Spika: Waziri mkuu, mawaziri wa wizara, spika wa bunge na naibu spika wa bunge wanatakiwa wasiwe wabunge.
Matokeo ya uchaguzi Mkuu: Matokeo ya uchaguzi mkuu yahojiwe mahakamani.
Tume huru ya uchaguzi: Kuwepo na tume huru ya uchaguzi isiyoteuliwa.
Tume ya uchaguzi iwe ni taasisi inayohusisha watu wenye taaluma hiyo na waajiriwe kama wafanyakazi wengine wa umma mfano hakimu, dakitari mwalimu n.k na isiwe tume yenye watendaji wanaoteuliwa.
Mwanasheria mkuu, jaji mkuu na viongozi wengine wa mahakama wasiteuliwe, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na viongozi wengine wa tume wasiteuliwe, mawaziri wasiteuliwe, wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe
Mgombea binafsi: Mgombea binafsi awepo.
Kuwawajijibisha wabunge: Wananchi wawajibishe wabunge wavivu.
Uhuru wa makama: Mahakama iwe huru kazi zote za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama upatikanaji kwa majaji, jaji mkuu na mwanasheria mkuu wa serikali.
Elimu ya kiongozi: Elimu ya diwani iwe kuanzia sitashahada (diploma). Elimu ya mbunge iwe kuanzia shahada (degree). Elimu ya waziri iwe kuanzia shahada ya uzamili (masters).
Muda wa kuwa kiongozi: Muda wa kuwa diwani uwe mwisho miaka 10, Muda wa kuwa mbunge uwe mwisho miaka 10. Muda wa kuwa waziri uwe mwisho miaka 10.
Waziri mkuu na mawaziri wa wizara: Waziri mkuu na mawaziri wa wizara wasiwe wabunge bali wawe wasomi wenye elimu kuanzia shahada ya uzamili wenye uzoefu na kazi za wizara husika na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.
Mawaziri wa wizara: wawe na elimu, maarifa, uzoefu na ujuzi wa wizara watakazofanyia kazi.
Sera ya Elimu: Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba ili hata akija kiongozi mwingine asiweze kuibadirisha. Watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote ibezi kwenye technical education.
Sera ya Afya na Bima: Tuwe na sera ya bima kwa watu wote ambayo iwe ni lazima kwa kila mtu. Utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu. Na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dola moja kwa siku na hao wapewe bima bure ndani ya katiba.
Wala Rushwa na Mafisadi: Ingizwe adhabu ya kifo kwa wala rushwa na Mafisadi.
Mifuko ya Hifadhi ya jamii: Mifuko ya Hifadhi ya jamii hasa sekta binafsi kama NSSF isisimamiwe na Serikali bali isimamiwe na vyama vya wafanyakazi.
Fao la kujitoa: Fao la kujitoa iwe haki ya mfanyakazi.
Karibuni kwa maoni kama unanyongeza tafadhari ongezea hapa au kama kuna kitu nimesahau au hakipo sawa ongezea.
Matokeo ya uchaguzi Mkuu: Matokeo ya uchaguzi mkuu yahojiwe mahakamani.
Tume huru ya uchaguzi: Kuwepo na tume huru ya uchaguzi isiyoteuliwa.
Tume ya uchaguzi iwe ni taasisi inayohusisha watu wenye taaluma hiyo na waajiriwe kama wafanyakazi wengine wa umma mfano hakimu, dakitari mwalimu n.k na isiwe tume yenye watendaji wanaoteuliwa.
Mwanasheria mkuu, jaji mkuu na viongozi wengine wa mahakama wasiteuliwe, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na viongozi wengine wa tume wasiteuliwe, mawaziri wasiteuliwe, wakuu wa mikoa na wilaya wasiteuliwe
Mgombea binafsi: Mgombea binafsi awepo.
Kuwawajijibisha wabunge: Wananchi wawajibishe wabunge wavivu.
Uhuru wa makama: Mahakama iwe huru kazi zote za mahakama ziachwe zifanywe na mahakama kama upatikanaji kwa majaji, jaji mkuu na mwanasheria mkuu wa serikali.
Elimu ya kiongozi: Elimu ya diwani iwe kuanzia sitashahada (diploma). Elimu ya mbunge iwe kuanzia shahada (degree). Elimu ya waziri iwe kuanzia shahada ya uzamili (masters).
Muda wa kuwa kiongozi: Muda wa kuwa diwani uwe mwisho miaka 10, Muda wa kuwa mbunge uwe mwisho miaka 10. Muda wa kuwa waziri uwe mwisho miaka 10.
Waziri mkuu na mawaziri wa wizara: Waziri mkuu na mawaziri wa wizara wasiwe wabunge bali wawe wasomi wenye elimu kuanzia shahada ya uzamili wenye uzoefu na kazi za wizara husika na wapitishwe na bunge na mahakama kwa kufanyiwa vetting na kuangaliwa juu ya record zao za uko nyuma.
Mawaziri wa wizara: wawe na elimu, maarifa, uzoefu na ujuzi wa wizara watakazofanyia kazi.
Sera ya Elimu: Sera ya Elimu iwekwe kwenye katiba ili hata akija kiongozi mwingine asiweze kuibadirisha. Watanzania waweze kusoma bure elimu ya msingi na sekondani na elimu yote ibezi kwenye technical education.
Sera ya Afya na Bima: Tuwe na sera ya bima kwa watu wote ambayo iwe ni lazima kwa kila mtu. Utengenezwe mfumo wa kila raia kuwa na bima ya bei nafuu. Na tuwatambue masikini wote wanaoishi chini ya dola moja kwa siku na hao wapewe bima bure ndani ya katiba.
Wala Rushwa na Mafisadi: Ingizwe adhabu ya kifo kwa wala rushwa na Mafisadi.
Mifuko ya Hifadhi ya jamii: Mifuko ya Hifadhi ya jamii hasa sekta binafsi kama NSSF isisimamiwe na Serikali bali isimamiwe na vyama vya wafanyakazi.
Fao la kujitoa: Fao la kujitoa iwe haki ya mfanyakazi.
Karibuni kwa maoni kama unanyongeza tafadhari ongezea hapa au kama kuna kitu nimesahau au hakipo sawa ongezea.